Posts

Showing posts from October, 2014

FAHAMU DALILI ZA AWALI KAMA MPENZI WAKO ANAKUSALITI (ANACHEPUKA) ‪

Image
Wataalam wa misemo wanasema ‘ajali haina kinga’, lakini ukweli ni kwamba kuna dalili au tabia ambazo hupelekea ajali na unaweza kuzitumia kuikwepa ajali panapowezekana. Moja kati ya sababu kubwa inayovunja uhusiano kati ya wawili walioanza mapenzi kwa kula kiapo au kuahidiana mengi wakipendana sana ni ‘USALITI (MICHUPUKO)’. Na usaliti huu mara nyingi hufanywa kwa kificho sana, lakini ukiwa makini sana na uhusiano wako unaweza kuanza kugundua mapema kama mpenzi wako anakusaliti. Hizi ni dalili 5 za awali kufahamu kama mpenzi wako anachepuka…zipo dalili nyingi lakini leo tunakupa dalili zinazojikita kwenye mlengo wa MABADILIKO.. 1. ANGALIA KAMA ANA MABADILIKO YA RATIBA NA MAELEZO YA KILE ANACHOFANYA Angali kama amebadilisha ratiba ya kurudi nyumbani akiwa amechelewa sana kutoka kazini tofauti na awali, na pia maelezo yake ukiyafuatilia kwa ukaribu yanakuwa na sababu tofauti na alizowahi kukueleza kwa utaratibu wa ofisi yake awali. Angalizo: kuna wakati mabadiliko haya ya ratiba yanawez

AIBU ILIYOJE! MUME WA MTU ANASWA NDANI YA DANGURO

Image
Na Waandishi Wetu NI aibu iliyoje! Mwanaume mmoja ambaye anadaiwa kuwa ni mume wa mtu, amekutwa ndani ya danguro moja lililopo Sinza ya Mapambano jijini Dar ikiwa ni mazingira ya kutatanisha. Njemba huyo akisihi kuachiwa baada ya sakata hilo. Ishu hiyo ilijiri usiku wa manane wa Ijumaa kuelekea Jumamosi ya wiki iliyopita. Awali, Oparesheni Fichua Maovu (OFM) ya Global Publishers ilipokea taarifa kutoka kwa vyanzo vyake kuwa ndani ya danguro hilo, ameingia mwanaume huyo aliyeonekana kuwa na heshima zake na kwa vile inaeleweka vitu vinavyoendelea, vyanzo vilikuwa na wasiwasi naye!Bila kupoteza muda, kikosi kazi cha OFM kilifuatilia eneo hilo na kufanikiwa kuingia ndani ya danguro hilo ambako walimkuta jamaa huyo akiwa anazungumza na wasichana watatu ingawa haikueleweka mara moja walikuwa wakizungumzia nini. Mmoja wa changudoa hao akikurupushwa kutoka kwenye danguro hilo. Baada ya kuwaona makamanda wa OFM, waliacha mazungumzo yao na

KADINDA AMUANIKA MPENZI

Image
Na Imelda Mtema MWANAMITINDO maarufu Bongo, Martin Kadinda ameamua kumuweka wazi mpenzi wake ambaye siku za nyuma alikuwa na mpango wa kufunga naye ndoa mapema mwaka huu lakini kukatokea tofauti kidogo wakahairisha zoezi hilo. Mwanamitindi maarufu Bongo, Martin Kadinda akiwa na mpenzi wake. Akizunguza na  mwandishi wa habari hivi karibuni, Kadinda  aliweka wazi kuwa huyo ndio mke wake mtarajiwa na Mungu akipenda watafunga naye ndoa mwakani.  “ Ni kweli ni mpenzi wangu nampenda sana na Mungu akipenda ndiye mke wangu ambaye nitafunga naye ndoa mapema tu mwakani na Mungu atusimamie katika hilo,” alisema Kadinda.  Na Imelda Mtema MWANAMITINDO maarufu Bongo, Martin Kadinda ameamua kumuweka wazi mpenzi wake ambaye siku za nyuma alikuwa na mpango wa kufunga naye ndoa mapema mwaka huu lakini kukatokea tofauti kidogo wakahairisha zoezi hilo. Mwanamitindi maarufu Bongo, Martin Kadinda akiwa na mpenzi wake.

