Posts

WATAKA UWANJA WA NDEGE MWANZA UJENGWE KISASA ILI KUINUA SEKTA YA UTALII

Image
Na Tiganya Vincent-MAELEZO_Dodoma Baadhi ya Wabunge wanaotoka Kanda ya Ziwa wameomba Wizara ya Ujenzi , Uchukuzi na Mawasiliano kujenga Uwanja wa Ndege wa Mwanza kwa kiwango cha Kimataifa ili kuimarisha sekta ya Utalii na usafiri wa anga katika kanda ya Ziwa. Walisema kuwa hatua itasaidia watalii wanaokuja nchini kushuka moja kwa moja mkoani Mwanza na kisha kuelekea katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti na maeneo mengine ya vivutio vya hapa nchini bila kupitia nchi jirani. Kauli hiyo imetolewa jana na Wabunge Dkt.Raphael Chegeni  na Mhe. Ezekeil Maige wakati wakichangia hotuba kuhusu utekelezaji wa bajeti ya Wizara ya Ujenzi ,Uchukuzi  na Mawasiliano kwa mwaka ujao wa fedha. Mhe. Dkt.Chegeni alisema kuwa Uwanja wa Ndege wa Mwanza ni muhimu ukajengwa kwa viwango vya Kimataifa ili uweze kuruhusu ndege mbalimbali kubwa na ndogo kuweza kutua bila tatizo. Alisema kuwa hatua hiyo itasaidia kuunganisha Mkoa wa Mwanza na nchi jirani za Rwanda, Uganda na Burundi na hivyo kuruhusu

MKWASA ATAJA KIKOSI CHA NYOTA 27

Image
Kocha Mkuu wa timu ya Soka ya Tanzania, Charles Boniface Mkwasa ameita kikosi cha wachezaji 27 watakaounda Taifa Stars ambacho kinajiandaa kucheza Misri Juni 4, 2016 katika mchezo wa kuwania kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON-2017). Mkwasa maarufu kama Master, alitangaza kikosi cha timu hiyo Jana Mei 18, 2016 mbele ya Kocha Msaidizi, Hemed Morocco na waandishi wa habari kwenye Ukumbi wa mikutano wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Ilala jijini Dar es Salaam. Kabla ya kuiva Misri, kikosi hicho kitafunga safari hadi Kenya kucheza na Harambee Stars katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa ambao wenyeji wameuombea Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) kwamba utambulike na kuingia kwenye rekodi za kimataifa ikiwa ni pamoja na kuingia kwenye mchakato wa kupima viwango vya soka. Katika kikosi hicho, Mkwasa amemuita beki Mlinzi mahiri wa Young Africans, Nadir Haroub maarufu kama Cannavaro huku akimwacha beki mwingine wa Young Africa

Serikali kudhibiti mitandao ya kijamii kwenye ofisi zake

Serikali imeanza mchakato wa kutekeleza mpango wa kudhibiti matumizi ya mitandao ya kijamii katika ofisi za umma ili kuongeza ufanisi. Mpango huo umelenga kuzuia mitandao ya kijamii ikiwamo Facebook, Twitter, Whatsapp na Instagram. Meneja wa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Wakala wa Serikali Mtandao (EGA), Suzan Mshakangoto alisema mpango huo umelenga kuwadhibiti watumishi wa umma wanaotumia mitandao hiyo kuanzia saa 1.30 asubuhi hadi saa 9.30 alasiri. Alisema sehemu kubwa ya wataalamu wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) wa taasisi za umma wameshapewa mafunzo mbalimbali kufanikisha mpango huo. Hatua hiyo imekuja baada ya aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi, Ombeni Sefue kuuagiza wakala huyo miezi mitano iliyopita kutafuta njia madhubuti ya kudhibiti matumizi ya mitandao ya kijamii ofisini ili kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi. “Mtumishi akishaingia ofisini hataweza kutumia mitandao ya kijamii na huduma za barua pepe nje ya mfumo wa Serikali kama Yahoo na Gmail

Magereza yasaini mkataba wa kuwafundisha wafungwa ujasiriamali

Image
JESHI LA MAGEREZA NCHINI LASAINI MKATABA WA UFUNDISHAJI ELIMU YA UJASILIAMALI KWA WAFUNGWA LEO 18.05.2016-DAR ES SALAAM Jeshi la Magereza limesaini Mkataba (MoU) na Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Technoserve – Tanzania kushirikiana katika ufundishaji wa wafungwa mafunzo ya Ujasiriamali wakiwa wanakaribia kumaliza vifungo vyao magerezani ili stadi hizo ziwasaidie kumudu maisha mapya baada ya kutumikia adhabu zao.  Programu hii itaendeshwa katika Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na Mfuko wa “Master Card” kwa vijana wa kike na kiume wenye umri kati ya miaka 18 hadi 30 hivyo wafungwa walioko katika Magereza yaliyomo Mkoani humo na wengine wenye sifa toka Kanda ya Nyanda za Juu Kusini ili kupata mafunzo kupitia progamu ya uimarishaji wa maendeleo ya vijana vijijini kupitia biashara “STRYDE” inayoendeshwa na Taasisi hiyo. Takwimu za sasa zinaonesha kwamba kati ya asilimia 30 na 35 ya wafungwa wanaomaliza vifungo vyao hurejea magerezani.Hivyo, mafunzo haya yatalenga kuwafanya wanapomaliza

