MATOKEO KIDATO CHA PILI
Naibu waziri wa Elimu Philip Mulugo ametangaza matokeo ya kidato cha pili kupitia vyombo vya habari leo na yalikuwa kama ifuatavyo hapo chini: 1. Waliofanya mtihani 386,248 2. Waliofaulu 249,325 (65%) 3. Waliofeli 136,923 (35%) 1.0 UTANGULIZI Mtihani wa Taifa wa Elimu ya Sekondari Kidato cha Pili ulifanyika nchini kote kuanzia tarehe 05/11/2012 na kumalizika tarehe 16/11/2012. Mwaka 2012 kulikuwa na jumla ya vituo 4,304 vilivyosajili watahiniwa, ikiwa ni ongezeko la vituo 117(2.79 %) ikilinganishwa na ile ya mwaka 2011. 2.0 WATAHINIWA WALIOSAJILIWA, WALIOFANYA NA WASIOFANYA MTIHANI 2.1 Idadi ya watahiniwa waliosajiliwa kufanya mtihani walikuwa 430,327, kati yao wasichana walikuwa 205,476 na wavulana 224,851. Idadi hii ni upungufu wa watahiniwa 36,240 (7.76%) ikilinganishwa na mwaka 2011 ambapo walikuwa 466,567. 2.2 Watahiniwa 386,271 sawa na asilimia 89.76 ya waliosajiliwa, walifanya mtihani wakiwemo wasi