Posts

Showing posts from July, 2016

Taarifa kutoka HESLB: Ofisi zitakuwa wazi Jumamosi na Jumapili hii

Taarifa kutoka HESLB: Ofisi zitakuwa wazi Jumamosi na Jumapili hii BODI YA MIKOPO YA WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU TAARIFA KWA UMMA OFISI ZA BODI YA MIKOPO KUWA WAZI KESHO JUMAMOSI NA JUMAPILI Bodi ya Mikopo inapenda kuwataarifu wadaiwa wote waliopo Dar es Salaam kuwa Ofisi za Bodi zitakuwa wazi kwa siku mbili za kesho, Jumamosi, Julai 30, 2016 na Jumapili, Julai 31, 2016 kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa 9:00 mchana ili kutoa huduma mbalimbali ikiwemo kuwasiliza wadaiwa. Hii ni fursa muhimu kwa wadaiwa wote wa mikopo ya elimu ya juu ambao hawajaanza kulipa mikopo kupata taarifa kuhusu madeni yao. Bodi ya Mikopo inatarajia kuanza kuwachukulia hatua za kisheria wadaiwa wote ambao hawataanza kulipa madeni yao mara moja. Hatua hizo ni pamoja na: i. Kufikishwa mahakamani; ii. Kutozwa faini; iii. Kunyimwa fursa za kupata mikopo; iv. Kunyimwa fursa za masomo nje ya nchi; na v. Kuzuiwa kusafiri nje ya nchi. Nyote mnakaribishwa ili kutumia fursa hii muhimu. Imetolewa na: Bw. Jerry Sa

Safari ya kuelekea Dodoma: Jambo 1 muhimu na 8 ya kuzingatia

Image
Kuna mambo ambayo ni lazima yaangaliwe katika uamuzi wa kuhamia Dodoma. Kuna masuala ya kuangalia kama idadi ya watumishi watakaohama na hawa wana familia ngapi, ikiwamo watoto wa shule. Lazima athari za kuhamisha watu wa namna hii hazina budi zitathminiwe na kupatiwa mwelekeo endelevu. Lazima kuangalia gharama za kuhama ghafla ni Sh ngapi na watakaolengwa ni watumishi wapi, yaani kada ipi na fedha zimetengwa kwenye kasma ipi! Aidha, hatua ziangaliwe za kuzuia bei ya viwanja kupanda bei ovyo kwa sababu idadi ya watu watakaotafuta viwanja itaongezeka kwani tayari kuna taarifa kuwa mamia ya wananchi wameanza kupeleka maombi yao ya kupata viwanja katika ofisi za Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu Dodoma (CDA). Hali hiyo imetokea baada ya Rais Dk. John Magufuli kutangaza nia ya Serikali kuhamia mjini Dodoma kwa kuwa ndiko yaliko makao makuu ya nchi. Kwamba kuna idadi kubwa ya watu wanaofika katika ofisi za Idara ya Ardhi katika mamlaka hiyo, na kwamba Jeshi la Polisi tayari linal

KATIBU MKUU TFF ATOA SABABU ZA AIRTEL KUIBUA VIPAJI

Image
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Mwesigwa Selestine amesema kutimia kwa malengo ya Kampuni ya Simu za mkononi ya Airtel imesukuma kampuni hiyo kuendelea kudhamini mashindano ya soka kwa vijana – wavulana na wasichana. Selestine alisema hayo kwenye hafla ya kukabidhiana vifaa kwa Airtel kwenda TFF kabla ya kwenda kwa klabu shiriki iliyofanyika Ukumbi wa TFF, Dar es Salaam. Vifaa vilivyotolewa kwa timu jezi kamili ikiwa ni pamoja na jezi za waamuzi, viatu, mipira na vizuia ugoko kutopata madhara. Alisema sababu hizo ni uhusiano mzuri kati ya TFF na Airtel inayotoa bora za mawasiliano kwa miaka sita sasa sambamba na kuendeleza vipaji kwani nusu ya wachezaji wa timu ya taifa ya vijana wenye umri wa chini ya miaka 17, wanatoka katika michuano hiyo ya mwaka jana. Wachezaji hao ni  Ramadhani Awm Kabwili, Nickson Clement Kibabage, Dickson Nickson Job, Ally Hamisi Ng’anzi, Syprian Benedictor Mtesigwa, Mohammed Abdallah Rashid na Muhsin Malima Makame na Kati

MAKAMU WA RAIS MH. MAMA SAMIA SULUHU HASSAN ABAINI CHANGAMOTO HOSPITALI YA SARATANI YA OCEAN ROAD

Image
Makamu wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan akimjulia hali mmoja wa wagonjwa waliolazwa katika taasisi ya saratani ya Ocean Road Jijini Dar es Salaam wakati wa ziara yake aliyoifanya katika hospitali hiyo jana Ijumaa (Julai 29, 2016). (PICHA NA ISMAIL NGAYONGA- MAELEZO) Na Beatrice Lyimo- MAELEZO MAKAMU wa Rais, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya ziara yake ya kwanza katika Hospitali ya Taasisi ya Saratani ya Ocean Road Jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuona wagonjwa sambamba na kuangalia  maendeleo ya hospital hiyo. Akiwa katika ziara hiyo Mhe. Samia amebaini baadhi ya changamoto zinazoikabili hospitali hiyo ikiwemo ya upungufu wa wauguzi na madaktari, uhaba wa mashine za mionzi, upungufu wa vifaa tiba pamoja na upatikanaji wa dawa za Saratani kwa wagonjwa hao. Amesema kuwa Serikali itahakikisha inaongeza mashine mbili mpya za mionzi kwa ajili ya kupimia wagonjwa wanaosumbuliwa na matatizo ya Saratani na kuahidi kupunguza deni la MSD wanaloidai hospital hiyo ili wagonjwa waw

Orodha ya wanachuo wanaorudi kusoma stashahada maalum ya ualimu UDOM

Image
Majina ya wanachuo waliokuwa wanasoma stashahada maalum ya ualimu chuo kikuu cha Dodoma waliopangiwa kurudi kwenye chuo hicho.

video: Makomando – Wanachezaje?

