Posts

Showing posts from July, 2010

HIVI NDO ILIVYOKUWA FIESTA KUJIPANGUSA MUSOMA

Image
Hivyo ndo ilivyokuwa jana katika swala zima la kujipangusa pande za Musoma,leo watu wa Mwanza wanajipangusa leo na kesho pia......... picha hizi ni kwa hisani ya michuzijr

DR. SLAA AWASILI MUSOMA MKOANI MARA KWA KISHINDO. MKUTANO WAKE KUFANYIKA LEO JIONI.

Image
MGOMBEA URAIS KWA TIKETI YA CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA) LEO MCHANA AMEPATA MAPOKEZI YA NGUVU SAMBAMBA NA MAANDAMANO TOKA UWANJA WA NDEGE MUSOMA HADI HADI HOTEL ALIPO FIKIA. MKUTANO WA CHAMA HICHO UNATARAJI KUFANYIKA LEO SAA 10:00 KATIKA VIWANJA VYA MUKENDO MSOMA MJINI. PICHANI WADAU WA CHAMA HICHO WAKIISUBIRI NDEGE INAYO MLETA IPATE KUTUA KIWANJA CHA NDEGE MUSOMA HUKU WAKIWA WAMEJIPANGA MSTARI KUMPOKEA MGOMBEA HUYO ALIYETANGAZA NIA. habari hii ni kwa hisani ya blog ya www.gsengo.blogspot.com

Clouds FM Live ndani ya musoma jioni hii

Image
Watangazaji wa Clouds FM 88.4 wakiruka hewani Live jioni hii kati kati ya mji wa Musoma kuhamasisha wakazi wa mji huo kujitokeza kwa wingi kwenye tamasha la Fiesta jipanguse 2010,ambalo linafanyika ndani ya Musoma hotel kwa kiingilia cha 5000/= tu kwa kila kichwa usiku wa leo,ambapo mdhamini mkuu wa tamasha hilo ni kampuni ya bia ya Serengeti a.k.a Mfalme wa raha kamili anayedumu zaidi.Kutoka kulia ni Ruben Ndege a.k.a Ncha Kali,Msanii wa kizazi kipya Godzila a.k.a mkali wa Salasala,Fatma Hassan a.k.a Fetty pamoja Mully B.

REST IN PEACE MOM

Image
MY MOM GODRIVER POTI NYANJA Leo imetimia mwaka mmoja tangu mama yetu kipenzi atutoke mnamo tarehe kama yaleo na mwezi kama huu mwaka jana,wanao bado tunakukumbuka sana mama,upumzike kwa Amani.

HaPpY bIrTHdAY Nyanja

Image
Nyanja kelvin Poti Leo ni siku yangu ya kuzaliwa nawashukuru wadau wangu wote tuko pamoja,natimiza robo karne. twendelee kushirikiana kwa pamoja kama kawaida

NAIPENDA SANA........

Image
Baada ya kombe la dunia macho na masikio yetu tunayarudisha katika ligi inayopendwa sana dunianI,na hii si nyingine bali ni ligi kuu ya Uingereza na mimi kama kawaida yangu huwa sifichi mapenzi yangu kwa timu yangu ninayoipenda sana ya Manchester United. soon ligi itaanza itakuwa ni mwezi wa 8...so info zaidi utazidi kuzipata kutoka katika blog yako.

Utata ujenzi barabara ya Serengeti

NDOTO ya Serikali na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutumia mradi wa ujenzi wa barabara ya kuunganisha mikoa ya Arusha na Mara inayopita katikati ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti kama mtaji wa kuombea kura kwa wananchi wa mikoa ya Kanda ya Ziwa katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu iko katika hatari ya “kuyeyuka” kutokana na jumuiya za kimataifa kupinga ujenzi huo. Barabara hiyo yenye urefu wa kilomita takribani 421 inatarajiwa kuanza kujengwa mwaka 2012 na tayari watalaamu wa upembuzi yakinifu wameanza kazi wakitarajiwa kuikamilisha mwishoni mwa mwaka huu. Taarifa kwamba ujenzi wa barabara hiyo kuwa “ulimbo” wa kura kwa wapiga kura wa Kanda ya Ziwa zinathibitishwa na kauli ya hivi karibuni ya Waziri wa Maliasili na Utalii, Shamsa Mwangunga. Waziri huyo amekaririwa na vyombo vya habari akisema ujenzi wa barabara hiyo kupitia Hifadhi ya Serengeti uko palepale kwa kuwa ni sehemu ya utekelezaji wa Ilani ya uchaguzi ya CCM. “Barabara hiyo ni ahadi iliyoko kwenye Ilani ya CCM kwa wapiga kura wa Kand

