Posts

Wanavijiji 4 Hanang' vyapokea hati za umiliki wa kimila wa ardhi

Image
Wenyekiti wa vijiji vinne vya wilaya ya Hanang’ wamepokea hati za hakimiliki za kimila za ardhi ya vijiji vyao baada ya kuwa vimepimwa na wao kupewa mafunzo ya matumizi bora ya ardhi kwa ufadhili uliotolewa na shirika la Oxfam kupitia shirika la Ujamaa Community Resource Team - UCRT. Vijiji hivyo vya Mureru, Ming'enyi, Dirma na Gehando vimekabidhiwa hati hizo na katibu tawala wa Wilaya ya Hanang’ John Gabriel aliyemuwakilisha mkuu wa wilaya hiyo katika hafla fupi iliyofanyika katika kijiji cha Mureru na kuhudhuriwa na wakazi zaidi ya 100 kutoka katika vijiji hivyo vinne. Akiongea kwa niaba ya wenyeviti wa vijiji hivyo vinne, Mbisha Gicharoda ambaye ni mwenyekiti wa kijiji cha Ming’enyi aliyashukuru mashirika ya Oxfam na UCRT kwa kuwapatia elimu ya matumizi bora ya ardhi na kuwasaidia kupata hati za hakimiliki za ardhi ya vijiji. "Sisi kama wafugaji tulikua hatujui thamani ya ardhi yetu, sasa tumeamka na kujua haki zetu na manufaa ya kuwa na cheti cha umil

PPRA Yafungia Makampuni 7 Kwa Udanganyifu, Yatoa Ripoti ya Mwaka

Image
Mwenyekiti wa Bodi ya PPRA, Balozi Matern Lumbanga Mwenyekiti wa Bodi ya PPRA, Balozi Matern Lumbanga (Kulia) akiongea na waandishi wa habari, Kushoto ni Afisa Mtendaji Mkuu wa PPRA, Dk. Laurent Shirima. Mamlaka ya Ununuzi wa Umma (PPRA), imeyafungia makampuni 7 pamoja na wakurugenzi wake kutokana na vitendo vya udanganyifu. Akizungumza na waandishi wa habari leo katika makao makuu ya PPRA, Mwenyekiti wa Bodi ya PPRA, Balozi Matern Lumbanga amesema kuwa Mamlaka hiyo imeamua kuyafungia makampuni hayo kwa mujibu wa kifungu cha 62 cha Sheria ya Manunuzi ya Umma Na. 7 ya Mwaka 2011 na Kanuni ya 98 ya Tangazo la Serikali Na. 446 la Mwaka 2013. Aidha, Balozi Lumbanga alisema kuwa kati ya makampuni hayo, Gagaja Contractors Company Limited, limefungiwa kwa kipindi cha miaka 10 (kutoka tarehe 2 Oktoba,2015 hadi 1 Octoba, 2025) kwa kosa la kuwasilisha dhamana za zabuni za kughushi wakati wa michakato ya zabuni. Aidha, Balozi Lumbanga alisema kuwa m

Maonyesho ya Mavazi Kuhamasisha AMANI TANZANIA

Image

Magoli ya Mbwana Samatta katika mechi dhidi ya Al Merreikh na kuifikisha TP Mazembe fainali.

Image
          Klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imetinga hatua ya fainali ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika baada ya kuibuka na ushindi wa goli 3-0 dhidi ya klabu ya Al Merreikh ya Sudan , huu ni mchezo wa pili wa marudiano baada ya ule wa awali kuchezwa Sudan wiki kadhaa nyuma. Mtanzania Mbwana Samatta amesaidia timu yake kupata ushindi wa goli 3-0 katika mechi hiyo ya marudiano baada ya kufunga goli mbili dakika ya 53 na 69 kabla ya Assale kupachika goli la tatu dakika ya 71. TP Mazembe inaingia hatua ya fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuifunga Al Merreikh  kwa jumla ya goli 4-2 idadi ya goli hizo ni pamoja na mechi ya kwanza Sudan . Mtanzania mwingine anayeichezea klabu hiyo Thomas Ulimwengu alipata nafasi ya kuingia dakika ya 58 ya mchezo baada ya kuchukua nafasi ya Kalaba , Ulimwengu hakupata nafasi ya kufunga goli ila alikuwa ni moja kati ya waliotengeneza goli la pili

Rais Kikwete ateua Wakuu wapya wa Wilaya 13 na kuhamisha 7

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amewateua wakuu wa wilaya wapya 13 na kuwahamisha vituo vya kazi wengine saba. Wakuu wa wilaya 13 walioteuliwa ni Shaaban Athuman Ntanambe ambaye anakuwa Mkuu wa Wilaya ya Chato, Mkoa wa Kagera; Thabisa Mwalapwa ambaye anakuwa Mkuu wa Wilaya ya Hanang, Mkoa wa Manyara; Richard Kasesera ambaye anakuwa Mkuu wa Wilaya ya Iringa, Mkoa wa Iringa, Ruth Msafiri ambaye anakuwa Mkuu wa Wilaya ya Kibondo, Mkoa wa Kigoma na Abdallah Njwayo ambaye anakuwa Mkuu wa Wilaya ya Kilwa, Mkoa wa Lindi. Wakuu wa Wilaya wengine wapya ni Asumpta Mshama ambaye anakuwa Mkuu wa Wilaya ya Wanging’ombe, Mkoa wa Njombe; Mohammed Mussa Utaly ambaye anakuwa Mkuu wa Wilaya ya Mpwapwa, Mkoa wa Dodoma; Dauda Yasin ambaye anakuwa Mkuu wa Wilaya ya Makete, Mkoa wa Njombe; Honorata Chitanda ambaye anakuwa Mkuu wa Wilaya ya Ngara, Mkoa wa Kagera; Vita Kawawa ambaye anak

US Green Card Lottery / DV-2017 Program now accepting applications

Online registration for the DV 2017 Program begun on Thursday, October 1, 2015 and concludes on Tuesday, November 3, 2015. Visit the following link to the US Official website for details: http://www.travel.state.gov/content/visas/en/immigrate/diversity-visa/instructions.html

Kielelezo cha NEC cha namna ya kupiga kura

Image

NHC YAZINDUA UUZAJI WA NYUMBA ZA BIASHARA NA MAKAZI ZA MOROCCO SQUARE

Image
 Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angela Kairuki akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa mauzo ya nyumba za biashara na makazi-Morocco Square uliofanyika jijini Dar es Salaam, mwishoni mwa wiki. (Picha na Francis Dande)  Baadhi ya wageni waalikwa wakiwa katika hafla hiyo.   Naibu Wazriri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angela Kairuki akiwa na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu.   Wageni waalikwa.  Wageni waalikwa.   Naibu Wazriri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angela Kairuki akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu.   Burudani ya muziki. Burudani ikiendelea.   Naibu Wazriri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angela Kairuki akiteta jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mchechu.    Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), Nehemia Mche

MAGAZETI YA LEO JUMATATU, OCTOBER 5

Image
. . . . . . . . . . . . . . . . . . . .