Posts

MKWASA ATANGAZA KIKOSI CHA TAIFA STARS...KIPO HAPA

Image
Kocha mpya wa Taifa Stars, Charles Boniface Mkwasa aliyechukua nafasi ya Mart Nooij ametangaza kikosi chake kipya kwa ajili ya kuivaa Uganda huku akimtema kipa Deogratius Munish ‘Dida’ na nafasi yake amemchagua Ally Mustapha ‘Barthez’. Wengine ambao Mkwasa amewatema ni Erasto Nyoni, Amri Kiemba na Kelvin Friday kutoka Azam FC pia Oscar Joshua kutoka Yanga, Pia Ibrahim Ajibu kutoka Simba. Waliorejea ni Kelvin Yondani pia Deus Kaseke huku akimchukua Michael Idan wa Ruvu Shooting. Pia Samuel Kamuntu wa JKT, Juma Abdul wa Yanga na Mudathir Yahya kutoka Azam wamejumuishwa kwamba wanaweza kuitwa wakati wowote. KIKOSI KAMILI: Mwadini Ally-Azam Ally Mustapha-Yanga Mudathir Khamis-KMKM Shomari Kapombe-Azam Michael Haidan-Ruvu Shooting Mohammed Hussein-Simba Mwinyi Hajj-KMKM Nadir Haroub-Yanga Kelvin Yondani-Yanga Aggrey Morris-Azam Hassan Isihaka-Simba Jonas Mkude-Simba Abdi Banda-Simba Simon Msuva-Yanga Said Ndemla-Simba Ramadhan Singano-

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI YAPO HAPA

Image

ARSENAL KUMSAJILI KIPA WA CHELSEA

Image
KIpa wa Chelsea Petr Cech Arsenal wanakaribia kuweka makubaliano ya kumsajili kipa wa Chelsea Petr Cech. Mazungumzo kati ya vilabu hivyo viwili yanaendelea huku kipa huyo akitarajiwa kuwa mchezaji wa kwanza atakayesajiliwa na Arsenal msimu ujao. Raia huyo wa Cech aliichezea Chelsea mechi 16 msimu uliopita na amekuwa katika uwanja wa Stanford Bridge kwa takriban miaka 11. Ameichezea Chelsea mara 300 na kushinda mataji 4 ya ligi,4 ya kombe la FA,mataji 3 ya kombe la ligi ,taji moja la vilabu bingwa Ulaya na taji moja la kombe la Yuropa. CHANZO:BBC  (Muro)

OWM YAPATA KOMBE KATIKA MAONYESHO YA UTUMISHI WA UMMA

Image
Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mhe. Ali Hassan Mwinyi akimkabidhi Kombe la ushindi Mchumi Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Idara ya Maendeleo ya Sekta Binafsi, Uwekezaji na Uwezeshaji Bw. Girson Ntimba baada ya Ofisi hiyo kuibuka mshindi wa kwanza katika Uratibu na Usimamizi Bora wa masuala ya Ukimwi wakati wa kilele cha Wiki ya Utumishi wa Umma tarehe 23 Juni, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) Wafanyakazi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wakifurahia kombe la Ushindi baada ya kuibuka mshindi bora katika masuala ya menejimenti ya Ukimwi wakati wa kilele cha Wiki ya Utumishi wa Umma tarehe 23 Juni, 2015. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu). chanzo:mjengwablog

NAPE AZUNGUMZIA UMUHIMU WA KUSHIRIKISHA WADAU WAKATI WA KUTUNGA SHERIA

Image

YALIYOTAWALA KATIKA MAGAZETI YA JUMATANO JUNE 24

Image

MAGAZETI YA LEO IJUMAA

Image
Na Awadh Ibrahim