Man United yambakisha Rooney

Image
wayne Rooney MKURUGENZI wa Manchester United, David Gill, atakutana na Wayne Rooney, kwa ajili ya kufanya mazungumzo ya kuongeza katika klabu hiyo. Wakati nyota huyo kabakisha miaka miwili katika mkataba wake, uongozi wa United, umepanga kumuongezea mkataba mchezaji huyo. Juzi, United, ilitangaza kukubaliana na Nemanja Vidic, kubaki klabuni hapo kufuatia taarifa kuwa angeweza kuhamia Real Madrid au AC Milan. Rooney, atafanya mazungumzo na United baada ya kurejea mapumzikoni na atakuwa mchezaji wa pili kusaini mkataba mpya na klabu hiyo. "Mpango wa sasa ni kukutana na Wayne na washauri wake pindi atakaporudi likizo kwa lengo la kuzungumzia mkataba mpya,” Gill, aliwaambia waandishi wa habari. "Aliwahi kusema na sisi tuliwahi kusema kuwa, tunahitaji kukutana na kulizungumzia suala hili, ili tuendelee kumpa maisha mapya hapa United. "Ukiangalia malengo yake na jinsi anavyojituma katika klabu hii ni wazi mpango huu utafanikiwa."?

Serikali kudhibiti wizi wa pamba Bunda

SERIKALI imesema katika msimu wa ununuzi wa zao la pamba ujao wa mwaka 2011, itaagiza mizani ya kisasa, ili kudhibiti udanganyifu kutoka kwa wafanyabiashara wa zao hilo ambao wamekuwa wakipunja wakulima kwa kutumia mizani ambayo haina ubora. Pia katika msimu ujao serikali itazikusanya mizani yote ya sasa kutoka kwa wanunuzi hao wa zao la pamba, ili zisitumiwe tena katika kupimia zao hilo. Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Stephen Wassira, alieleza hayo mwishoni mwa wiki katika Kijiji cha Kung’ombe wilayani hapa wakati akizungumza na wananchi kwenye mkutano wa kampeni za kuwania kuteuliwa kwenye kura za maoni za wananchama wa CCM katika Jimbo la Bunda. Alieleza hayo baada ya kuulizwa na mwananchi kuhoji serikali imejipanga vipi katika kukabiliana na tatizo la wanunuzi wa zao la pamba wanaotumia mizani mibovu kwa lengo la kuwapunja wakulima. Akijibu swali hilo, Wassira alisema serikali imeweka mipango madhubuti wa kuhakikisha wakulima wa zao la pamba hawafanyiwi udanganyifu wa aina

Kanisa Katoliki latoa tamko kuhusu Dkt. Slaa

KANISA Katoliki limekuja juu na kukanusha tuhuma zinazoelekezwa kwa kanisa hilo kuwa limemtuma Dkt. Willibrod Slaa kuwania urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 31, mwaka huu. Vile vile kanisa hilo limesema kuwa Kanisa Katoliki si taasisi inayojihusisha na harakati za kisiasa wala si chama cha kisiasa kinachohusika kwa namna yoyote ile na uteuzi wa wagombea wa nafasi mbalimbali. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Rais wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania, Mhashamu Jude Ruwa'ichi alisema kuwa habari za kanisa hilo kuhusishwa na Dkt. Slaa katika harakati zake za siasa zimelenga kulichafua kanisa na kulipunguzia heshima ndani ya jamii. "Tunapenda Watanzania wenzetu waelewe kuwa Kanisa Katoliki halijamtuma wala halitamtuma mtu yeyote kugombea nafasi ya uongozi kwa jina la kanisa, kwani si jukumu lake...kanisa litaendelea kuhubiri upendo, haki, amani, mapatano na mshikamano na litaendelea kutoa mchango wake n

