Posts
KONGAMANO LA KATIBA
- Get link
- Other Apps
JUMUIYA YA WANATAALUMA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM (UDASA) inawaletea: KONGAMANO LA KATIBA MADA KUU: MCHAKATO NA MAUDHUI YA KATIBA MPYA WAZUNGUMZAJI WAKUU: Prof. ISSA SHIVJI Ndg. JENERALI ULIMWENGU TAREHE: Jumamosi, 15 Januari 2011 UKUMBI: Nkrumah, Chuo Kikuu cha Dar Es Salaam MUDA: SAA 4:00 AsubuhiI hadi SAA 8:00 Mchana NYOTE MNAKARIBISHWA
DOGO JANJA ASEMA YEYE NI MUZIKI NA SHULE
- Get link
- Other Apps
MSANII mdogo kuliko wote wanaotamba kwa sasa hapa nchini Abduaziz Chende maarufu kama Dogo Janja amesema pamoja na umaarufu alioanza kuupata kamwe hawezi kulipa kisogo suala la elimu. Mwanahip hop huyo mwenye miaka 14 amesema kuwa anaamini eklimu ndiyo ufunguo wa maisha hivyo kutokana na umri wake kuwa mdogo hawezi kupoteza haki yake hiyo ya msingi sababu ya muziki. Kwa sasa msanii huyo aliyekuwa akiishi jijini Arusha yupo jijini Dar es Salaam na tayari ameshaanza kidato cha kwanza katika sekondari ya Makongo, huku akiendelea na muziki. Yatari msanii huyo ambaye anafanya kazi chini ya kundi la Tip Top Connection lenye maskani yake Manzese, Dar es Salaam amekamilisha yake ya pili iitayo I Get Money akimshirikisha Godzillah. Awali alitoka na wimbo unaoitwa "Anajua" aliowashirikisha Madee na Tundaman