Posts

Showing posts with the label MAKALA

MHADHIRI DENIS MPAGAZE: KIGEZO CHA KUTUMWA NA WAZEE KUGOMBEA NAFASI YA UONGOZI NI HOJA DHAIFU

Kuna baadhi ya maandishi ukiyasoma basi kuna kitu lazima kitakugusa, na hii ndio inanisukuma kukichukua alichokiandika mwalimu wangu Mr. Mpagaze aliyenifundisha maswala ya mawasiliano ya umma mwaka wa pili nilipokuwa chuoni St. Augustine (SAUT) Denis Mpagaze Mtu unajijua kabisa uwezo wa kuwa kiongozi hauna. Kwa sababu ya tamaa na njaa zako unaamua kuwaadaa wananchi kwamba wazee wa mji wanakutaka ukagombee. Achana na hoja dhaifu! Kwanza kwa kauli hiyo ya kutumwa na wazee inaonesha jinsi unavyotegemea watu wafikiri kwa niaba yako na wakati kiongozi bora ni yule anayeonesha njia. Unaendeleza utamaduni wa kubebwa bebwa (Godfathers). Yaani ni ishara ya kwamba hata uk ipata madaraka hutakuwa na uwezo wa kufanya maamuzi, badala yake utawaachia wazee kufanya maamuzi kwa niaba yako na kuipoteza jamii. Nasema hivi kwa sababu wazee watakushauri uwe na hofu ya maisha na kuishia kuwaibia wananchi.Kama huamini ninachokisema, angalia mafisadi wakubwa na wahujumu uchumi nchi hii karibu wote ni waze

MBONGO AUAWA KWA SUMU UJERUMANI

Image
Marehemu Robert John Mpwata (34) enzi za uhai wake. Na Makongoro Oging’, Issa Mnally/Uwazi MTU mmoja anayeaminika kuwa ni Mtanzania, Robert John Mpwata (34) anadaiwa kuuawa kwa kuwekewa sumu na mwili wake kukutwa chumbani kwake katika Mji wa Shorten nchini Ujerumani siku chache zilizopita. Habari kutoka kwa baadhi ya marafiki zake waliopo huko, zinasema Robert aliyekuwa mwanamichezo aliyecheza sarakasi, karate na judo, aliwasiliana nao kwa njia ya simu mara kwa mara na walipata taarifa za kifo chake siku saba ya kufariki dunia. Inadaiwa kabla ya kifo cha mwanamichezo huyo, alikuwa akiwasiliana vizuri na wenzake, lakini umauti wa ghafla uliomkuta na mazingira yake, unawapa hofu kuwa huenda alifariki baada ya kuwekewa sumu. Inadaiwa kuwa Februari 8, mwaka huu ilikuwa ni siku waliyotakiwa kufanya onyesho, kitu ambacho kiiwafanya wawe na mawasiliano ya mara kwa mara. Mwandishi wa habari hii aliwasiliana na ubalozi wa Tanzania nchini Ujerumani, ambako mfanyaka

Saratani ya tezi dume ni muuaji wa kimyakimya

Image
Watu wengi wamekuwa na shauku ya kutaka kujua ugonjwa wa saratani ya tezi dume, huku wakidhani ni mpya. Lakini ukweli ni kuwa umekuwapo miaka mingi na wengi wameugua. Takwimu zinaonyesha wanaume wengi huugua ugonjwa huu unaoongezeka kwa kasi ya hali ya juu. Kulingana na utafiti uliofanywa na Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORIC), kutoka mwaka 2006, zinaonyesha kuwa kila mwaka kumekuwa na ongezeko la kesi mpya ya wagonjwa saratani ya tezi dume. Novemba ya kila mwaka, jumuiya za kimataifa huadhimisha tukio ambalo hujulikana kama Movemba. Maadhimisho hayo huhusisha kukuza kwa masharubu, kukusanya fedha na kuleta mwamko na ufahamu wa masuala ya afya kwa wanaume kama vile saratani ya tezi dume. Jina hilo la Movemba ni mchanganyiko wa neno ‘Masharubu na Novemba’. Maadhimi