MTANDAO GANI WA SIMU UNATUMIA? SAIDIA KUFANIKISHA UTAFITI HUU

MAMBO VIPI MDAU? KUNA UTAFITI UNAFANYIKA KUHUSIANA NA HUDUMA ZA SIMU ZINAZOTOLEWA NA MAKAMPUNI YALIYOPO HAPA NCHINI TANZANIA, TAFADHALI MDAU TUMIA DAKIKA ZAKO MBILI TU KUJAZA FOMU HII KWA KUPONYEZA LINK HII, NI RAHISI SANA, NATANGULIZA SHUKURAN ZA DHATI KABISA KWA WOTE MTAKAOTUSAIDIA KUFANIKISHA UTAFITI HUU. Mtandao gani wa simu unatumia? Je! ungependa kutoa maoni yako sasa? Bonyeza link hii https://www.surveymonkey.com/s/MDRNVPH

RAIS MICHAEL SATA WA ZAMBIA AFARIKI

Image
Rais wa Zambia, Michael Sata enzi za uhai wake. RAIS wa Zambia, Michael Sata amefariki dunia jana usiku akiwa jijini London nchini Uingereza alipokuwa akipatiwa matibabu baada ya kuugua kwa muda mrefu. Sata aliyeingia madarakani tangu Septemba 23, 2011 amefariki akiwa na umri wa miaka 77 katika Hospitali ya King Edward VII, London. Sata amefariki kwa ugonjwa ambao bado haujawekwa…

MAGAZETI YA LEO JUMATANO

Image

MSHIRIKI WA BIG BROTHER AFRIKA KUTOKA TANZANIA LAVEDA NA ALUSA WA KENYA WATOLEWA NJE YA JUMBA HILO

Image
Matumaini ya watu wengi kumuona mshiriki  kutoka Afrika Mashariki ndani ya jumba la Big Brother Africa kuibuka na ushindi, yameshuka kwa kiasi kikubwa baada ya washiriki kutoka nchi mbili za Afrika Mashariki kutolewa nje ya jumba hilo. Aliekuwa mshiriki wa Tanzania Laveda kwenye Big Brother Hotshots 2014. Wiki moja baada ya washiriki Lillian kutoka Nigeria, Esther kutoka Uganda na Sabina kutoka Kenya kutolewa kwenye mjengo huo, Mtanzania Laveda aliyekuwa na mahusiano ya karibu na Permithias pamoja na Mkenya Alusa wamekutana na ‘rungu’ la kura lililowatupa nje ya jumba hilo. Laveda anakuwa mshiriki wa sita wa jinsia ya kike kutolewa nje ya jumba la BBA huku Alusa akiwa ni mshiriki wa kwanza wa kiume kutolewa Big Brother Hotshots.

Dawa zitapatikana vipi mahospitalini wakati MSD inaidai Serikali bilioni 90?

UHABA mkubwa wa dawa na vifaa tiba umezikumba hospitali nyingi nchini, zikiwemo za Muhimbili na Ocean Road, kutokana na serikali kudaiwa zaidi ya sh. bilioni 90 na Bohari Kuu ya Dawa, (MSD). Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika lisilo la kiserikali linalofuatilia masuala ya afya nchini la SIKIKA, Irenei Kiria, alisema jana jijini Dar es Salaam kuwa hali hiyo inahatarisha maisha ya wananchi kwa kukosa matibabu. Irene alisema kutokana na madeni hayo, MSD imesimamisha usambazaji wa dawa katika hospitali za serikali, zikiwemo za rufani na za wilaya, hasa za Mpwapwa na Kiteto, ambazo zinadaiwa mamilioni ya shilingi. Alisema Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, kwa mfano, inadaiwa sh. bilioni nane, huku Hospitali ya Wilaya ya Kiteto mkoani Manyara, ikidaiwa sh. milioni 38. Kwa mujibu wa Kiria, ongezeko la deni hilo limekuwa likiathiri ufanisi na utendaji kazi wa MSD, kwakuwa taasisi hiyo haijiendeshi kwa faida. Alisema kutolipwa kwa fedha hizo kwa wakati kunaifanya MSD k

CHADEMA, CUF, NCCR MAGEUZI NA NLD VYATILIANA SAINI MAKUBALIANO YA USHIRIKIANO

Image
Viongozi wa juu wa vyama vinne vya siasa nchini Tanzania vimeingia makubaliano ya ushirikiano wa shughuli mbalimbali za siasa hii leo na miongoni mwa mambo hayo ni kusimamisha wagombea wa pamoja katika uchaguzi wa Serikali za Mtaa na Uchaguzi Mkuu wa wabunge, madiwani, wawakilishi na Rais 2015. Kutoka kushoto ni James Mbatia wa NCCR-MAGEUZI, Prof Ibrahim Li[pumba wa chama cha Wananchi CUF, Freeman Mbowe wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na Dk. Emmanuel makaidi wa NLD wakionesha hati yao ya makubaliano waliyoisaini jana katika viwanja vya Jangwani Dar es Salaam  Viongozi hao wakishangilia kuzaliwa kwa ushirikiano huo huku makatibu wao wakiwa wameketi.  kwa kuangalia siani za makubaliano wa ushirikiano bofya soma zaidi.  Wafuasi, wanachama, wa vyama vya siasa vinavyounda ukawa wakifuatilia mkutano h

