Posts

SAMAHANI KWA USUMBUFU UTAKAO JITOKEZA

Samahani sana wapenzi wa Blog hii,napenda kuwafahamisha kuwa hakutakuwa na taarifa nyingi za mara kwa mara  kama mlivyozoea kwani nitakuwa katika kipindi cha Mitihani ya kumaliza semister ya 1 ambayo itaanza Jumatatu tarehe 28/01/2013 mpaka tarehe 8/02/2013 hivyo nitakuwa busy na Mitihani hiyo.

CCM KIRUMBA HAPATOSHI LEO, NI YANGA DHIDI YA BLACK LEOPARDS YA AFRIKA KUSINI.

Image
Yanga Africans. Kocha Mkuu wa klabu ya Yanga, Ernest Brandts amesema timu yake itafanya vizuri katika mechi ya marudiano ya kirafiki dhidi ya Black Leopards ya Afrika Kusini niliyopangwa kufanyika mapema jioni ya leo ndani ya uwanja wa CCM-Kirumba mjini Mwanza. Brandts alisema wachezaji wake wote wamefikia kiwango kile anachotaka na mchezo huo utakuwa muhimu sana kwake kwani ni wa mwisho kabla ya kuingia katika kampeni za kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara. Alisema kuwa Black Leopards ni timu nzuri na walipata mazoezi mazuri katika mechi ya kwanza iliyofanyika kwenye uwanja waTaifa jijini na kushinda kwa mabao 3-2.

MAFUNZO YA KWANZA YA U-DJ KUFANYIKA NCHINI

Image
ICHT DJ ACADEMY, ACADEMY YA KWANZA KUFUNGULIWA JIJINI DAR     YA KUFUNDISHA KUDJ PROFESSINALLY, KOZI ZITAKAZOFUNDISHWA NI:-   INTRODUCTION TO THE DJ INDUSTRY AMBAPO NDANI YAKE KUNA PACKAGE YA KOZI SABA (7) . 1.Set up Machine 2.Mixer Operation 3.Pioneer Operation 4.Basic Mixing 5.Beat Count 6. Beat to Beat mixing 7.Acapella Mixing NA     ADVANCE INTRODUCTION     TO THE DJ INDUSTRY:   AMBAPO NDANI YAKE KUNA PACKAGE YA KOZI (5). 1. Sound and Level 2. Turntable Operation 3. Perfect mixing 4. Scratching 5. Creative mixing and Techniques WALIMU WATAKAO FUNDISHA NI DJ PQ, DJ ZERO NA DJ D OMMY. ACADEMY IKO NYUMA YA BEST BITE KARIBU NA NYUMBANI LOUNGE. MAFUNZO YANATEGEMEA KUANZA TAREHE 4 FEB 2013.             KWA MASILIANO ZAIDI JINSI YA KUPATA FOMU ZA KUJIUNGA PIGA                                         NAMBA:         0712 58 08 59                                                Email :   itchdjacademy@gmail.com source : http://gsengo.blogsp

TAZAMA PICHA BAADA YA UKUTA KUANGUKA KATIKA KITUO CHA MABASI CHA UBUNGO ASUBUHI NA KUSABABISHA HASARA NA UHARIBIFU MKUBWA

Image
 Baadhi ya magari yaliyoangukiwa na ukuta.  Magari mbalimbali yakiwa chini ya kifusi.  Gari aina ya Noah likiwa limegandamizwa na zege.  Hii ndiyo hali halisi ya tukio lilivyokuwa.  Gari aina ya Toyota likiwa limebonyezwa na zege.  Watu wakiangalia magari yao.  Kenyela akiongea jambo juu ya ajali hiyo.  likuwa ni hasara tupu. .UKUTA WA ENEO  LA NDANI YA KITUO CHA MABASI UBUNGO BUS TERMINAL UMEANGUKIA MAGARI ZAIDI YA 24 YALIYOKUWA YAMEPAKI ENEO AMBALO HUTUMIKA KUPAKI WAKIWA WANASINDIKIZA ABIRIA NA NDUGU ZAO,CHANZO CHA AJALI HIYO NI MKANDARASI WA ENEO HILO ALIKUWA ANABOMOA UKUTA HUO,NA PIA IMERIPOTIWA KUWA KUNA BAADHI YA MAJERUHI source  http:// thegeebtz.blogspot.com

DARASA FT WINNIE -NISHIKE MKONO (OFFICIAL VIDEO)

Image

DAKTARI WA MAGONJWA YA WANAWAKE NA WATOTO HOSPITALI YA MKOA WA MARA AFARIKI DUNIA

Image
MAREHEMU DOCTA JOSEPH NYAMAGWIRA Na Shomari Binda DAKTARI Msaidizi Mkuu Daraja la kwanza wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara,Joseph Nyamagirwa (59) amefariki Dunia juzi asubuhi katika Hospitali ya Rufaa ya Bugando Mkoa wa Mwanza kwa tatizo la uvimbe sehemu ya chini ya utumbo mpana. Daktari huyo ameacha pengo kubwa katika Hospitali ya Mkoa wa Mara kutokana na kuwa tegemeo kubwa hasa kwa kutibu watoto na wanawake pamoja na upasuaji ambapo kwa sasa hospitali hiyo inahitaji madaktari 12 na hivi sasa waliopo ni watatu tu.     Akitoa taarifa ya kifo hicho,Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mara, Iragi Ngerageza alisema kuwa Marehemu alikuwa na tatizo la tumbo ambalo alikuwa akilalamikia kuwa linauma ambapo Jan.8 Mwaka huu alifika Hospitalini hapa kwa matibabu ambayo iliwalazimu kumpeka katika hospitali ya Rufaa ya Bugando na siku hiyo hiyo akifanyiwa upasuaji wa kina.   Alisema kuwa pamoja na jitihada za madaktari bingwa kuokoa maisha yake lakini hali yake

MWANZA FASHION WEEKEND MODELS SEARCH

Image
Kwa  mara ya kwanza katika jiji la Mwanza unaletewa Mwanza Fashion Weekend itakayofanyika mwezi March tarehe 2.  Msako wa models wa kike na kiume watakaopita kwenye runway siku ya onesho utafanyika jumamosi hii tarehe 19-1-2012 katika hoteli ya Goldcrest Ghorofa ya nane kuanzia saa 4 asubuhi mpaka saa 8 mchana.  Njoo upate nafasi ya kuonesha kipaji chako na kuonesha mavazi ya wabunifu maarufu Afrika Mashariki kama vile Mustspha Hassanali, Martin Kadinda na wengine wengi.