Mikopo elimu ya juu yabagua masomo

Image
Dodoma. Mbunge wa Viti Maalumu (CCM), Ritta Kabati ameihoji Serikali kuwa kwa nini Sera ya mikopo kwa elimu ya juu inatolewa kwa kozi za sayansi na ualimu badala ya kutoa mikopo kwa kozi zote. “Serikali hutenga fedha nyingi kila mwaka kwa ajili ya Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu ili vijana wanaojiunga na vyuo vikuu wakopeshwe, sasa kwa nini inaupendeleo?” alihoji. Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Jenister Mhagama alisema utoaji wa mikopo hufuata taratibu za kisheria na miongozo ya Serikali hasa katika vipaumbele vya Taifa. “Mahitaji ya kitaifa ndiyo yanayoiongoza Serikali kuainisha programu zinazopewa kipaumbele katika kutoa mikopo kwa nia ya kuwashawishi wanafunzi wasome,” alisema. Alisema kuanzia mwaka wa masomo 2014/2015 vipaumbele vya Taifa ni Ualimu wa sayansi na Hisabati, Sayansi za Tiba, Uhand

UCHAMBUZI WA GEORGE MARATU JUU YA WABUNGE WA MKOA WA MARA WENYE NAFASI YA KURUDI BUNGENI, AMTAJA MBUNGE MMOJA TU MWENYE NAFASI

Utafiti huu umefanywa na mwandishi wa ITV bwana George Maratu juu wa wabunge wa mkoa wa Mara wenye nafasi ya kuweza kurudi bungeni mwaka 2015, utafiti huu nime ucopy kwa jinsi ulivyo bila ku edit chochote kutoka katika account yake ya facebook. Nikachukulia kigezo cha prominance kwa kuwa wabunge hawa wanawakilisha maeneo ambayo mimi Nyanja ninatokea. TAHADHALI…CHANGIA HOJA HII KWA HOJA BILA KUJALI KUWA WANAOTAJWA WAKIPOTEZA UBUNGE BASI NA KITUMBUA CHAKO KITAJAA MCHANGA…Utafiti wa miezi sita iliyopita, umeonyesha wazi kwa mkoa wa Mara ni Mbunge mmoja tu anaweza kurudi 2015 kwa asilimia 80 hadi sasa… Jimbo la Tarime mbunge Nyambari Nyangwine (CCM) kurudi kwake ni asilimia 7 tu hadi sasa,sababu hajatekeleza ahadi zake,kushindwa kutembelea wapiga kura, mbali na kuonekana wakati wa matukio tena pengine kwa kujificha jificha na kikubwa kutuhumiwa kuwa mmoja ya watu wanaongoza makundi ndani ya chama chake ingawa pia serikali yake ya CCM imesaidia kutatua baadhi ya changamot

MAKALA: JE UMEANDAA MASWALI YA KUMUULIZA KIONGOZI WAKO KABLA YA UCHANGUZI UNAOKUJA? SOMA MAKALA HII KUTOKA KWA MHADHIRI MSAIDIZI CHUO CHA SAUT.

Mwandishi wa makala hii ni mhadhiri msaidizi na mkuu wa Idara ya mawasiliano na uandishi wa habari Chuo Kikuu Kishiriki cha Mt. Agustino cha Tanzania (SAUT) Songea. Anapatikana kwa denis_mpagaze@yahoo.com, 0753665484 au unaweza kusoma makala zake kupitia ukurasa wake wa facebook Denis Mpagaze Ubabe, dharau, kejeli na unafiki ni dhambi ambazo zinalitafuna Taifa letu kwa kasi zaidi ya upepo. Nchi yetu imegeuka kuwa kisima cha ubabe, vitisho na dharau. Kitendo cha Mbunge wa Kasulu kuhoji mstakabali wa nchi yetu na kuitwa tumbili ni ubabe, dharau na kejeli. Kitendo cha wananchi wa Kigamboni kuhoji uhalali wa kuongezeka kwa nauli ya kivuko na kuambiwa asiyeweza kulipa apige mbizi ni dharau. Kitendo cha wananchi kuambiwa maji sio mkojo kupatikana kila sehemu ni kebehi. Kitendo cha wananchi kuuliza uhalali wa kigogo kutumia ndege ya serikali na kujibiwa mlitaka atumie punda ni majivuno. Kitendo cha waandishi wa habari kuhoji mstakabali wa nchi yetu na kuishia kung’olewa k