Posts

TUKUTANE CCM KIRUMBA LEO KUSHUHUDIA AND 1

Image
Mida ya jioni leo hapa katika kiwanja cha CCM Kirumba itapigwa bonge moja ya game kutoka kwa wanyamwezi wa And 1 pamoja na wana Mwanza,so Don't Miss Ground nzima. Goli.

ROMA MKATOLIKI KUYAWEKA MAISHA YAKE YA MZIKI KWENYE DOCUMENTARY YAKE MPYA.

Image
Msanii anayeiwakilisha TANGA katika bongo fleva ROMA, baada ya kuchukua tuzo mbili za Kilimanjaro kama Msanii bora wa Hip Hop na wimbo wake Mathematics kuchukua kama wimbo bora wa Hip Hip hivi sasa anatengeneza Documentary yake inayoeleza maisha yake kimuziki toka alivyoanza mziki shida alizopitia mpaka kufikia hivi sasa alipofikia.   Roma akiwa katika studio ya Tongwe Rec akiitengeneza DVD hiyo ambayo amesema nimapema sana kusema itatoka lini ila haitochelewa kutoka na anaamini watu wataipenda na italeta utofauti kidogo maana story iliyomo ndani ya Documentary hiyo iko kitofauti na itamgusa kila mmoja. source djchoka.blogspot.com

Grooveback JUMAMOSI HII @ Nyumbani Lounge

Image

Veejay Tash Na Meccacheka kukisanua Arusha Leo

Image
Veejay Tash Na Meccacheka kukisanua live pande za Empire Sports Bar ndani ya Shoprite Complex Arusha Kesho kwa hisani kubwa ya Sister Tumaini wa Empire pamoja na Brother Erick wa MJ,Entry ni bure so come one come all tufurahie muziki wetu wa Arusha bila kukosa show kali toa kwa breakdancers wa ukweli..

BEYONCE NDIYE MWANAMKE MZURI KUSHINDA WOTE DUNIANI!?

Image
Tunaweza kubishana mpaka asubuhi.Iweje,kwanini…mbona yule, hata mimi namjua nk.Lakini malumbano yetu yanaweza kuwa porojo tu kwani kwa mujibu wa Jarida maarufu la People la nchini Marekani, mwimbaji/mwanamuziki na mshindi wa tuzo kadhaa za Grammy,Beyonce Knowles(ukipenda Mrs.Jay-Z) ndiye Mwanamke Mzuri kushinda wote DUNIANI kwa mwaka 2012. Nimeweka neno duniani katika herufi kubwa kwa sababu binafsi huwa nina tatizo na wamarekani wanapoiona Marekani kuwa dunia. Ukiwaambia kwamba kuna mwanamke fulani mzuri sana yupo Tanzania au Kenya au Uganda watakushangaa.Hawaijui hivyo dunia unayoiongelea wewe. Beyonce ambaye ana umri wa miaka 30 sasa na Mama wa mtoto mmoja,Blue Ivy Carter, ameelezea kufurahishwa sana na heshima hiyo aliyopewa na Jarida la People. Wanawake wengine ambao wamewahi kushinda heshima hiyo ya People ni Michelle Pfeiffer, Julia Roberts, Nicole Kidman, Halle Berry, Jennifer Aniston, Angelina Jolie na Jennifer Lopez ambaye alishinda mwaka ja

SSPRA GENERAL ELECTION ON 28 APRIL 2012

Image

HARAIKI YA WANAFUNZI YAPAMBA SHEREHE ZA MUUNGANO WA TANZANIA

Image
Haraiki ya   wanafunzi wapatao   1,727 kutoka shule za msingi mbalimbali Tanzania bara na visiwani   wameipamba vizuri sherehe ya maadhimisho ya miaka 48 ya Muungano wa Tanzania yaliyofanyika   leo katika viwanja vya Uhuru jijini Dar es Salaam. Kati ya wanafunzi hao, ni wanafunzi 727 ambapo 500 wanatoka Tanzania bara, 200 Tanzania visiwani na 27 ni mahodari wa kucheza sarakasi ambao waliingia uwanjani na kutengeneza maumbo mbalimbali pamoja na kuimba wimbo maalumu uitwao Uamuzi wa Busara. Maumbo yaliyotengenezwa na haraiki hiyo ni pomoja na bendera ya taifa, herufi zenye   umbo la miaka 48 ya Muungano, na maumbo ambayo ndani yake walicheza salakasi na ngoma za asili za ndalandala kutoka Tanzania bara na chaso kutoka Zanzibar. Maumbo mengine ni pamoja na madini ya Tanzanaiti ambayo hayapatikani sehemu yoyote duniani zaidi ya Tanzania na maumbo ya mazao ya uchumi ya katani na pamba yanayolimwa Tanzania bara na karafuu Tanzania vis