Uingereza kuwabana wanafunzi wa kigeni
Sheria kali zilizoanzishwa nchini Uingereza kuhusu wanafunzi kutoka nje ya ulaya wanaokuja nchini humo kwa masomo zitawafanya wanafunzi wengi kutoka barani Afrika kutoweza kusomea Uingereza. Idara ya uhamiaji Uingereza - UK Border Agency, imesema watu wengi wametumia vibaya na kukiuka sheria za uombaji wa viza hasa za wanafunzi. Serikali ya Uingereza imeongezea vikwazo kupiga vita ukiukaji wa sheria hizi. Ukiukaji wa sheria umekuwa ukifanyika kufuatia kukomeshwa kwa uchunguzi uliokuwa ukifanywa kuhakikisha kwamba wanafunzi wanarudi nchini mwao baada ya kumaliza masomo yao na mda waliopewa na idara ya uhamiaji Uingereza kumalizika. Ingawaje wanafunzi wanachunguzwa kabla ya kupewa viza, hawajakuwa wakichunguza hivi karibuni kuhakikisha kwamba wamerudi nchini mwao.Imekuwa vigumu kujua idadi ya wale wanaorudi na wale wanaoishi Uingerza kinyume cha sheria. Idara ya uhamiaji inasema kwamba itakuwa vigumu sana kuvunja sheria za uhamiaji siku zijazo. Mnamo mwaka 2011, Idara hio itakuwa na tech