Posts

Showing posts from November, 2015

KAULI YA MEMBE BAADA YA RAIS MAGUFULI KUFUTA SAFARI ZA WATENDAJI WA SERIKALI

Image
Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe amempongeza Rais wa Awamu ya Tano, Dk John Magufuli kwa kupiga marufuku safari za nje ya nchi, akisema mawaziri na watendaji wa Serikali walikuwa wakigongana angani na ndege utadhani Tanzania ilikuwa ikiwaka moto. Mbunge huyo wa zamani wa Mtama alisema uamuzi huo utaokoa fedha nyingi za Serikali na kumtaka Rais kushusha rungu hilo hadi kwenye mashirika. Wakati Membe akieleza hayo, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue alisema kila safari ya nje ina gharama yake na kila safari itakayofutwa zitapatikana fedha kusaidia masuala mengine ya maendeleo katika jamii. Juzi, Dk Magufuli alipiga marufuku safari za nje ya nchi kwa watendaji na kwamba shughuli ambazo wangekwenda kuzifanya, kuanzia sasa zitahitaji kibali kutoka kwake au zitafanywa na mabalozi wa Tanzania walioko katika nchi husika. Jana Membe alisema: "...Tulikuwa tunagongana huko hewani utadhani huku nyumban

Kauli ya EU, Marekani kuhusu Sheria ya Uhalifu wa Kimtandao na ukiukwaji haki za binadamu Tanzania

Image

WANAOWANIA USPIKA WAANZA KUCHUKUA FOMU

Image
  Aliyekuwa Waziri wa Uchukuzi Mhe. Samuel Sitta akisaini kitabu cha wageni kabla ya kuchukua fomu za kuwania uspika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mbele ya  Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa anayeshughulikia Oganaizesheni,  Ndugu Mohamed Seif Khatib  Aliyekuwa Waziri wa Uchukuzi Mhe. Samuel Sitta akizungumza na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa anayeshughulikia Oganaizesheni,  Ndugu Mohamed Seif Khatib mara baada ya kuchukua fomu ya kuwania nafasi ya uspika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania .  Aliyekuwa mbunge wa jimbo la Karagwe Gosbert Blandes akikabidhiwa fomu za kuwania nafasi ya Uspika wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka kwa Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa anayeshughulikia Oganaizesheni,  Ndugu Mohamed Seif Khatib   George Nangale akipitia fomu ya kuwania nafasi ya uspika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mara baada ya kukabidhiwa na  Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa anayeshughulikia Oga

Askari polisi afutwa kazi baada ya video kuonesha akipokea fedha

Image
JESHI la Polisi mkoani Tanga limemfukuza kazi askari wa kikosi cha usalama barabarani aliyetambulika kwa namba F. 785 CPL Anthony Temu (46) wa kituo cha Polisi Kabuku kwa kosa la kufedhehesha jeshi hilo. Akitoa taarifa kwa vyombo ya habari ofisini kwake Kamanda wa Polisi mkoa wa Tanga, Zuberi Mwombeji amesema askari huyo amefukuzwa baada ya kuthibitishwa kwa taarifa iliyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii ikimuonyesha akiomba na kupokea rushwa wakati akitekeleza majukumu yake.  

MAMBA KULINDA WAFUNGWA HATARI INDONESIA

Image
Indonesia huwa na sheria kali sana za kukabiliana na walanguzi wa mihadarati Mkuu wa shirika la kupambana na dawa za kulevya Indonesia amependekeza mamba watumiwe kulinda wafungwa waliohukumiwa kunyongwa. Budi Waseso anataka taifa hilo lijenge gereza kwenye kisiwa na kizingirwe na mamba akisema wanyama hao ni walinzi bora kushinda wanadamu, kwani hawawezi kuhongwa. Amesema atazuru maeneo mbalimbali katika taifa hilo kutafuta mamba wakali zaidi. Indonesia ina moja ya sheria kali zaidi za kupambana na dawa za kulevya duniani na ilianza tena kunyonga watu baada ya kusitisha hukumu hiyo kwa miaka mine 2013. "Tutaweka mamba wengi sana huko,” Bw Waseso alinukuliwa na tovuti moja nchini humo kwa jina Tempo. "Huwezi kuwahonga mamba. Huwezi kuwashawishi waruhusu washukiwa watoroke.” Mpango huu bado umo katika hatua za mwanzo mwanzo nab ado haijaamuliwa gereza hilo litakuwa wapi na ni lini litafunguliwa, shirika la habari la AFP limesema.

MAGAZETI YA LEO TANZANIA, NOVEMBER 11

Image

SOMA MAGAZETI YA LEO NOVEMBER 10

Image

Mbunge asitisha msaada wa "mabasi ya wanafunzi" kwa kushindwa uchaguzi

Aliyekuwa mbunge wa Jimbo la Mikindani, mkoani hapa, Hasnein Murji, amesitisha huduma ya usafiri kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Naliendele kufuatia kushindwa ubunge katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 25. Murji aligombea jimbo hilo kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM). Alikuwa akitoa usafiri kwa wanafunzi wa shule hiyo tangu mwaka 2011 alipochaguliwa kuwa mbunge wa jimbo hilo. Wakizungumza na Nipashe kwa nyakati tofauti shuleni hapo, wanafunzi hao walisema kuwa kitendo cha kutochaguliwa mbunge huyo kimewaathiri kiusafiri. ‘Tangu alipochaguliwa kuwa mbunge wa jimbo hili, alitoa magari mawili ambayo yalikuwa yanapokezana, tulikuwa hatulipi nauli, tulikuwa tunawahi vipindi kwa sababu tulikuwa na uhakika wa usafiri,’ alisema mmoja wa wanafunzi hao. Walisema usafiri wa daladala ni mchache, lakini pia wanatozwa nauli ya Sh. 500 badala ya Sh. 200. Walidai kuwa wakati mwingine wazazi wanashindwa kumudu gharama na kushindwa kufika shuleni kwa sababu ya kukosa nauli. W

Ratiba ya shughuli za Mkutano wa Kwanza wa Bunge 2015

Image

Matokeo ya mtihani wa Kitaifa wa Darasa la Saba 2015

ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA KILIMANJARO LINDI MARA MBEYA MOROGORO MTWARA MWANZA PWANI RUKWA RUVUMA SHINYANGA SINGIDA TABORA TANGA MANYARA GEITA KATAVI NJOMBE SIMIYU Baraza la Mitihani Tanzania - NECTA kimetangaza matokeo ya mitihani ya darasa la saba iliyofanyika September 9 na 10 mwaka huu ambapo mikoa ya kanda ya ziwa imefanya vizuri ikilinganishwa na mikoa mingine nchini. Akitangaza matokeo hayo jijini DSM, Katibu Mtendaji wa Baraza hilo Dk. Charles Msonde amesema jumla ya watahiniwa 51,8034 kati ya 76,3602 wamefaulu sawa na asilimia 67.84, ambapo kati yao wasichana wamefaulu kwa asilimia 64.60 na wavulana asilimia 71.58 huku kiwango hicho cha kikiongezeka kwa asilimia 10.85 ukilinganisha na ufaulu wa mwaka jana wa asilimia 56.99. Dk. Monde amezitaja shule zilifanikiwa kuingia kumi bora kitaifa mwaka huu ni pamoja na shule ya Waja Springs ya Geita iliyoshika nafasi ya kwanza ikifuatiwa na Enyamai ya Mara na Twibhoki pia ya Mara