Mwasiti, Hussein Machozi, Lina, Adam - Bus breakdown - Fiesta 2010

Find more videos like this on TEEN TZ

Mchungaji agoma kuzika majambazi

Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), amekataa kushawishika amzike Kikristo moja ya Majambazi kati ya wawili waliyouawa na Jeshi la Polisi na kukaa kwenye jokofu la Hospitali ya Mkoa wa Dodoma kwa siku saba. Jambazi hilo linalojulikana kwa jina la Gerald Machange (26), na lenzie Paulo Yohana (18), ya Chang’ombe mkoani hapo, yaliuawa baada ya kujaribu kuwatoroka Polisi toka kwenye gari yalipokamatwa na vitu walivyokuwa wakiiba kwenye Hotel ya Emirates. Akiwafariji wafiwa na Waombolezaji nyumbani kwa wazazi wa jambazi Machange, Mchungaji Naftari Njavike wa KKKT Chinangali aliuambia umati uliofurika msibani kwamba, Neno la Mungu linatuasa kuwa, ‘Niangalieni mimi Mkaokolewe’; Lakini watu wameaacha kumuangalia Mungu na badala yake wanaangalia vitendo viovu. “Nawataka mfahamu, Kanisa halina nafasi ya kutetea tabia mbovu za namna hiyo, zinazofanywa kwenye jamii zenye lengo la kuwakosesha amani, utulivu, mshikamano, na tija ya wananchi katika maendeleo yao ya kila si

Miss Open University of Tanzania Leo

Image
Warembo washiriki wa Shindano la Miss Open University of Tanzania Excellence 2010,wakiwa wamejipanga kwa ajili ya picha.Shindano hilo linatarajia kufanyika leo katika ukumbi wa Chuo Kikuu Huria (Open University of Tanzania) kilichopo Kinondoni Biafra.Warembo wanaoshiriki katika shindano hilo ni Kiran Mohamed,Bahati Abdallah,Christine Justine,Veronica Allan,Salma Ally,Rehema Faraji,Zahara Muhidin,Nancy Muray,Mariana Kavishe,Jacqueline Mwombeki na Glory Mosha.FM Academia wazee wa Pamba ndio watakaopendezesha shindano hilo kwa upande wa burudani.Shindano hilo linakuja kwa udhamini wa Vodacom Tanzania,Times Fm,Clouds Fm na Mount Moriah Hotel iliyopo Kinondoni

MUSOMA KUMEKUCHA SASA

Image
Augustin Mgendi Anaitwa Augustin Mgendi ni mwana habari aliyesoma Royal jijini Dar es Salaam na sasa ni mtangazaji wa redio Victoria fm ya mjini Musoma na mwakilishi wa gazeti la Jambo Leo mjini Musoma. Umati wa wakazi wa kata ya Mkendo mjni Musoma ambao jana walijitokeza kuwasikiliza wagombea wa CCM wanaoomba ridhaa kuwakilisha bendera ya CCM katika nafasi ya ubunge katika jimbo la Musoma. Picha ya wagombea wa ccm wanaomba ridhaa ya wana CCM wenzake wa kwanza kulia ni Deus Munasa na Mbunge anayemaliza muda wake Vedastus Mathayo. Ni mmoja wa wagombea wa nafasi ya ubunge katika chama cha Mapinduzi CCM ambaye amesoma Korea na sasa amerudi nyumbani kuleta mabadiliko anaitwa Eiud Esseko Tongolo ambaye ana kauli mbiu ya Changamoto ya mabadiliko Musoma (Challenge Musoma Change). Picha ya katibu wa CCM mkoani Mara akiwa ofisini anaitwa Ndekubali Ndeng'aso Habari hii na picha ni kwa hisani ya mdau Augustin Mgendi

HAPPY BIRTHDAY B-DOZEN

Image
'B-dozen' Leo ni Birthday ya Hamisi Mandi aka 'B-dozen' mtangazaji maarufu wa kipindi cha XXL cha Clouds FM,sijui unafikisha miaka mingapi lakini all in all tunakutakia maisha marefu brother.HaPpY bIrThDaY 'B-dozen'.

