Posts

CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM CHAFUKUZA WANAFUNZI 43.

Image
Askari wakikabiliana na mwanafunzi huyu wa kike kwenye yaliyotoke mwezi 11, 2011, Maandamano yaliyopelekea wanafunzi 43 wa UDSM kufukuzwa Chuo. CHUO Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), kimewafukuza wanafunzi 43 na kuendelea kufuatilia nyendo za wengine tisa, baada ya kubainika kuwa walihusika katika matukio mbalimbali ya vurugu na uhalifu chuoni hapo. Kati ya wanafunzi hao, wanane walikuwa wamesimashiwa masomo kwa muda wa miezi tisa na 35 walisimamishwa ili kusubiri kumalizika kwa kesi zao zilizopo mahakamani. Uamuzi huo umekuja ikiwa zimepita siku mbili tangu baadhi ya wanafunzi chuoni hapo, kuvamia jengo la Ofisi za utawala la chuo hicho na kuwazuia maofisa na wafanyakazi wa chuo kutoka au kuingia ndani, hadi watakapoletewa taarifa za pesa zao kutoka Bodi ya Mikopo(TCU). Wanafunzi hao waliokuwa wanaendeleza mgomo wao ulioanza Jumatatu wiki hii wakidai taarifa za kwa nini pesa zao zinachelewa wakati bodi ya mikopo, ilishasema wamezileta chuoni hap

HAPPY BIRTHDAY DAVID LYIMO

Image
Wish all da best in ur life bro........... A birthday is just the first day of another 365-day journey around the sun. Enjoy the trip.

Msimamo wa John Mnyika kuhusu suala la posho

Kufuatia habari tarehe 28 Novemba kuhusu ‘kupanda kimya kimya kwa posho za wabunge kwa zaidi ya asilimia 150’ tarehe 29 Novemba 2011 nilitoa kauli yangu kama mbunge na katibu wa wabunge wa CHADEMA kuhusu suala husika. Katika kauli hiyo nilieleza kuwa: “ Wabunge wa CHADEMA hatujapokea taarifa rasmi kwamba masharti ya kazi ya ubunge yamebadilika na kwamba viwango vya posho vimeongezwa. Wala kamati ya wabunge wa CHADEMA haijawahi kuridhia ongezeko lolote la posho ya vikao (sitting allowance) kwa wabunge. Napenda kutumia fursa kusisitiza msimamo wetu wa kutaka posho za vikao (sitting allowance) ziweze kufutwa kwa wabunge na katika mfumo mzima wa malipo ya wakati wa kazi miongoni mwa watumishi wa umma”. Hivyo, kama mbunge na katibu wa wabunge wa CHADEMA nilitoa mwito kwa Rais Jakaya Kikwete kwa niaba ya Serikali na Spika Anna Makinda kwa niaba ya Bunge kutoa kauli kuhusu suala hili ili kuondoa hisia zinazojengeka kwamba ‘wabunge wote tumekaa bungeni na kukubaliana kujiongezea

Haki za watu wa jinsia moja zashinikizwa

Marekani imetangaza hadharani kuwa itapambana na ubaguzi dhidi ya wapenzi wa jinsia moja nchi za nje kwa kutumia msaada kutoka nchi za kigeni na diplomasia kushinikiza mabadiliko. Waziri wa mambo ya nje Hillary Clinton aliwaambia wanadiplomasia Geneva: "Haki za wapenzi wa jinsia moja ni haki za binadamu" Taarifa kutoka utawala wa Obama inayaelekeza mashirika ya serikali ya nchi hiyo kuangazia haki za wapenzi hao wanapofanya uamuzi wa kutoa misaada na uhifadhi wa kisiasa. Sera kama hizo tayari zinatumika kwa usawa wa kijinsia na ghasia za kikabila. "Isiwe jambo la uhalifu kwa mtu kufanya mapenzi ya jinsia moja," Bi Clinton alisema katika umoja wa mataifa Geneva, akiongeza kuwa utamaduni au dini siyo sababu ya kufanya ubaguzi. Wanadiplomasia hao pia ilihusisha wawakilishi kutoka nchi ambazo mapenzi ya jinsia moja ni uhalifu. Mabaloz

