DOGO JANJA ASEMA YEYE NI MUZIKI NA SHULE



MSANII mdogo kuliko wote wanaotamba kwa sasa hapa nchini Abduaziz Chende maarufu kama Dogo Janja amesema pamoja na umaarufu alioanza kuupata kamwe hawezi kulipa kisogo suala la elimu.
Mwanahip hop huyo mwenye miaka 14 amesema kuwa anaamini eklimu ndiyo ufunguo wa maisha hivyo kutokana na umri wake kuwa mdogo hawezi kupoteza haki yake hiyo ya msingi sababu ya muziki.
Kwa sasa msanii huyo aliyekuwa akiishi jijini Arusha yupo jijini Dar es Salaam na tayari ameshaanza kidato cha kwanza katika sekondari ya Makongo, huku akiendelea na muziki.
Yatari msanii huyo ambaye anafanya kazi chini ya kundi la Tip Top Connection lenye maskani yake Manzese, Dar es Salaam amekamilisha yake ya pili iitayo I Get Money akimshirikisha Godzillah.
Awali alitoka na wimbo unaoitwa "Anajua" aliowashirikisha Madee na Tundaman

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA