Magereza yasaini mkataba wa kuwafundisha wafungwa ujasiriamali


JESHI LA MAGEREZA NCHINI LASAINI MKATABA WA UFUNDISHAJI ELIMU YA UJASILIAMALI KWA WAFUNGWA LEO 18.05.2016-DAR ES SALAAM


Jeshi la Magereza limesaini Mkataba (MoU) na Taasisi isiyo ya Kiserikali ya Technoserve – Tanzania kushirikiana katika ufundishaji wa wafungwa mafunzo ya Ujasiriamali wakiwa wanakaribia kumaliza vifungo vyao magerezani ili stadi hizo ziwasaidie kumudu maisha mapya baada ya kutumikia adhabu zao. 

Programu hii itaendeshwa katika Mkoa wa Mbeya kwa kushirikiana na Mfuko wa “Master Card” kwa vijana wa kike na kiume wenye umri kati ya miaka 18 hadi 30 hivyo wafungwa walioko katika Magereza yaliyomo Mkoani humo na wengine wenye sifa toka Kanda ya Nyanda za Juu Kusini ili kupata mafunzo kupitia progamu ya uimarishaji wa maendeleo ya vijana vijijini kupitia biashara “STRYDE” inayoendeshwa na Taasisi hiyo.

Takwimu za sasa zinaonesha kwamba kati ya asilimia 30 na 35 ya wafungwa wanaomaliza vifungo vyao hurejea magerezani.Hivyo, mafunzo haya yatalenga kuwafanya wanapomaliza vifungo vyao waweze kupata maarifa ya kuanzisha shughuli zao wenyewe za kujipatia kipato halali na kuacha vitendo vya uhalifu katika jamii wanamoishi vinavyowafanya kurejea magerezani.

Aidha, mafunzo haya ya Ujasiriamali yatajikita katika kuwafundisha kilimo biashara, matumizi mazuri ya fedha binafsi, uwezo wa kutumia ujuzi, ubunifu na tafakari ya kina katika kufanya maamuzi, mpango biashara, mawazo ya biashara na uwezo wa kuandaa mpango biashara n.k.

Ushirikiano huu ni mkakati endelevu wa Jeshi la Magereza katika kuboresha Programu za Urekebishaji wa wafungwa magerezani ili wawe raia wema na wenye tija katika jamii na Taifa kwa ujumla. 

Program za Ujasiriamali kwa wafungwa zinaendeshwa pia katika baadhi ya Magereza kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kama vile Dorcas International na New Life in Christ katika Gereza la Karanga – ushonaji viatu, ufumaji na uokaji mikate, Gereza Arusha – uokaji mikate, ufundi seremala na ufumaji. 

Jeshi la Magereza linawakaribisha wadau wa ndani na nje kushirikiana katika urekebishaji wa tabia za wafungwa ili wawe na michango chanya katika jamii na Taifa kwa ujumla.

IMETOLEWA NA KITENGO CHA HABARI NA MAWASILIANO
MAKAO MAKUU YA JESHI LA MAGEREZA
DAR ES SALAAM




AddThis Sharing Buttons

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA