Daladala katika mitaa ya Mwanza. K ile kipindi cha Daladala kinachorushwa kila siku kupitia ITV kikifanyika ndani ya Daladala ambamo humo abiria hujadiliana masuala mbalimbali yanayozunguka katika harakati za maisha yao ya kila siku, sasa ni zamu ya mkoa wa Mwanza hivyo basi ukikutana na Daladala maeneo ya Nyegezi, Kilimahewa, Pansiasi, Igombe, Igoma, Mabatini, Magu na kwingineko kote panda kisha husika.... Mtangazaji wa kipindi cha Daladala kinachorushwa kupitia ITV Daniel Kijo akisalimiana na mkuu wa mkoa wa Mwanza Erenest Ndikilo, pindi crew ya kipindi hicho ilipodhuru ofisini kwa mkuu huyo jijini Mwanza leo tayari kuanza shughuli zake rasmi kuanzia wiki ijayo siku ya jumatatu. Jenerali Ulimwengu akizungumzia mdahalo wa Uhuru wa vyombo vya habari uliofanyika jana katika chuo cha SAUT -Mwanza . Mdahalo ulilenga kuainisha maeneo yanayohusiana na uhuru wa vyombo vya habari ni changamoto zipi, matatizo yapi, wapi kunahatarisha uhuru wa tasnia ya habari, ni namna gani y