NAHODHA WA BAFANABAFANA AUAWA

Image
Nahodha ambaye pia ni golikipa wa timu ya soka ya taifa la Afrika kusini Senzo Meyiwa enzi za uhai wake. Nahodha ambaye pia ni golikipa wa timu ya soka ya taifa la Afrika kusini Senzo Meyiwa amefariki dunia baada ya kupigwa risasi. Jeshi la polisi la nchi hiyo limesema. Tukio hilo limeripotiwa kutokea katika nyumba ya mpenzi wake iliyopo katika mji wa Vosloorus kusini mwa Johannesburg. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 aliichezea klabu ya Orlando Pirates na alicheza mechi nne zilizopita za timu yake ya taifa katika mechi za kufuzu za fainali ya mataifa ya Afrika. Jumamosi alikuwepo katika tukio la timu yake pindi waliposonga mbele katika nusu fainali ya ligi ya Afrika kusini. Katika maelezo yake Jeshi la polisi la afrika kusini limesema kwamba Meyiwa ameripotiwa kufariki wakati akiwasili hospitalini.  BBC

TUMA MAJINA MAWILI YA WANAWAKE UNAODHANI WANASTAHILI KUPEWA TUZO YA MWANAMKE BORA WA MWAKA 2014/15

Image
source:GP

MAHMOUD JUMA MLALI ABAINISHA VIPAUMBELE VYAKE VYA KUITUMIKIA SERIKALI YA MTAA WA REGENT ESTATE

Image
Mjumbe na Balozi wa nyumba kumi ndugu Mahmoud Juma Mlali atangaza na kunadi vipaumbele vyake katika kuwahudumia wakazi wa eneo la Regent Estate katika uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika tarehe 31 October 2014, kampeni zinaanza leo mpaka tarehe 27, hivyo mkazi wa Regent Estate jitokezeni kwa wingi kusikiliza sera za Bwana Mahmoud katika ofsi ya tawi Regent Estate leo saa 10 jioni.

Uboreshaji wa Daftari la Wapiga Kura kuanza katikati mwa Mwezi Novemba

Image
Na Magreth Kinabo,Maelezo Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) imesema kwamba zoezi la majaribio ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura linatarajia kuanza rasmi katikati mwa mwezi Novemba mwaka huu. Aidha NEC imefafanu kwamba zoezi hilo, litafanyika kwa kutumia mfumo mpya wa 'Biometric Voter Registration'(BVR) katika majimbo matatu ya uchaguzi ambayo ni Kawe katika Manispaa ya Kinondoni, Kilombero, Halimashauri ya Mji wa Kilombero na Mlele, Halimashauri ya Mlele, ambapo vituo vya uandikishaji vimewekwa katika kata zilizomo katika majimbo husika. (Martha Magessa) Hayo yalisemwa na Makamu Mwenyekiti wa NEC pia na Jaji Mkuu Mstaafu wa Zanzibar Mhe. Hamid Mahamoud Hamid,wakati akisoma taarifa kuhusu kuanza kwa shughuli za Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika leo jijini Dares Salaam. "Tume tayari imekwishapokea baadhi ya vifaa muhimu vya uandiki

PICHA: MAHMOUD JUMA MLALI ARUDISHA FOMU YA KUGOMBEA NAFASI YA UONGOZI SERIKALI YA MITAA

Image
Makabidhiano yakifanyika katika ofsi ya CCM tawi la Regent Estate Mgombea wa nafasi ya Uenyekiti wa serikali ya mtaa wa Regent Estate- Dar Es salaam Bwana Mahmoud Juma Mlali kupitia kura ya maoni CCM akirudisha fomu katika ofsi ya  CCM tawi la Regent Estate kwa Katibu  wa tawi ndugu Richard Chacha kabla ya kuanza kwa mchujo wa wagombea wa nafasi hiyo. Mahmoud Mlali akikabidhi fomu kwa katibu wa tawi la CCM Regent Estate