Posts

TAARIFA YA MTATIRO KUHUSU KUKAMATWA KWA PROF: LIPUMBA

Image
Prof. Lipumba akiwa katika gari la Polisi (picha: Habari Mseto blog) PROFESA LIPUMBA AKAMATWA NA POLISI KWA NGUVU! Ndugu zangu, hivi punde nimeongea na Maharagande Mbarala na Bonifasia Mapunda na wamenijulisha kuwa, Profesa Lipumba na Manaibu Wakurugenzi wawili wa Chama Cha Wananchi CUF (Shaweji Mketo na Abdul Kambaya), pamoja na walinzi wa Profesa Lipumba, wamekamatwa na polisi. Pia, nimeongea na mhe. Joram Bashange, Mkurugenzi wa Fedha wa CUF, tayari yuko Central Police lakini hajaruhusiwa kuwaona viongozi. Mawakili wa CUF wanaelekea polisi pia. KUMBUKIZI YA MWAKA 2001 Ukamataji huo uliotumia nguvu kubwa umetokea leo majira ya Mchana wilayani Temeke. Leo ni Januari 27 na ni siku yenye kumbukumbu muhimu kwa Chama Cha Wananchi CUF baada ya matukio ya mauaji yaliyofanyika tarehe na mwezi kama huu huko Zanzibar ambako wafuasi wa CUF zaidi ya 100 waliuawa kwa risasi na vyombo vya dola. Mauaji hayo yalifuatiwa na maandamano mbalimbali yakiwemo ya Dar Es Salaam yaliyoongozwa na Pro

MAAFISA MAWASILIANO WATEMBELEA MRADI WA KUCHAKATA GESI WA TANZANIA MNAZI BAY AND SONGO SONGO GAS PROCESSING PLANT NA KUTOA MSAADA KATIKA HOSPITAL YA LIGULA

Image
Mkurugenzi wa Idara ya Habari –MAELEZO Assah Mwambene (kulia) akikabidhi kwa niaba ya Maafisia Mawasiliano Serikalini msaada wa Kitanda cha wagonjwa kwa Mganga Mkuu wa Hospitali ya Ligula Mkoani Mtwara Dkt. Mohamed Abraham Gwao walipotembelea Hospitalini hapo leo. Mkurugenzi wa Idara ya Habari –MAELEZO Assah Mwambene (kulia) akikabidhi kwa niaba ya Maafisia Mawasiliano Serikalini msaada wa Kitanda cha wagonjwa kwa Mganga Mkuu wa Hospitali ya Ligula Mkoani Mtwara Dkt. Mohamed Abraham Gwao walipotembelea Hospitalini hapo leo. Kushoto ni Mwenyekiti wa Chama cha Maafisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO) Bw. Innocent Mungy. Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bibi. Sihaba Nkinga akitembeea katika eneo la mradi wa nyumba za wafanyakazi wa Mradi wa kuchakata Gesi  Tanzania Mnazi Bay and Songo Songo Gas Processing Plant  wakati wa ziara ya Maafisa Mawasiliano Serikalini leo Mkoani Mtwara. Kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Habari – MAEEZO Bibi. Zamaradi Kaw

DHARUBA KUBWA YA THELUJI NA UPEPO MKALI IMEIPELEKEA KUSIMAMISHA HUDUMA ZA UMMA KASKAZINI MASHARIKI YA MAREKANI.

Image
  Zaidi ya watu 60 million wataathirika kutokana na kimbunga kikubwa cha upepo unaoambatana na unyeshaji wa theleji katika eneo la kaskazini mashariki ya Marekani. Lori maalumu la usafishaji likiondoa theluji iliondoka barabara ya South Church Street, katika mji wa Hazleton, Pennsylvania siku ya Jumatatu Jan 26, 2015. Photo via  . dailymail.co.uk Kwa mujibu wa kitengo cha hali ya hewa nchini Marekani, imetaja maeneo ambayo yataathiriwa na dhoruba hiyo, ya kihistoria ambayo itapelekea zaidi ya watu kadhaa kukosa huduma ya umeme, pamoja na huduma za usafiri wa anga na nchi kavu.   Imetaja baadhi ya majimbo ambayo yatakumbwa na kimbunga hicho kuwa ni New York, New Jersey, Massachusetts, Connecticut na Rhode Island, ambapo imepelekea viongozi wakuu wa majimbo hayo kutangaza hali ya hatari kwa tukio hilo ambalo litatokea siku ya Jumatatu, Jumanne na Jumatano.   Imetabiriwa kiasi cha unyeshaji wa theluji hiyo 36inches katika jimbo la New York 16 hadi 26 inches katika jim

