Posts

Showing posts from April, 2015

WARSHA: UMUHIMU WA WANAUME KATIKA FAMILIA

Image

BOT WAZUNGUMZIA KUHUSU KINACHOSEMWA KUHUSU SARAFU YA SH. 500

Image
Asilimia 94 ya madini katika sarafu ya sh. 500 ni chuma na asilimia 6 ni Nickel, ameeleza Mkurugenzi wa Huduma za Kibenki katika Benki Kuu ya Tanzania, Bw. Marcian Kobello.  Pia ndivyo ilivyoelezwa wakati wa uzinduzi wa sarafu hii mnamo mwezi Septemba mwaka jana kabla haijaingizwa katika mzunguko mwezi Oktoba 2014.  Bw. Kobello amesema hadi sasa sarafu zenye thamani ya sh. 1,162,000,000/- zimekwisha sambazwa kote nchini na kwamba kuna kiasi cha kutosha cha sarafu hiyo endapo itahitajika. “Hakuna kabisa madini ya fedha katika sarafu ya sh. 500,” amesema Bw. Kobello na kuongeza kuwa haitegemewi kwamba mfanyabiashara yeyote anaweza kununua sarafu hiyo kwa bei ya juu kuliko thamani yake halisi. “Kwa hiyo, tunapenda kuwafahamisha wananchi kwamba kuna kiasi cha kutosha cha sarafu za sh. 500 nchini na kwamba kununua sarafu hiyo kwa bei ya juu kuliko thamani yake ni kujiingizia hasara,” ameeleza mkurugenzi huyo. Pia ameongeza kuwa Nickel sio miongoni mwa madini maarufu kwa ajili ya kuten

SOMA MAGAZETI YA LEO ALHAMIS, APRIL 30

Image

Majina wasanii watakaowania tuzo za KTMA mwaka huu

Image
1. MTUMBUIZAJI BORA WA MUZIKI WA MWAKA- KIUME 1 MZEE YUSSUF 2 CHRISTIAN BELLA 3 DIAMOND PLANUMZ 4 ALLY KIBA 5 NYOSHI EL SAADAT 2.MTUMBUIZAJI BORA WA MUZIKI WA MWAKA- KIKE 1 VANESSA MDEE 2 KHADIJA KOPA 3 ISHA MASHAUZI 4 SHAA 5 DAYNA NYANGE 3.MWIMBAJI BORA WA KIUME- TAARAB 1 MZEE YUSSUF 2 PRINCE AMIGO 3 HASSAN VOCHA 4 HASSAN ALLY 5 MUSSA KIJOTI 4. MWIMBAJI BORA WA KIUME- BONGO FLEVA 1 ALI KIBA 2 BEN POL 3 JUX 4 DIAMOND 5 BELLE 9 5.MWIMBAJI BORA WA KIUME- BENDI 1 JOSE MARA 2 KALALA JUNIOR 3 KHALIDI CHOKORAA 4 CHAZ BABA 5 NYOSHI EL SADAT 6.MWIMBAJI BORA WA KIKE- TAARAB 1 KHADIJA KOPA 2 ISHA MASHAUZI 3 HADIJA YUSSUF 4 LEIYLA RASHID 5 FATUMA NYORO 7.MWIMBAJI BORA WA KIKE – BONGO FLEVA 1.LADY JAY DEE 2.VANESSA MDEE 3.LINAH 4.GRACE MATATA 5.MALAIKA 9.WIMBO BORA WA TAARAB 1 HASID HANA SABABU-HADIJA YUSSUF 2 LADY WITH A CONFIDENCE-KHADIJA KOPA 3 CHOZI LA MAMA-MZEE YUSUPH 4 FANYA YAKO-LEYLA RASHID 5 MAPENZI HAYANA DHAMANA-ISHA MASHAUZI 10.WIMBO BORA WA MWAKA 1 MWANA -ALI KIBA 2

KONGO BRAZZAVILE YAPIGA MARUFUKU UVAAJI WA HIJABU

Image
Serikali nchini Kongo - Brazzaville imepiga marufuku uvaaji wa hijabu nchini humo. Kwa mujibu wa taarifa iliotolewana redio ya taifa Kongo, serikali imepiga marufuku kwa waislamu kuvaa hijabu na kufunika uso, wakati wageni wakipigwa marufuku kutumia misikiti nyakati za usiku nchini kote kama sehemu ya jitihada za kupambana na ugaidi katika taifa hilo la Afrika ya Kati.  Kwa mujibu wa Waziri wa Mambo ya Ndani, Zephirin Raymond Mboulou, uamuzi huo ulichukuliwa baada ya uchunguzi na kukamata baadhi ya watu katika vipengele vya makosa ya jinai na kudai wanaohusika na matendo hayo huvaa hijabu za kufunika uso na kuacha macho tu.  Serekali imesema kuwa wanaruhusu kujifunika kichwa tu bila kuziba uso na wageni waotumia msikiti nyakati za usiku kama malazi wamepigwa marufuku kwani misikiti si kwa ajili ya kulala bali kwa kufanya ibada.  Afisa wa Polisi, Mbata Ya Bakolo, ametaarifu Waislamu juu ya mwendelezo wa operesheni ya Polisi ambao una lengo la kupambana na uhalifu na uhamiaji har

