Posts

Team Diamond vs Team Alikiba: Kinachoendelea Instagram Kinatutia Aibu Watanzania!

Image
Upinzani kati ya Diamond Platnumz na Alikiba sasa unaelekea kubaya. Kiukweli nimesikitishwa sana na kile ambacho ninakiona kikiendelea kwenye Instagram kati ya kambi hizi mbili. Infact nahisi ushabiki huu una hasara nyingi kuliko faida kwenye industry yetu. Kwa leo sitaongelea jinsi ushabiki wa wasanii hawa wawili wenye nguvu unavyofanya wasanii wengine wanaofanya vizuri nchini kutoangaliwa, bali nitazungumzia kusikitishwa na kile kinachofanyika Instagram ambapo mashabiki wa Alikiba wameanzisha kampeni ya kuhakikisha kuwa Diamond anakosa tuzo kwenye MTV MAMA pamoja na mashabiki wa Diamond kumtukana Davido bila hatia! Kwanini lakini tunafanya hivi? Hivi kweli tunaamua kujidhalilisha kiasi hiki? Majirani zetu wanatucheka, wanatubeza, wanatushangaa kweli kweli! Ushindani huu wa ndani kati ya wasanii hawa wawili kwanini uondoe utaifa wetu? Ushabiki gani huu? Diamond Platnumz amechaguliwa kuwania vipengele vitatu kwenye tuzo za mwaka huu za MTV MAMA, iwapo akishinda, ushindi wake

BASI LA TAIFA STARS LASHAMBULIWA KWA MAWE, LAPASULIWA KIOO

Image
WATU wasiojulikana jana walilishambulia kwa mawe basi la timu ya soka ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars maeneo ya Kariakoo, Dar es Salaam. Basi hilo lililokuwa limebeba baadhi ya wachezaji wa tumu hiyo waliokuwa wakitoka mazoezini Uwanja wa Karume, Dar es Salaam lilishambuliwa kwa mawe na watu wanaosadikiwa kuwa mashabiki wenye hasira. Taifa Stars juzi ilifungwa mabao 3-0 na Misri katika mechi yake ya kwanza ya Kundi G kufuzu Fainali za Mataifa ya Afrika 2017 mjini Alexandria. Mabao yote ya Misri yalipatikana kipindi cha pili, wafungaji Rabia dakika ya 61, Morsi dakika ya 65 na Mohamed Salah dakika ya 70. Lakini wachezaji ambao walishambuliwa kwa mawe wakiwa kwenye basi hilo, hawakwenda Misri. Kikosi cha Stars kilichokuwa Misri, kinatarajiwa kuwasili leo na kuungana na wenzao waliobaki Dar es Salaam. Kwa pamoja wachezaji hao watakwenda kambini Zanzibar kwa maandalizi ya mchezo wa CHAN dhidi ya Uganda mwishoni mwa wiki. Kipigo cha Misri kilikuwa cha nne mfululizo kwa S

KURASA ZA MBELE NA NYUMA ZA MAGAZETI YA LEO JUMATANO,JUNE 17

Image

NEW VIDEO:Yamoto Band - Nisambazie Raha [Official Video]