BBA All Star-Mwisho Mwapamba mjengoni tena

Image
Mwisho Mwapamba BBA All Star Ni habari nyingine Ilianza Big Brother Africa mwaka 2003, ikaja Big Brother Afrika II (2007), ikaja Big Brother III (2008), baadaye Big Brother Revolution (2209), hata hivyo, zote zinatajwa ni tisa, 10 na itakayofunika ni ya 2010 ambayo inakwenda kwa jina la Big Brother All Stars. Sababu ambayo inatajwa kuifanya Big Brother mwaka huu kuwa ya kipekee ni uamuzi wa kuwachukua mastaa waliong’ara kwenye fainali zilizopita na kuwapa nafasi ya kuingia tena mjengoni ili kushindana tena. Tanzania imeshiriki mashindano hayo mara zote, na kufanya vizuri zaidi mwaka 2007, pale Ricahrd Bezuidenhout aliponyakua taji na kujibebea kitita cha Dola za Kimarekani 100 ambazo kwa ‘chenji’ ya wakati huo zilikuwa shilingi 130,000,000. Mwanga wa mafanikio kwa Tanzania kwenye mashindano hayo, ulioneshwa mapema mwaka 2003, pale Mwisho Mwampamba ‘Mr. Morogoro’ aliposhika nafafasi ya pili, nyuma ya Cheris Makubale wa Zambia. Mwaka 2008, Tanzania iliwakilishwa na Latoya Lyakurwa ambaye

MAMIA WAJITOKEZA KUMSIDIKIZA VINCENT NYERERE KURUDISHA FOMU

Image
Vincent Nyerere pamoja na Kambarage na wananchi wa jimbo la musoma mjini Wakazi wa jimbo la Musoma mjini leo wamejitokeza kwa wingi wakimsidikiza mgombea Ubunge wa jimbo la Musoma mjini kwa tiketi ya chama cha CHADEMA bwana Vincent Nyerere wakati wa urejeshaji wa fomu ya kugombea ubunge kwa tiketi ya chama hicho.wadau wote wa blog hii wanakutakia kila la kheri katika kuuletea mkoa wetu Maendeleo.

Manchester United Kits 2010/2011

Image
Manchester new jersey Share all new kit debates/images in here. Before I start, you should realise that I am not claiming these to be real or official, but have found them on the internet in various places, and as you might expect, there has been much discussion!

BIG BROTHER AFRICA 2010 KUANZA KESHO

Image
Lile shindano maarufu la Big Brother Africa kwa mwaka huu wa 2010 linatarajiwa kuanza rasmi Jumapili kesho tarehe 18 Julai 2010 huko Johanesburg nchini Afrika Kusini. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kampuni ya MultiChoice Tanzania , jumla ya washiriki 14 watatambulishwa siku hiyo wakati wakiingia katika Jumba la Big Brother. Shindano hilo litadumu kwa siku 91. Mshindi wa Big Brother 2010 anatarajiwa kuondoka na kitita cha US Dollars 200,000. Kama kawaida shindano hilo litakuwa likirushwa hewani kupitia kituo cha DStv-Channel 198. Tangu shindano hilo lianzishwe,kumekuwa na maoni tofauti tofauti kuhusu faida au hasara za shindano kama hilo.Wapo watu ambao wamekuwa wakidai kwamba shindano hilo linachangia katika kuporomoka kwa maadili kutokana na vitendo vya ki-ngono ngono vinavyofanywa na washiriki wa shindano hilo. Pamoja na hayo,shindano hilo limekuwa likijipatia mashabiki na wafuasi chungu mbovu kila mwaka. Mwaka jana Tanzania iliwakilishwa na mmoja wa wash

Ni Robo Tu Ya Wanaume Wa Dar Wenye Mbegu Zenye Rutuba

IMEFAHAMIKA, kuwa idadi ya wanaume wa Kitanzania wenye mbegu za uzazi zisizorutubisha hivyo kutoweza kurutubisha yai la mwanamke na kusababisha mimba inaongezeka. Kwa mujibu wa gazeti la ‘ The Citizen’ toleo la Jumamosi ( Leo), Julai 17,2010 zaidi ya asilimia 35 ya wanaume wanaofanya vipimo vya rutuba za mbegu za uzazi wamegundulika kuwa hawana. Mara nyingi lawama za kukosa mtoto katika familia zimekuwa zikielekezwa kwa mwanammke kutokana na .... Soma zaidi ; http:// www.kwanzajamii.com

