Posts

ADHA YA MVUA ILIVYOONEKANA MWANZA JANA JANUARI 14, 2016

Image
Barabara ya Nyerere Makutano ya Kenyatta Mwanza Sokoni Daraja la Mabatini Eneo la Mabatini Mwanza

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI, JANUARY 14

Image

AKAMATWA NA VIPANDE 8 VYA MENO YA TEMBO KATAVI

Image
Kamanda wa Polisi wa Mkoa Katavi Dhahiri Kidavashari akiwa ameshika meno ya Tembo aliyokamatwa nayo mtuhumiwa Nzuri Ndizu mkazi wa Kijiji cha Mbede Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi ambae alikamatwa juzi akiwa na vipande 8 yenye thamani ya milioni 120 . Mtuhumiwa Nzuri Ndizu Mkazi wa Kijiji cha Mbende Wilaya ya Mlele akiwa katika ofisi ya Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi baada ya kukamatwa na meno ya tembo vipande nane yenye thamani ya shilingi milioni 120 hapo juzi. Meno ya Tembo vipande nane (8) vyenye uzito wa kilo 50 ya thamani ya milioni 120 ambayo ni sawa na tembo hai wanne aliyokamatwa nayo hivi karibuni mtuhumiwa Nzuri Ndizu Mkazi wa Kijiji cha Mbede Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi. (Picha na Katavi yetu blog) Mtu mmoja aliyefahamika kwa jina la Nzuri Ndizu (44) Mkazi wa Kijiji cha Mbede Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi amekamatwa akiwa na meno ya tembo nane yenye uzito wa kilogramu 50 yakiwa na thamani ya shilingi milioni 120 ambapo ni sawa na tembo wanne waliuawa.

TTCL YAKOPA DOLA MILIONI 22 KUSAMBAZA MTANDAO 3G NA 4G LTE

Image
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Dk. Kamugisha Kazaura (kushoto) na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Uwekezaji (TIB), Jaffer Machano (kulia) wakisaini hati ya makubaliano ya mkopo katika hafla iliyofanyika jijini Dar es Salaam jana. TTCL na Benki ya TIB zimesaini makubaliano ya dhamana ya Benki na Mkopo wa Dola za Marekani milioni 22 ikiwa ni awamu ya kwanza ya mkopo wa Dola za Marekani milioni 329 zitakazotolewa kwa kampuni ya TTCL. Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Dk. Kamugisha Kazaura (kushoto) akibadilishana hati ya makubaliano ya mkopo na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Uwekezaji (TIB), Jaffer Machano mara baada ya kutiliana saini. TTCL na TIB zimesaini mkataba wa makubaliano ya dhamana ya Benki na Mkopo wa Dola za Marekani milioni 22 ikiwa ni awamu ya kwanza ya mkopo wa Dola za Marekani milioni 329 zitakazotolewa kwa kampuni ya TTCL. Ofisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL), Dk. Kamugisha Kaza

DAKTARI AMPIGA NGUMI MGONJWA NA KUMUUA

Image
Urusi Kanda ya video ya CCTV imetolewa ambapo daktari mmoja nchini Urusi alimpiga ngumi mgonjwa na kumuua. Kisa hicho kilitokea katika mji wa Belgorod kilomita 670 kusini mwa mji mkuu wa Moscow mnamo mwezi Disemba tarehe 29. Mgonjwa huyo alikuwa amempiga teke muuguzi mmoja kabla ya daktari huyo kumpiga ngumi ya kichwa kulingana na vyombo vya habari vya Urusi na kuzirai kabla ya kuaga dunia akiwa hospitalini. Wachunguzi wanadhani kwamba hakumuua kwa makusudi lakini wameanzisha kesi ya uhalifu. Habari hiyo ilisambaa baada ya kanda hiyo kutolewa

Serikali kugawanya kwa uwiano madaktari na mabingwa nchini

Image
Subi Nukta 1/12/2016 10:23:00 PM No Comment Mheshimiwa Ummy Mwalimu akizungumza na Mganga Mfawidhi wa hospitali ya Peramiho, Dk Venance Mushi, alipotembelea hospitali hiyo  SERIKALI imesema itapanga mgawanyo maalumu ili mikoa yote iweze kunufaika na huduma za Madaktari na Madaktari bingwa na kutatua kero za wananchi wanazopata za kufunga safari ndefu kuhangaikia huduma za wataalamu hao. Aidha itaendelea kushughulikia suala la kuboresha mazingira ya kazi kwa Madaktari na watumishi wa Sekta ya Afya kwa ujumla ikiwa ni pamoja na maslahi yao ili kuwafanya wahamasike kufanya kazi hapa nyumbani badala ya kwenda kufuata maslahi makubwa nje ya nchi. Kauli hiyo ya serikali imetolewa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, wazee na watoto Ummy Mwalimu wakati wa uzinduzi wa huduma za madaktari bingwa mkoani Ruvuma jana Alisema Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Daktari John Magufuli, imedhamiria kukabiliana na upungufu wa Madaktari kwa kuanzisha utaratibu maalumu