Polisi yakamata wasichan 15 waliokuwa wapelekwe Oman

Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limewakamata wasichana 15 katika nyumba iliyopo maeneo ya Ukonga, waliokuwa tayari kusafirishwa kwenda Oman kufanya kazi za ndani.  Akizungumza na waandishi wa habari jana, Dar es Salaam, Kamishna wa Polisi wa kanda hiyo, Simon Sirro, alisema wasichana hao walikamatwa baada ya Polisi kupata taarifa toka kwa msiri kuwa kuna mtu amewaweka wasichana kwa ajili ya kuwasafirisha.  Sirro alisema Polisi walifuatilia na kufika katika eneo hilo na kufanikiwa kuwakuta katika nyumba ya Hadija Mohamed (40) wakiwa wamegawanywa katika vyumba viwili.  Alisema uchunguzi wa awali, umebaini kuwa mwanamke huyo anashirikiana na mwenzake Salma Habibu (43) mkazi wa Temeke kuwatafutia masoko nchini Oman na wao ni mawakala wanaoletewa kutoka mikoani na kuwapokea kwa ajili ya kuwasafirisha.  Aidha alisema watuhumiwa hao watapelekwa mahakamani ili sheria ichukue mkondo wake.  Pia ametoa onyo kwa watu wenye tabia hiyo kuacha, kwani wasichana hao wakifikishwa

MAGAZETI YA LEO MAY 19

Image

MAKONDA: WANAWAKE NDIYO CHANZO CHA UFISADI NCHINI

Image
RC Makonda akizungumza na wananchi wa Vingunguti. Wananchi wakimsikiliza RC Makonda. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akikagua machinjio ya Vingunguti baada ya kuzungumza na wananchi wa Kata ya Mnyamani Dar es Salaam jana asubuhi. Kushoto ni Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala, Omari Kumbilamoto. Wananchi wa Kata ya Mnyamani Vingunguti wakiwa kwenye mkutano huo wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (hayupo pichani) Makonda (kushoto), akisalimiana na wananchi na viongozi wakati akiwasili kwenye mkutano huo. Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala, Omari Kumbilamoto (wa pili kulia), akizungumza katika mkutano huo kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuzungumza na wananchi. Kutoka kulia ni Diwani wa Kata ya Mnyamani, Shukuru Dege, RC. Makonda na Meneja wa Benki ya Wananchi Dar es Salaam (DCB), Tawi la Ukonga, Das Ndazi. Meneja wa Benki ya Wananchi Dar es Salaam (DCB), Tawi la Ukonga, Das Ndazi (kushoto), akizun

BOMU FEKI LAAHIRISHA MECHI YA MAN UNITED

Image
Mashabiki waliokwenda kuangalia mechi wakishikwa na butwaa baada ya kuambiwa kuna bomu uwanjani Old Trafford. Polisi nchini Uingereza imethibitisha kuwa kitu kilichokuwa kinadhaniwa kuwa ni bomu kilichoonekana kwenye uwanja wa timu ya Manchester United wa Old Trafford hakikuwa bomu kama ilivyodhaniwa bali kilikuwa ni kifaa cha wanausalama cha mazoezi kwa ajili milipuko. Kifaa hicho kiliachwa na walinzi wa kampuni moja ya binafsi baada ya kufanya mazoezi yaliyowahusisha mbwa wenye kunusa vifaa na vitu vya kihalifu. Kutokana na kuonekana kwa kifaa hicho mechi kati ya Manchester United na Bournemouth iliahirishwa. Tayari kifaa hicho kimeshaharibiwa chini ya uangalizi mkali wa timu ya kuthibiti milipuko. Tayari maafisa wa mji wametaka uchunguzi ufanyike na kuita kitendo hicho kuwa ni cha kizembe na cha kudhalilisha. Maelfu ya mashabiki walioondolewa katika uwanja wa Old Trafford ambapo mechi baina ya wenyeji Machester United na Bournemouth iliahirishwa na itachezwa siku ya

Shukurani za Michuzi kwa kufanikisha mazishi ya Maggid

Image
Familia ya Ankal Muhidin Issa Michuzi inapenda kutoa shukrani nyingi sana sana kwa ndugu, jamaa, majirani, marafiki na wafanyakazi wenzie kwa kujitoa kwa hali na mali katika wakati huu mgumu wa msiba wa mawanae Maggid (pichani) aliyefariki huko Durban, Afrika Kusini Jumapili ya wiki iliyopita na kuzikwa katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es salaam juzi Jumamosi. Ni vigumu mno kumshukuru mtu mmoja mmoja kutokana na wingi wenu na kwa jinsi kila mmoja wenu alivyojitoa na kuonesha upendo wa dhati kabla na baada ya mazishi. Tunaweza kujaza kurasa 200 kama hizi na tusiwe tumehitimisha robo tu ya shukrani zetu kwa kila mmoja wenu. Hivyo tunaomba radhi kwa yoyote ambaye hatutomtaja, kwani wafadhili wetu nyie mko wengi mno. Pamoja na hayo shukrani za kipekee ziwaendee Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Mama Janeth Magufuli na familia yao yote, Rais Mstaafu wa awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete na Mama Salma Kikwete na familia yao yote, Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Alha

MAGAZETI YAJUMATATU MAY 16

Image