HOSPITALI YA MUSOMA YAKABILIWA NA TATIZO LA UPUNGUFU WA DAMU
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
HOSPITALI ya mkoa wa Mara mjini Musoma bado inakabiliwa na tatizo kubwa
la upungufu wa damu jambo ambalo limetajwa wakati mwingine kuchangia
vifo hasa vya wanawake wajawazito na watoto.
Mganga mfawidhi wa
hospitali ya mkoa wa Mara Dk Joseph Nyamagwira Amesema kupungua kwa
damu katika hospitali hiyo kumetokana na mwamko mdogo wa wananchi katika
kuchangia damu hiyo hivi sasa.
Amesema ingawa hospitali imekuwa ikijitahidi kuhifadhi sehemu ya damu
kwa ajili kukabiliana na dharura,lakini wakati mwingine benki ya damu ya hospitali hiyo imekuwa ikiishiwa kabisa ikiwemo damu ya kundi la O
jambo ambalo limekuwa likisabisha wagonjwa wa kundi hilo kupoteza
maisha.
Hata hivyo Dk Nyamagwira,amesema pamoja na ndugu za
wagonjwa kujitolewa kuchangia damu hiyo,lakini kutokana na magonjwa
yaliopo hivi sasa damu hiyo imekuwa haitumiki kumuongezea mgonjwa wakati
huo hadi ipelekwe kwenye vipimo vikubwa katika hospitali ya rufaa ya
Bugando jijini Mwanza ambapo zaidi ya asilimia 50 ya damu hiyo mara
nyingi imekuwa ikimwagwa baada ya kubainika kuwa si salama.
Kwa
sababu hiyo ametoa wito kwa taasisi za shule,vyuo,majeshi na watu
binafsi kurudia zoezi kama ilivyokuwa awali kwa kujitolea kutoa damu
ambayo itasadia kuokoa maisha ya watu wengine wakiwemo watoto,wanawake
wajawazito na wananchi wanaopatwa na majanga ya ajali.
Taarifa hii ni kwa hisani ya Agustino mgendi mwakilishi wa blog hii kutoka Musoma.
Taasisi mpya ya binafsi inayotoa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu imeanzishwa, kwa wale ambao ndugu zao wamekosa mikopo kupitia taasisi ya serikali ya utoaji wa mikopo ya elimu ya juu HESLB wanaweza kuwashauri waombe huko. taasisi hiyo inaitwa HLSSF ( Higher Learning Students Supporting Fund) kwa maelezo zaodi tembelea tovuti hii hapa http://www.hlssf.org/ Taasisi hii inatoa huduma zingine kama ifuatavyo Inatoa mikopo kwa wanafunzi wa elimu ya juu kwa ajili ya kuwasaidia kulipa karo,kununua chakula,kulipia gharama za malazi,kununua vitabu na kufanya utafiti pamoja na mafunzo kwa vitendo. Inawatafutia scholarship za kusoma ndani na nje ya nchi wanafunzi wote ambao wanasifa za ufaulu stahili kadiri ya masharti ya wafadhili. Inawatafutia kazi wahitimu wote wa vyuo vikuu.Hii inafanywa kwa kuwakutanisha wahitimu na waajiri kadiri ya fani zao. Inatoa fursa ya kuwasaidia wahitimu wa vyuo na vijana wengineo wanaotaka kujiajiri katika fani za kiso...
Chukua japo dakika 10 za kusoma kitabu cha mwanamalundi, mtu maarufu aliyewahi kutokea katika historia ya kabila la kisukuma, hizi ni picha nilizozitoa katika kitabu hicho chenye karatasi kama 7, ni mojawapo ya kitabu nilichotamani kukisoma kupata ukweli juu ya mtu huyu, kwa bahati nzuri nimekikuta kwa mama yangu mkubwa katika kabati lake la vitabu, hivyo nikaona sio mbaya nikiweza kushare na marafiki zangu ambao nao wanatamani kujua historia ya mtu huyu maarufu kuwahi kutokea hapa Tanzania.
Comments
Post a Comment