Jeneza lenye mwili wa marehemu Msafiri Jonathan Mbwambo (38) likishushwa kwenye gari kwa maandalizi ya wananchi kutoa heshima zao za mwisho katika viwanja vya Ngusero, Usa-River jana. Shughuli hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa dini, viongozi wa chama, RPC wa Mkoa wa Arusha, Mkuu wa Wilaya ya Arumeru, OCD wa Arumeru na wananchi wengine. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Thobias Andengenye (katikati) akifuatilia hotuba za wasemaji wa makundi ya jamii yaliyowakilishwa. Kutoka kushoto anaonekana kwa mbali Mh Vicent Nyerere (Musoma), Mh Joshua Nassari (Arumeru Mashariki), Mh Godbless Lema, Mh Cecilia (Viti Maalumu), Kamanda Andengenye, na OCD John wa Arumeru Kamanda Andengenye akisalimia wananchi. Baadae aliahidi kuwa Jeshi lake litatoa zawadi ya shilingi milioni 10 kwa mtu atakaesaidia kupatikana kwa waliohusika na mauaji hayo na kwamba Polisi watahakikisha wanawasaka wahalifu hao kwa udi na uvumba hadi wapatikane. Mbunge wa Arumeru Mash