NHC waanza kuwatimua Wapangaji batili

Image
Shirika la Nyumba ya Taifa (NHC) limeanza kuwaondoa kwa nguvu baadhi ya wapangaji ambao wamebainika kuishi kwenye nyumba hizo kwa kurithishana badala ya kufuata utaratibu maalumu uliopangwa na shirika. Picture Hatua hiyo imewakumba baadhi ya wapangaji katika maghorofa ya Keko Mtaa wa Magurumbasi A ambapo kazi hiyo ilisimamiwa na viongozi wa NHC na Kampuni ya udalali ya Msolopa. Mwandishi wa gazeti la DarLeo alishuhudia mpangaji Pantalelo Mushi akiondolewa vitu vyake ndani ya nyumba chini ya usimamizi wa wajumbe wa nyumba kumi. Ofisa wa NHC, Anneth Natai, amesema kumekuwa na mazoea ya wapangaji kuwarithisha watu wengine bila ya idhini ya uongozi. Kutokana na kitendo hicho, NHC imekuwa ikipatwa na usumbufu pindi kunapotokea tatizo na hata wengine kushindwa kufuata masharti yao. “Kuna wapangaji wengine wamekuwa wakilipa kodi kubwa kwa kuwapa wamiliki halali ambayo hata sisi hatuijui na pia tumekuwa hatuwafahamu wapangaji halisi,” amesema. Amesema kazi ya uondoaji wapangaji wasiotamb

viwango vipya vya soka.... Brazil yashuka

* Hispania yashika ukanda, Tanzania yazidi kuzama ZURICH, Uswisi BRAZIL imeporomoka kwa nafasi mbili kwenye ubora wa viwango vilivyotolewa jana na Shirikisho la Soka la Kimataifa, FIFA, huku Hispania ikishika ukanda ikifuatiwa na Uholanzi. Mabingwa hao wa dunia mara tano, walikuwa wakishika namba moja kwenye chati hizo za FIFA tangu April 2010 imeporomoka ikiwa ni baada ya matokeo mabaya ya Fainali za Kombe la Dunia zilizofanyika Afrika Kusini. Brazil iliondoshwa na Uholanzi katika mechi ya robo fainali kwa kufungwa mabao 2-1 ambayo ilikuwa ikishika nafasi ya nne kabla ya kupanda nafasi ya pili kwenye viwango hivi vipya vya Fifa. Uholanzi ilifungwa bao 1-0 na Hispania kwenye fainali. Kwa mujibu wa viwango hivyo vipya vya Fifa, Tanzania imeshuka kwa nafasi nne kutoka nafasi ya 108 ambayo ilikuwa ikiishikilia mwezi Aprili mpaka nafasi ya 112. Januari mwaka huu, Tanzania ilikuwa nafasi ya 108 sawa na Februari kabla ya kushuka kwa nafasi moja hadi 109 mwezi Machi. Ilipanda tena kwa nafasi

The place To be In Musoma Town

Image
MASERO INN hii ni Hotel Masero inn inayopatikana pale maeneo ya mtaa wa Mukendo karibu kabisa na club Metropole,asante Mdau Rogers kwa picha hii wadau wamekupata,usikose kupata Lunch yako pale na kila haina ya madikodiko

Mpendazoe agombea ubunge kwa Chadema

Image
Viongozi wa CCJ wakikabidhiwa kadi na Mwenyekiti wa Chadema CHAMA Cha Jamii (CCJ) kimeondokwa na vigogo wake na waanzilishi kadhaa wake akiwamo msemaji wake mkuu, Fred Mpendazoe aliyetangaza kugombea ubunge kwa tiketi ya Chadema. Mwenyekiti wa chama hicho Richard Kiyabo, naibu Katibu Mkuu Nickson Ng'ihily na Msemaji wa Chama, Fred Mpendazoe jana walikabidhiwa kadi za Chadema jijini Dar es Salaam na mwenyekiti Freeman Mbowe. Muda mfupi baada ya kupokea kadi hizo, viongozi hao walitangaza nia ya kugombea ubunge katika majimbo tofauti nchini kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu. Fred Mpendazoe ambaye mwanzoni mwa mwaka huu aliacha ubunge, kuihama CCM na kujiunga na CCJ, ametangaza kuwania ubunge wa Jimbo la Segerea, Richard Kiyabo anaenda Bukene na Ng'ihily anagombea Jimbo la Temeke. Jimbo la Segerea pia linawaniwa na Dk Makongoro Mahanga wa CCM. Kabla ya kujiunga na CCJ, Mpendazoe alikuwa mbunge wa Jimbo la Kishapu mkoani Shinyanga kupitia CCM. Akizungum

MUNGU WANGU.....HUJAFA HUJAUMBIKA

Image
OMG!!!!! Take Heart. Hujafa hujaumbika Hii ndiyo ajali iliyoangamiza zaidi ya watu 230 DRC baada ya gari la mafuta kupinduka.ili ni fundisho kwetu magari yanayobeba mafuta siyo ya kukimbilia Habari hii ni kutoka tovuti ya www.u-turn.co.tz

DAWA YA UKIMWI YAPATIKANA !!!

