Posts

KADA ACHUKUA FOMU, ATEMBEA HADI STENDI

Image
Kada wa CCM, Antony Chalamila (mbele kulia) akitembea kwa miguu wakati ekienda kutafuta basi la kumrejesha mkoani Morogoro, baada ya kuchukuwa fomu za kuomba kugombea kiti cha Urais kupitia chama hicho, mjini Dodoma jana. Picha na Edwin Mjwahuzi. Antony Chalamila (66) amekuwa mgombe wa 41 kuchukua fomu ya kuomba kupitishwa na CCM kuwania urais, lakini kivutio kilikuwa ni jinsi alivyochapa mguu kutoka ofisi za chama hicho hadi stendi ya mabasi kurudi mkoani Morogoro. Wakati kada huyo akijitokeza tano kabla ya muda wa kuchukua na kurejesha fomu kuisha, makada wengine wawili walirejesha fomu, huku Balozi Amina Salum Ali akilalamikia kukithiri kwa rushwa katika mchakato. Chalamila, ambaye aliongozana na msaidizi wake Benjamin Ruvunduka kwenda kuchukua fomu ofisi za makao makuu ya CCM, hakuwa na usafiri wowote wakati wa kuondoka na hivyo kutembea umbali wa takriban kilomita 1.2 kwenda kituo cha mabasi kurejea mkoani kwake Morogoro. (P.T) “Naelekea Morogoro hivi sasa wananisub

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI

Image

Buti "made in" Magereza Tanzania hili

Image
Muonekano wa viatu aina ya Buti vinavyotengenezwa katika Kiwanda cha Viatu cha Gereza Kuu Karanga Moshi, viatu hivyo hutumiwa na Maafisa na Askari wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama vikiwa tayari vimekwishatengenezwa kama vinavyoonekana katika picha. Wafungwa wa Gereza Kuu Karanga Moshi wakiwa wanashona viatu aina ya Buti ambavyo hutumiwa na Maafisa na Askari wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama hapa nchini kama wanavyoonekana katika picha wakishona sehemu ya juu ya viatu hivyo. Wafungwa hao wa Gereza Kuu Karanga wananufaika na Stadi ya Ushonaji viatu katika Kiwanda hicho kwa kujipatia ujuzi wa Ushonaji. Picha: Lucas Mboje / Jeshi la Magereza ( via )

LINAH AJIWEKA KIMAHABA KWA KAKA’AKE ZARI

Image
Staa wa Muziki wa kizazi kipya, Estelinah Sanga ‘Linah’ akiwa ameketi na William Bugeme ‘Boss Mtoto’ ambaye ni kaka wa Zarina Hassan ‘Zari’ kiukoo. MREMBO  anayefanya poa kunako Bongo Fleva, Estelinah Sanga ‘Linah’, anadaiwa ‘kujiegesha’ kimahaba kwa shemeji yake Mbongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ aitwaye William Bugeme ‘Boss Mtoto’ ambaye ni kaka wa Zarina Hassan ‘Zari’ kiukoo. Ndani ya Ukumbi wa Triple 7 uliyopo Kawe jijini Dar hivi karibuni, paparazi wetu aliwaona wakiingia sambamba na kukaa beneti kama mtu na mpenzi wake jambo lililozua maswali kibao kutoka kwa wateja waliokuwepo ukumbini hapo. Linah na Boss Mtoto katika pozi la kimahaba. Mbali na kunaswa siku hiyo, pia paparazi wetu amekuwa akiwashuhudia mara kadhaa wawili hao wakiwa pamoja katika kumbi mbalimbali za starehe jijini Dar. Mara ya mwisho, Linah na Boss Mtoto walikuwa pamoja kwenye hafla ya utoaji wa Tuzo za Kili Music zilizofanyika ndani ya Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar, mapema mwezi huu. Nd

NE-YO KUFANYA MAKAMUZI KWENYE TUZO AMBAZO DIAMOND NA VANESSA MDEE WANAWANIA!

Image
Ne-yo. STAA kutoka nchini Marekani ambaye ni mwimbaji, mwandishi wa mashahiri, dansa na mwigizaji, Ne-yo ni mmoja mwa wasanii watakaotoa burudani katika utoaji Tuzo za Muziki za MTV Africa (MAMAs) huko nchini Afrika Kusini. Taaarifa hiyo imethibitishwa na habari iliyowekwa katika akaunti ya Twitter ya MTV Africa ikieleza kuwa mkali huyo wa R&B tayari amethibitisha kupiga shoo katika tuzo hizo. Tuzo hizo zinatarajiwa kutolewa Jumamosi ya Julai 18, 2015 huko KwaZulu-Natal, Afrika Kusini ambapo Tanzania inawakilishwa na wasanii wawili Vanessa Mdee na Diamond Platnumz. Hawa ndiyo washiriki wetu katika tuzo hizo:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya Tarehe 26 Juni 2015

Image

MKOA WA DAR ES SALAAM WAMDHAMINI BERNARD MEMBE

Image
  Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe akionyesha fomu zilizojazwa na wanaCCM wa Mkoa wa Dar es Salaam zaidi ya 1,500 kwa ajili ya kumdhamini ili aweze kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), baada ya kukabidhiwa na Katibu wa CCM Wilaya ya Kinondoni, Athuman Shesha (kulia) katika Ukumbi wa Vijana Kinondoni Juni 25.2015. Kushoto ni mkewe Mama Dorcas Membe.    Picha zote na John Badi   Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe akizungumza na umati wa wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) waliofurika katika ukumbi wa Vijana Kinondoni mkoani Dar es Salaam Juni 25.2015, kwa ajili ya kumdhamini ili aweze kuwania urais katika uchaguzi mkuu ujao kwa tiketi ya chama hicho, ambapo wanaCCM zaidi ya 1,500 walimdhamini. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa na Mbunge wa Jimbo la Mtama, Bernard Membe akiagana na umati wa wanach