JIHADHARI, CHUPA YA MAJI NI HATARI

Image
Ni kawaida sana siku hizi kupuuzia jumbe nyingi zinazotumwa kwenye makundi mbalimbali ya mawasiliano kwa sababu nyingi ya hizo huwa ni ngano tu. Ila mtu anapokuwa na muda anaweza kuulizia ukweli kutoka kwa wengine. Ndicho nilichokifanya leo. Nilipuuzia ujumbe uliotumwa kwenye kundi moja (tizama picha hapo juu), nikidhani ni moja ya zile zinazotungwa ili kuwapa watu kiwewe tu, lakini baadaye nikapata wazo la kuutuma kwenye kundi jingine na kuuliza 'Inawezekanaje?"  Majibu niliyopata yamenipa sababu ya kumshukuru aliyetuma ujumbe huo kwa kunisababisha niwe makini kuhusiana na hilo. Nimefahamishwa: "Ni possible kabisa sis. Imeshatokea na ilimhusisha mtu namfahamu sema tu aligonga gari nyingine kwa nyuma. Chupa ya maji aliiweka kwenye ile nafasi kwenye gia pale kumbe aliposhika breki ikaanguka na hakujua so safari ikaendelea baadaye kidogo akashika breki kumbe imesogea kwenye pedal" Mwingine pia akachangia: "Subi hiyo ya chupa ya maji ilishanitokea

CHUKUA HANDBAG YAKO KWA BEI NAFUU KABISA

Image
JIPATIE HANDBAG ZA KISASA KABISA, KAMA UPO NDANI YA JIJI LA DAR UTALETEWA MPAKA ULIPO PIGA NAMBA 0715 019393 UTAPATA MAELEKEZO YOTE, MIKOBA NI ELF 50 TU. MIKOBA YOTE INA VITOTO NDANI. Mkoba huu ni mmoja, unaweza kuugeuza na ukaonekana mwingine

Nkurunziza: Sitarudi nyuma katika kugombe urais

Image
Rais Pierre Nkurunziza wa Burundi amesema kuwa, hatasalimu amri kwa wale wanaofanya njama kutaka asigombee urais katika uchaguzi mkuu ujao nchini humo. Hayo yamesemwa na Willy Nyamitwe, mshauri wa Rais Nkurunziza akimnukuu rais huyo ambapo pia amekosoa maandamano ya wapinzani wanaopinga azma yake ya kushiriki katika uchaguzi ujao na kuitaja hatua hiyo kuwa ni kinyume na demokrasia.  Nyamitwe amesisitiza kuwa, Rais Nkurunziza hatasalimu amri katika azma yake hiyo. Amewataja wale wanaoandamana kupinga hatua hiyo kuwa, wanatishia usalama wa wananchi katika uchaguzi ujao. Mshauri huyo wa raia wa Burundi anasema chama tawala CNDD-FDD, kama vilivyo vyama vingine vya siasa na katika fremu ya mwenendo wa kidemokrasia, kina haki ya kumteua mgombea yeyote kimtakaye. Kwa muda wa siku tatu sasa, maeneo kadhaa ya Burundi yamekuwa yamekumbwa na machafuko makali ambayo yamesababishwa na hatua ya chama tawala CNDD-FDD kumuidhinisha Rais Nkurunziza kupeperusha bendera ya chama hicho k

MAGAZETI YA LEO JUMATANO, APRIL 29

Image
 Kurasa za mbele na nyumba katika magazeti ya leo TZ

Hotuba ya Rais Mwinyi alipozungumza na Wazanzibari Marekani

Image
Info Post Tumeshirikishwa taarifa hii na Abou Shatry/Chief  @SwahiliVilla blog

MANNY PACQUIAO AWASILI LAS VEGAS TAYARI KUPAMBANA NA FLOYD MAYWEATHER

Image
 Ndege aliyosafiri nayo Pacquiao ikiwa uwanjani Philippines    Pambano kati ya Mfilipino Manny Pacquiao na Mmarekani Floyd Mayweather linatarajia kufanyika tarehe May 2, 2015. LasVegas, Nevada. Pambano hilo linatarajia kuingiza zaidi ya kiasi cha $ 300million.    Msafara wa Manny Pacquiao ukitoka Los Angeles kwenda Las Vegas  Basi la kifahari lililombeba Pacquiao lilisindikizwa na bikers kwenda Las Vegas Instagram Selfie ya Pacquiao akiwa na mashabiki wake ndani safarini kuelekea Las Vegas Manny Pacuiao amekua akijifua na kocha wake Freddie Roach, kwenye Freddie Roach Wild Card Gym huko Los Angeles, CA na baadae kusafiri umbali wa maili 270 ndani ya basi lake kuelekea Las Vegas, NV.  Twitter Selfie ya Manny Pacquiao na Mkewe ndani ya basi kuelekea Las Vegas   Manny Pacquia na mwanae wa mwisho, Israel, waliwasili katika hoteli ya  Mandalay Bay tayari kujifua mara ya mwisho kabla ya mpambano huo. Kwa picha zaidi bofya SOMA ZAIDI Picha kwa hisani y