WANASAYANSI nchini Marekani wamegundua chembechembe za kinga ambazo zinauwezo mkubwa wa kupambana na kuua virusi vya ugonjwa wa Ukimwi ambao hadi sasa hauna chanjo wala tiba ya uhakika. Ugunduzi huo tayari umethibitishwa na wataalamu mbalimbali, ikiwemo Mamlaka ya Chakula na Dawa ya Marekani. Vyombo mbalimbali vya habari vya kimataifa vimeripoti kuhusu ugunduzi huo ambao unaelekea kutoa mapambazuko mapya kwa ugonjwa huo hatari ambao umekuwa ukiathiri nguvu kazi sehemu mbalimbali duniani, hususan nchi zinazoendelea. Wanasayansi hao wa Taasisi ya Magonjwa ya Kuambukiza na Mzio (Niaida) walieleza katika taarifa yao ya wiki iliyopita kuwa kwenye utafiti huo wamebaini aina mbili za chembechembe zinazoweza kumsaidia binadamu kupambana na virusi vya ukimwi. Mkurugenzi wa Niaida, Dk Anthony Fauci alizitaja chembechembe hizo za kinga kuwa ni VRCO1 na VRCO2 ambazo utafiti wake umeonyesha kuwa zinaweza kuua virusi vya ukimwi kwa asilimia 90. Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) dawa huthib

REDNAPP HADI MWAKA 2013

Image
Redknapp Meneja wa klabu ya Tottenham Harry Redknapp ameongeza mkataba wa kuendelea kukinoa kikosi cha klabu hiyo mpaka mwaka 2013. Mzee huyo mwenye umri wa miaka 63 ameongeza mkataba huo huku akiwa ameifanyia makubwa klabu hiyo ambayo msimu ujao itashiriki kwenye michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya baada ya kumaliza katika nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi kuu ya soka nchini Uingereza. Hatua hiyo ya kuamiliwa na mabosi wake na kupewa mkataba mpya imemkuna sana Harry Redknapp ambae anadai huenda imeshababishwa na utawala mzuri alionao katika kikosi chake ambapo mara kadhaa amekua akiwaeleza ukweli wachezaji wake. Kabla ya kusaini mkataba mpya, mkataba wa zamani wa miaka miwili wa Harry Redknapp ulikuwa unatarajia kufikia kikomo mwaka ujao.

Azam FC yatangaza 22: Wapya 8, Waachwa 10

Klabu ya soka nchini, Azam FC inayoshiriki ligi kuu soka ya VodaCom Tanzania Bara imetangaza usajili wa wachezaji ishirini na wawili, wanane kati yao wakiwa wapya huku kumi wa kikosi kilichopita wakiachwa. Picture Said Mohammed Abeid / Mwenyekiti - Azam FC Katika taarifa iliyomo katika tovuti ya klabu hiyo, wachezaji wapya waliosajiliwa na timu hiyo ni Mohamed Binslum (Huru), Jackson Chove (JKT Ruvu), Jabir Aziz na Ramadhan Chombo 'Redondo' (Simba), Mrisho Ngasssa (Yanga), Kalimangonga Sam Daniel Ongala Rampling 'Kali Ongala' (GIF-Sweeden), Patrick Mutesa Mafisango (APR- Rwanda) na Peter Senyonjo (Polisi-Uganda). Wachezaji waliobaki ni John Bocco, Erasto Nyoni, Jamal Mnyate, Salum Aboubakar 'Sure Boy', Vladmir Niyonkuru, Philip Alando, Luckson Kakolaki, Malika Ndeule, Aggrey Morice, Salum Swed, Ibrahim Shikanda, Ally Manzi, Seleman Kasim 'Selembe' na Ibrahim Mwaipopo. Wachezaji waliopanda toka timu ya vijana 'Azam Academy' ni sita ambao ni Sino A

Justin Bieber - Somebody To Love Remix ft. Usher

SPAIN MABINGWA WAPYA KOMBE LA DUNIA

Image
Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini pamoja na Rais wa Fifa,Sepp Blatta wakiwa na mabingwa wapya wa Dunia mara baada ya kuwakabidhi kikombe chao cha ubingwa walioupata kwa kuitungua timu ya Taifa ya Uholanzi bao 1-0 lililofungwa na mchezaji Andres Iniesta dakika nne tu kabla ya mechi kumalizika.