Image

Ndugu wa mtanzania aliyekamatwa kwa unga Pakistan wazungumza

Image
Baada ya wiki hii katika mitandao ya kijamii kusambaa video inayomuonyesha kijana mtanzania anayedaiwa kuwekwa rehani nchini Pakistan kutokana biashara ya unga, ndugu wa kijana huyo anayetambulika kwa jina la ‘Adamu Akida’ wamezungumza. Akiongea na gazeti la Mtanzania kaka wa Adamu aliyejitambulisha kwa jina la Hemed Abdallah (si jina lake halisi) alisema miezi minane iliyopita, Adamu alikwenda kwa kaka yake ambaye ni mtoto wa mama yake mdogo aliyetambulika kwa jina la Juma, na kuomba msaada wa mtaji kwani kazi yake ya kinyozi haikuwa ikilipa na hali ya maisha ilikuwa ngumu. Alisema baada ya kueleza shida yake hiyo, kaka yake huyo (Juma) alimuhoji kama yupo tayari kwa ajili ya kutafuta maisha nje ya nchi, na Adamu alikubali kufanya kazi ya aina yoyote ili mradi aweze kupata pesa. “Adamu kwa sasa ameshikiliwa kwa muda wa miezi minane, hatujui kama alikuwa ameingia katika janga hili hadi pale tulipoona video zake katika mitandao ya kijamii. Hapa aliyepo ni baba yake mdo

WIKI YA REKODI KWA LABEL YA WCB, HARMONIZE NAYE NA REKODI YAKE HII MPYA

Image
Inaweza kuwa ni wiki nzuri kwa Label ya  WCB  kwani hapo Jana  Diamond Platnumz  aliweza kusherehekea rekodi yake ya Video  "KIDOGO"  kufukisha Watazamaji  Milioni 1  ndani ya Siku 4. Hii pia inaweza ikawa rekodi mpya kwenye muziki wa  Harmonize , hii ni video mpya ya wimbo alioupa jina  ‘Matatizo‘  ambayo ilitoka Jul 4, 2016 na kwa sasa imeshafikisha watazamaji milioni moja ndani ya siku 12. Kwenye hii video tumeona maisha halisi ya msanii  Harmonize  kabla ya kuwa maarufu kwenye bongo fleva.

MARUFUKU RUSHWA KATIKA KUTATUA MIGOGORO YA ARDHI

Image
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Angeline Mabula akipekua mafaili ya hukumu za migogoro ya ardhi ili kujiridhisha kama haki inatendeka kwa wananchi wakati alipotembelea Baraza la Ardhi na Nyumba la Tanga mjini. Naibu Waziri wa Ardhi Mhe. Dkt Angeline Mabula akiongea na watendaji wa Baraza la Ardhi na Nyumba la Tanga mjini. Baadhi ya watendaji na watumishi wa umma wakimsikiliza Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Angeline Mabula katika ofisi za Baraza la Ardhi na Nyumba la Tanga mjini. ………………………………………………………………………………………………… Na Hassan I. Mabuye Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Angeline Mabula ayataka Mabaraza ya Ardhi na Nyumba kuepuka rushwa kutoka kwa wenye fedha ili kuwapa upendeleo na kukandamiza wanyonge katika maamuzi yahusuyo migogoro ya ardhi. Mheshimiwa Mabula ameyasema hayo wakati alipofanya ziara ya kutembelea Baraza la Ardhi na Nyumba la Tanga mjini. Wakati wa ziara hiyo Mhe. Naibu Waz

Taarifa ya NSSF ya kusimamishwa kazi Wakurugenzi na Mameneja

Image

Gugu Zulu, mwendesha magari ya langalanga Afrika Kusini afariki akikamlisha Trek4Mandela mlima Kilimanjaro

Image
Raia wa Afrika Kusini waliopanda Mlima hivi karibuni kwa lengo la kuchangisha fedha kwa ajili ya kununua taulo za kusaidia watoto wa kike. Aliyechuchumaa mbele (mwenye kofia), Gugu Zulu ndiye anatajwa kufariki Dunia wakati akielekea Kileleni. Na Dixon Busagaga  Ra ia wa Afrika ya Kusini Guguleth Mathebula Zulu (38) aliyefika nchini kwa ajili utalii wa kupanda Mlima Kilimanjaro amefariki leo tarehe 18.7.2016 baada ya kupatwa na tatizo la kushindwa kupumua kwenye mwinuko wa juu mlimani.   Shirika la Hifadhi za Taifa nchini kwa kushirikiana na mamlaka mbalimbali za serikali zinaendelea na uratibu wa kurejesha mwili wa marehemu nchini Afrika ya Kusini kwa ajili ya taratibu za maziko.   Zulu alifika nchini na kuanza kupanda Mlima Kilimanjaro tarehe 14.7.2016 kwa ajili ya kuenzi jitihada za Rais wa Kwanza wa Afrika ya Kusini Nelson Mandela za kusaidia familia maskini nchini Afrika ya Kusini, hususani kuwapatia mahitaji muhimu watoto wa kike ambao hawana uwezo wa kupata mahitaji mu

MAGAZETI YA LEO JUMANNE

Image