MAKALA YA WILLY EDWARD NA KUHAMA KWA MWANAMUZIKI CHARLES BABA KUTOKA AFRICAN STARSBENDI YA
NAMFAHAMU vyema na nimekuwa nikifuatilia nyendo zake kwa karibu mwanamuziki nguli wa bendi ya African Stars 'Twanga Pepeta', Charles Gabriel Cyprian 'Chaz Baba' tangu alipotua bendi hiyo akitokea Mchinga Sound. Wakati huo Mchinga Sound ilikuwa ikimilikiwa na aliyepata kuwa Naibu Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo na Naibu Waziri wa Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi na Mbunge wa Jimbo la Mchinga, Mudhihir Mudhihir. Uhamisho wa Chaz Baba kutoka Mchinga Sounda kwenda Twanga Pepeta ulizua tafrani kubwa kati ya Mudhihir na Mkurugenzi wa Kampuni ya African Stars Entertainment Tanzania (ASET), Asha Baraka, hadi kufikia hatua ya kurushiana makonde Leaders Club. Tuyaache hayo! Chaz Baba ambaye ni mwimbaji, mtunzi na rapa, alizaliwa mwaka 1981 jijini Dar es Salaam. Alipata elimu ya msingi na sekondari lakini aliishia kidato cha pili mwaka 2004. Shughuli za muziki alianza tangu akiwa masomo