Ajali ya lori yaua watano mkoani Rukwa

Watu watano wamekufa papo hapo na wengine kujeruhiwa baada ya lori walilokuwa wakisafiria kushindwa kupanda mlima Lukangao na kupinduka. Ajali hiyo ilitokea juzi saa kumi na moja jioni katika kijiji cha Ntendo, Sumbawanga mkoani Rukwa. Gari hilo ni lori aina ya Scania lenye namba za usajili T 347 ATX ambalo ni mali ya mfanyabiashara Khalid Salum Abdallah, lililokuwa likiendeshwa na Abeid Said (32), mkazi wa Mazwi. Wakati likipata ajali, lori hilo lilikuwa limebeba zaidi ya magunia ya mpunga 80 pamoja na watu 10 waliokuwa wamekaa juu wakitokea kijiji cha Majimoto wilayani Mpanda. “Wakati likipanda mlima, lilipata pancha na hivyo kupoteza mwelekeo na kupinduka na watu kupoteza maisha,” alisema Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Rukwa, Isunto Mantage. Kamanda Mantage aliwataja waliokufa kwenye ajali hiyo kuwa ni mwanafunzi wa Sekondari ya Karema, Lucy Andrew (24), Fumbuka Elias (28), Mayunga Mathias (30), na wengine wawili ambao bado hawajatambuliwa. Majeruhi waliotajwa ni Athanas Choka (26), N

SHYROSE BHANJI KUGOMBEA UBUNGE KINONDONI • 2010

Image
Shy-Rose Sadruddin Bhanji Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Shy-Rose Sadruddin Bhanji ametangaza kujitosa katika nafasi ya ubunge jimbo la Kinondoni jijini Dar es Salaam kupitia CCM na lengo lake kubwa ni kuwa kiungo muhimu katika jamii ya wanakinondoni. Akitangaza azma yake ya kuomba ridhaa kwa wanachama wa CCM katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Shy-Rose alisema kwa mtazamo wake neno ubunge kwa mwaka 2010 linahitaji tafsiri mpya kabisa. `…kwa sasa mbunge anatakiwa kuwa ni kiungo cha jamii badala ya kuwa mwakilishi wa jimbo kama ilivyozoeleka` alifafanua Shy-Rose. `Mwaka 2010 ni mwaka wa mabadiliko na ndio maana nimeona kwamba ili kila mwananchi kuweza kuwajibika, nafasi ya mbunge inahitaji kutafsiriwa upya ili iendane na wakati na matatizo ambayo yanayotukakabili wananch` alisema. Kwa maana hiyo amesema kwamba hata sifa za mbunge zinahitaji kutafsiriwa upya kabisa, kwani majukumu yake yamebadilika kuendana na wakati. Ametaja baadhi ya sifa hizo mpya ni kuwa mhamasishaji, kiung

WACHEZAJI 70 WACHAGULIWA KUUNDA TIMU YA SERENGETI BOYS

Image
Zaidi ya wachezaji sabini wateuliwa kuunda timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17. Zaidi ya wachezaji sabini wameteuliwa kuunda timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 SERENGENTI BOYS kutoka katika mashindano ya COPA COCA COLA ambayo tayari yameingia katika hatua ya nusu fainali. Kocha masaindizi wa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 SLYVESTER MASHI amesema vijana wanaoshiriki mashindano ya mwaka huu ya COPA COCA COLA wameonyesha vipaji vya hali ya juu na ni hazina kwa taifa Mashindano ya COPA COCA COLA yameingia katika hatua ya NUSU FAINALI kwa mchezo mmoja kati ya KINONDONI na MJINI MAGHARIBI wakati kesho KIGOMA inateremka dimbani kuivaa TEMEKE

Anaswa akimlawiti mtoto wake Liveee!!