ROBO FAINALI YA MICHUANO YA ProLIFE SAUT: WANAMAHUSIANO YA JAMII WANG’ARA DHIDI YA WAHASIBU; HUKU MECHI YA KWANZA IKISHUHUDIA WANASHERIA WAKISUSIA MCH

Image
Robo fainali ya michuano ya mashindano ya ProLife katika Chuo cha Mtakatifu Agustino, Mwanza imeanza leo pale iliposhuhudiwa michezo miwili ya miamba ya soka chuoni hapo ambapo mechi ya kwanza ilikuwa ni kati ya timu ya Sheria (LLB) dhidi ya Walimu (EDUCATION) ulioanza saa 8 kamili mchana huku mchezo wa pili ulikuwa ni kati ya Mahusiano ya Jamii na Masoko (BAPRM) dhidhi ya Wahasibu (ADA). Katika mchezo wa kwanza mashabiki waliokuwepo uwanjani walishuhudia mchezo huo ukiishia kati baada ya timu ya Sheria kugomea mchezo huo kutokana na kilichodaiwa kuwa muamuzi wa mchezo huo kufanya maamuzi yalionyeesha dhahiri kuwapendelea timu ya Walimu hivyo mchezo huo kuishia katikati mwa kipindi cha pili na sheria kujitoa katika mashindano hayo hivyo walimu kupita kwenye raundi inayofuata kwa mbeleko hiyo. Aidha katika mchezo wa pili miamba ya soka ya SAUT timu ya Mahusiano ya Umma ilitoa kipigo cha mbwa mwizi pale ilipowagalagaza Wahasibu kwa jumla ya magoli mawili b

CHAMA CHA WANAFUNZI WANAOSOMA UHUSIANO WA UMMA NA MASOKO (SSPRA) WAFANYA SEMINA JUU YA MATUMIZI YA MTANDAO .

Image
Mkuu wangu wa kamati ya Uhusiano wa vyombo vya habari na Publication Bw. Francy Moses akiwasilisha mada yake ya juu ya kutumia mtandao na kufanya design ya publication mbalimbali. ME mwenyewe Nyanja kelvin Poti ambaye ni katibu mkuu wa kamati ya media relations and Publication ya SSPRA nikitoa mada juu ya maswala mazima ya mitandao wa internet na matumizi yake katika tasnia ya watu wa Mahusiano ya umma na Masoko. Baadhi ya wanachama wa SSPRA wakisikiliza semina hiyo kwa makini. Mdau Francy Moses (mwenye shati nyekundu) akirekebisha mambo mbele yake ni wanachama wa SSPRA katika semina hiyo.

WALIMU WATANGAZA KUGOMA NCHI NZIMA

Image
Rais wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), Gratian Mukoba akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam jana kuhusu mgomo wa walimu nchi nzima utakaoanza mwezi Januari kama Serikali haitatimiza makubaliano yaliyofikiwa ya kuwalipa madai yao. CHAMA Cha Walimu Tanzania (CWT), kimetangaza mgomo wa walimu nchi nzima kuanzia Januari mwakani ikiwa ni hatua ya kuishinikiza Serikali iwalipe walimu deni la malimbikizo ya stahili zao mbalimbali, linalofikia Sh49.6 bilioni. Hatua hiyo imekuja baada ya Serikali kushindwa kutimiza ahadi yake ya kuanza kuwalipa walimu fedha hizo tangu Novemba mwaka huu. Rais wa CWT, Gratian Mukoba alisema jana jijini Dar es Salaam alipozungumza na wandishi wa habari kuwa Serikali iliahidi kuwalipa walimu Novemba hadi Desemba mwaka huu ili kumaliza deni hilo. “Natangaza kuwa shule zitakapofunguliwa mwezi Januari 2012, sisi walimu tutaendelea kuwa likizo mpaka kero zetu zitakapotatuliwa,” alisema Mukoba. Alisema tangu Juni mwaka huu,

MAADHIMISHO YA SIKU YA UKIMWI DUNIANI MKOANI MWANZA

Image
Maandamano ya wadau wanaojishughulisha na mapambano ya kudhibiti UKIMWI katika jiji la Mwanza yakiingia katika uwanja wa Nyamagana Siku hii inatukumbusha kama sehemu ya jamii kupanga mikakati endelevu ya kuzuia Maambukizi mapya, kuzuia Unyanyapaa na kukabiliana na vifo vitokanavyo na UKIMWI. "Kiwango cha maambukizi katika jiji la Mwanza kimeshuka toka 12% mwaka 1999 hadi 5.7% mwaka 2007 hii ni kutokana na ushirikiano wa dhati kati ya Halmashauri ya jiji na wadau wake" Ilisema sehemu ya risala toka kwa wadau wanaojihusisha na masuala ua Ukimwi katika maadhimisho siku ya Ukimwi duniani desemba mosi 2011. Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Said Amanzi (shati la kitenge) akiwa na diwani wa kata ya Nyamagana Biku Khotecha kwenye Maadhimisho hayo yaliyofanyika katika Uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza. "Tathmini mbalimbali zinaonyesha kuwa bado kuna mianya ya mtu kuambukizwa VVU katika jamii kupitia ngono zembe na mtu aliyeambukizwa na VVU. Sababu nyingine ni pamo

Jitokeze kesho, 2nd Dec, 2011 Ukumbi IFM ktk Mkutano wa wadau ulioitishwa na TANESCO!Kukataa ongezeko la bei ya umeme

Kesho tarehe 2 Disemba 2011 katika Ukumbi wa Makumbusho Dar es salaam (mkabala na IFM) kuanzia saa 4 asubuhi EWURA imeitisha Mkutano wa Wadau kujadili ombi la TANESCO la kupandisha bei ya umeme kwa wastani wa 155% (zaidi ya mara tatu ya bei ya sasa). Nawaomba wanamtandao wote tuhamasishe umma kwa kutumia TEHAMA (sms, facebook, twitter, email na njia nyingine) ili wananchi waweze kuhudhuria mkutano husika kwa wingi na kutoa maoni. Mtakumbuka kwamba tarehe 23 Novemba 2011 nilitoa taarifa kwa umma kwamba Serikali inapaswa kusitisha ombi la dharura la kupandisha bei ya umeme kwa kiwango kikubwa ili kuepusha athari katika usalama na uchumi kutokana na mfumuko wa bei na kupanda kwa gharama za maisha. Aidha, serikali inapaswa kuchukua hatua za haraka kulinusuru Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) dhidi ya mzigo mkubwa wa gharama unaotokana na ufisadi wa muda mrefu katika mikataba ya gesi asilia na gharama za mitambo ya kufua umeme wa dharura badala ya kuweka mkazo katika ku

How to Write a Business Proposal

You have a great idea for a new product or service. Before a bank or investment firm will lend you money to get off the ground, you'll need to craft a solid business proposal. Follow these relatively simple steps to get your foot in the door on getting enough mullah to survive the arduous task of developing your product and making your dream a reality. 1. Talk with somebody who has written several successful business proposals. Ask what worked and what didn't. 2. Outline a two-part proposal. The first part will describe the business opportunity and your plans to take advantage of it. The second will present financial data - tax returns, a balance sheet and a summary of your operating plan. 3.Write the proposal. Limit the first part to 10 pages. Make it concise and clear. When describing the market opportunity, cite sources. 4.Explain what makes you and your company different from competitors. Perhaps you have special skills and experiences. You might have a new technology. Talk

NIGERIA YAPITISHA SHERIA YA KUPIGA MARUFUKU USHOGA

Kwa kile Kinachoonekana kama kuikomoa Uingereza na wanaharakati wa haki za mashoga, Bunge la senate la nigeria limepitisha Sheria ya Kuzuia Ushoga nchini humu. Ikumbukwe kuwa katika nchi zilizo endelea Ushoga unachangia zaidi ya asilimia 60% ya Maambukizi ya VVU. Suala la Kujiuliza ni kuwa wakati tunasimamia maadili ya Kiafrika na kuepuka ukiritimba wa Nchi zilizoendelea wa masharti mabovu ya Misaada, Je hatua hii ina manufaa au hasara gani katika mapambano na VVU? . Mfano Tanzania VVU kwa mashoga ni zaidi ya 12%. Je ni busara kuufumbia macho ushoga kimaadili na kuendeleza harakati za kuzuia VVU kwa jamii hiyo? Au ni vema kufumba macho kwa wanaharakati wa haki za Jamii hiyo na Kusimamia maadili yetu? Majibu Unayo

HAPPY BIRTHDAY FREDRICK BUNDALA (SKYWIZZY)

Image