Image

YALIYOTAWALA KATIKA MAGAZETI YA LEO TZ,JUNE 16

Image

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI, JUNE 13 YAPO HAPA

Image
MAGAZETI MENGINE YATAWAJIA HIVI PUNDE

MKURUGENZI MKUU WA TWITTER KUJIUZULU

Image
Mkurugenzi Mkuu wa Twitter, Dick Costolo anayetarajia kujiuzulu. Mkurugenzi Mkuu wa Twitter, Dick Costolo, ana nia ya kujiuzulu ifikapo Julai mosi, kufuatia shinikizo kutoka kwa wawekezaji, ambao wanalalamikia kukua polepole wa mtandao huo wa kijamii. Baada ya kujiuzulu nafasi hiyo ya Mkurugenzi Mkuu, Costolo atabaki kuwa Mjumbe wa bodi ya Wakurugenzi wa kampuni hiyo. Twitter imeshindwa kupata faida katika kipindi cha miaka tisa tangu ilipoanzishwa. Mwanzilishi mwenza wa mtandao huo Jack Dorsey anatarjiwa kuchukua nafasi hiyo kama kaimu Ofisa Mkuu kuanzia Julai mosi na kukalia wadhifa huo hadi pale mrithi wake atakapochaguliwa. Katika taarifa yake, Costolo amesema kuwa anafurahishwa na wafanyikazi wa kampuni hiyo. Mnamo mwezi Aprili kampuni hiyo ilipata hasara ya dola milioni 162 hivyo kufanya ukuaji wa kampuni kushuka kwa kiwango kikubwa na kuathiri uwekezaji. Bei ya hisa zake ilishuka kwa asilimia 30 na sasa zinaendelea kuuzwa kwa bei ya uanzilishi wake ya mwaka 20

HAPPY BIRTHDAY UNCLE ERICK MAKOBA

Image
 Every year I realize a bit more how lucky I am to have you as my uncle. Happy Birthday uncle..... May your birthday be as wonderful and fantastic as you.

150 KORTINI KWA KUJIANDIKISHA MARA MBILI DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGAKURA KWA MFUMO MPYA BVR

Image
  TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema watu 152 watafikishwa mahakamani mkoani Njombe kutokana na kujiandikisha mara mbili katika Daftari la Kudumu la Wapigakura kwa mfumo mpya wa ‘Biometric Voter Registration Kit’ (BVR). Aidha, imeeleza kuwa kata 130 zimeongezeka kutokana na Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kufanya mabadiliko ya kiutawala katika kata, vijiji,vitongoji na Mitaa hivyo kulazimu NEC kuhairisha kwa wiki moja uandikishaji wa daftari uliokuwa ukianza jana kwa baadhi ya mikoa. Kaimu Mkurugenzi wa Uchaguzi NEC, Dk Sisti Cariah alisema hayo jana wakati akielezea kuahirishwa kwa wiki moja uandikishaji hadi Juni 16 mwaka huu kwa mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Manyara na Mara. Akizungumzia suala la watu kujiandikisha mara mbili, alisema katika mkoa wa Njombe ambao Daftari hilo liko tayari na wiki ijayo litawekwa wazi kwa siku tano na kisha kufanyiwa marekebisho kwa siku moja na wamebaini watu 152 waliojiandikisha mara mbili. Alisema watu hao w

Picha za Rais Kikwete alipokutana na Watanzania The Hague, Uholanzi

Image
Watanzania waishio Uholanzi walikusanyika siku ya Jumatatu Juni 9, 2015 katika hoteli ya Crowne Plaza jijini The Hague kukutana na kumsikiliza Rais Jakaya Mrisho Kikwete aliyekuwa nchini humo kwa mwaliko wa Mfalme Willem-Alexander  Wajumbe walioongozana na Rais Kikwete katika ziara hiyo  Sehemu ya umati wa Watanzania waishio Uholanzi  Sehemu ya umati wa Watanzania waishio Uholanzi  Sehemu ya umati wa Watanzania waishio Uholanzi  Sehemu ya umati wa Watanzania waishio Uholanzi  Sehemu ya umati wa Watanzania waishio Uholanzi  Ujumbe wa Rais Kikwete  Balozi wa Tanzania nchini Uholanzi Mhe. William Masilingi akimkaribisha mgeni  Sehemu ya umati wa Watanzania waishio Uholanzi  Sehemu ya umati wa Watanzania waishio Uholanzi  Wadau wa Uholanzi wakiwa na furaha kumuona JK  Sehemu ya umati wa Watanzania waishio Uholanzi  Sehemu ya umati wa Watanzania waishio Uholanzi  Sehemu ya umati wa Watanzania waishio Uholanzi  Sehemu ya umati wa Watanzania waishio Uholanzi  Sehemu ya umati wa Watanzania