Watoto wa kazi wa Afande Mwema,mkoani Pwani limemtundika nyuma ya nondo mpuuzi mmoja aliyetambulika Ally Salehe (36), mkazi wa Kibaha, kwa tuhuma za kukutwa akimlawiti mtoto wake wa kiume ambaye ni denti wa darasa la nne. Kwa mujibu wa bosi wa Polisi mkoani Pwani, Absalomon Mwakyoma, mtuhumiwa huyo alikamatwa juzi usiku baada ya kukutwa na majirani akifanya kitendo hicho cha kinyama. Amesema majirani walikuwa na tetesi kuhusiana na mtuhumiwa kumfanyia kitendo hicho mtoto huyo ambaye ni wa mkewe lakini walishindwa kumchukulia hatua. Amesema siku za mwizi ni arobaini kwani mtuhumiwa alikuwa akifanya kitendo hicho kwa muda mrefu hivyo juzi usiku majirani walimnasa live mtuhumiwa akimfanyia ukatili mtoto huyo pembeni ya mti karibu na nyumba wanayoishi. Baada ya majirani kumkamata mtuhumiwa huyo walianza kumpa kipigo kikali na kisha kumpeleka kituoni. Imedaiwa wakati mtuhumiwa huyo anafanya kitendo hicho mkewe alikuwa ndani akiendelea na shughuli nyingine. Hata hivyo imedaiwa kuwa mke wa mt

na huu ndio mpango mzima wa fiesta 2010.

Tamasha la kumi la burudani na michezo na sanaa nchini Tanzania, linalojulikana zaidi kwa jina la Fiesta limewadia, msimu unaanza tarehe 7 mwezi Julai ambapo utakuwa ni msisimko wa burudani kwa mwezi mzima, huku wasanii wakitembelea baadhi ya mikoa ya Tanzania yenye msisimko wa sanaa kujumuika na mashabiki wa sanaa, na kuonesha kazi zao. Kwa mwaka huu wa 2010, Fiesta imepewa msemo wa Jipanguse, ikiwa na mlengo wa kuhamasisha vijana, kuachana na tabia ya kulalamika kuhusiana na matatizo wanayokutana nayo katika maisha yao ya kila siku, na badala yake wachukulie matatizo hayo kama ni sawa na kuanguka, wajipanguse na kuendelea na safari ya maisha.. Kauli mbiu hii inamsisitiza kijana wa kitanzania kuachana na habari za kuhubiri matatizo yake huku akiomba msaada wa kuyatatua wakati akitumainiwa kama mjenzi wa Taifa, kupitia burudani kijana anaelimishwa kuhubiri jinsi ya kuutumia ujana wake kukabiliana na ugumu wa Taifa akiwa kama nguzo ya Taifa. Mikoa nane ya Tanzania itajipangusa kiburudan

2 IN 1.........FLAVA NITE Feat: LADY JAYDEE & MACHOZI BAND, DJ BONI LUV & DJ MACKAY

Image
Siku ya mkesha wa 77, Itakuwa ni Jumanne tar 6 July. Hapana kukosa kati pale mimi pia nitakuwepo habari hii ni kutoka kwa lady jaydee blog.

KUWA MAKINI

Image
Inasemekana kuwa ATM ni eneo ambalo linabeba vimelea vya magonjwa keypads ndizo hasaaa zenye vimelea vingi kwa sababu ni watu wengi wanatumia ambao hujui wametoka wapi wameshika nini hivyo na wewe kuja tu na kuanza kutumia unaweza beba vimelea vya magonjwa kwenye mikono yako.Nawa mikono mara kwa mara hasa kama umetoka kutoa hela kwenye Atm Machines kabla hujaanza kupeleka mikono kinywani,puani,machoni n.k...

BET AWARDS 2010 KUFANYIKA LEO

Image
WalE wapenzi wa burudani wanaopendelea kufatilia maswala ya burudani kwa ujumla,ile siku iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu ndo imefika leo NI Utowaji wa tuzo utaKAfanyika leo kwa majira ya Africa mashariki itakuwa saa 3 usiku so kaa karibu na Tv yako uweze kuona mpango mzima kwa wale wenye ving'amuzi vya DSTV.

NIGERIA'S PRESIDENT SUSPENDS NATIONAL SOCCER TEAM

News on the CNN website reads, "Nigeria's president Goodluck Jonathan has suspended the national soccer team from international competition for two years after their dismal performance at the World Cup." "President Goodluck Jonathan has directed that Nigeria withdraws from international competition for two years to enable the country to put its house in order," spokesman Ima Niboro told reporters. Nigeria's Sports Minister Ibrahim Isa Bio confirmed the decision in an interview with CNN. He said: "The government has taken a decision we believe is in the interests of Nigeria that we should for now, withdraw from international competition because our football since 1996 seems not to be growing. "The government spends a lot of money to encourage football in Nigeria and we need to go back to the drawing board the way Ghana did two years ago. "The president Goodluck Jonathan has endorsed this decision and the Nigerian people are excited about it. &q