FAHAMU UKWELI JUU YA TUKIO LILILOTOKEA LEADERS CLUB KATI YA ALI KIBA NA DIAMOND,UCHAWI WATAWALA, HIRIZI ZAOKOTWA

Image
HALI inazidi kuwa mbaya kwa mastaa wawili wa muziki wa Bongo Fleva wanaogombea unyota kimuziki, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Ali Saleh Kiba, safari hii yameibuka mapya kwa kila msanii kuogopa kumshika mkono mwenzake kutokana na imani za kishirikina. Mashabiki wa Mbongofleva Ali kiba waliionyesha kumkubali zaidi kuliko, 'Daimond Platnumz' katika viwanja vya Leaders Club. TUJIUNGE LEADERS Matukio hayo ya kusisimua yaliwatia hofu kubwa mashabiki na wadau wa muziki Bongo muda mfupi kabla ya nyota hao kukaribishwa stejini kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar, mwishoni mwa wiki iliyopita. HIRIZI ZAKUTWA UWANJANI Kwa mujibu wa wanahabari wetu, katika Viwanja vya Leaders, Kinondoni, kulikutwa hirizi zilizozagaa, zilizodaiwa kudondoshwa  na vijana waliokamatwa wakiwa wamevalia sare zenye majina ya mastaa hao wawili. Moja ya Hirizi iliyotupwa katika viwanja hivyo. Katika hali ya kushangaza, mmoja wa mashabiki waliohudhuria onyesho hilo ambaye aliz

AJALI YA MOTO KICHANGA CHAOKOA FAMILIA!

Image
Na Gabriel Ng’osha/Risasi Mchanganyiko KICHANGA  kinachokadiriwa kuwa na umri wa miezi nane, wiki iliyopita kiliiokoa familia yake kuteketea kwa moto, baada ya kuamka usiku na kulilia kunyonya, kitendo kilichomshtua mama yake aliyebaini nyumba yao ilikuwa ikiungua, huko Kibamba Lungwe jijini Dar es Salaam. Sehemu ya nyumba iliyoungua. Akisimulia tukio hilo, mama wa kichanga hicho, Asha Mohamed, alisema alishtuka baada ya mtoto kuanza kulia akitaka kunyonya, alipoamka ndipo akaona mwanga mkali juu ya paa, hali iliyomlazimu kuamka na kwenda kumgongea Abuu ili kutafuta njia ya kutoka,” alisema mama huyo akiongeza kuwa sebuleni, moto ulikuwa umetapakaa. Kijana Abuu Masoud (15), baada ya kuamshwa, alionyesha ujasiri na upendo mkubwa kwa kujitoa mhanga kuwasaidia wadogo zake watatu waliokuwa wamelala katika moja ya vyumba vya nyumba hiyo. Baada ya kuingia katika chumba hicho, alifanikiwa kumtoa mtoto mmoja. Watoto walionusulika kuteketea kwa moto. “Nilipofungua mlango wa sebuleni

WASTARA AKIRI KUSHUKA KISANAA BAADA YA KUFARIKI SAJUKI

Image
Stori: Mayasa Mariwata/Risasi Mchanganyiko  STAA  wa filamu nchini, Wastara Juma amesema anajihisi kupoteza mwelekeo unaomfanya kushuka kisanaa tokea kufariki kwa mumewe, Juma Kilowoko ‘Sajuki’ kwani ari yake ya kufanya kazi imepotea. Staa wa filamu nchini, Wastara Juma. Akipiga stori na paparazi wetu hivi karibuni, alisema Sajuki alikuwa ni msaada mkubwa sana kwake kisanaa mbali na maisha ya kawaida, kwani anashindwa kupita njia alizokuwa anapitishwa na mumewe huyo kiasi cha kujikuta akitoa filamu kati ya mbili hadi tatu kwa mwaka. “Nikiri tu kwamba nimeshuka kisanaa, kasi ya kipindi kile imepungua, mume wangu alikuwa akijituma kuhakikisha mikakati yetu inaenda, kwa mwaka mzima nilitoa filamu hata tatu lakini toka asa naambulia moja tu mwaka mzima,” alisema.