Posts

MAMBO 10 ALIYOZUNGUMZA LOWASSA NA WAANDISHI WA HABARI KWA MARA YA KWANZA

Image
Mhe. Edward Lowassa amefanya mkutano maalum leo nyumbani kwake mjini Dodoma ambapo ananukuliwa kusema yafuatayo kwa muhtasari: 1. Hahusiki lolote na sakata la Richmond na ndio sababu hata kamati ya Mwakyembe haikuona sababu ya kumhoji. Amesisitiza kuwa cheo cha uwaziri mkuu ndio ilikuwa lengo la kamati ya mwakyembe na spika wa bunge kipindi hicho Samwel Sitta. Amesisitiza hicho sio kikwazo kwake katika kuingia Ikulu kwani sakata la Richmond lilipikwa kumchafua. Amechukua muda mrefu kuzungumzia hili la Richmond na amesema atalisema zaidi Arusha wikendi hii. 2. Anaamini kila mtangaza nia ana makundi ya kumuunga mkono. Yeye katika mkutano huu na wahariri leo ameambatana na Nazir Karamagi, Peter serukamba, Diana chilolo, Hussein Bashe na wengineo huku wengi wakiwa ni waliojeruhiwa katika serikali ya awamu ya nne akiwemo Aliekuwa DC Igunga Elibariki Kingu. Pia aliyekuwa mkurugenzi wa HakiElimu Elizabeti Misoki naye alikuwepo. Amehoji kwani akina Karamagi wana tatizo gani na kwan

MAGAZETI YA LEO JUMANNE, MEI 26

Image

MWIGULU NCHEMBA AJIUZULU WADHIFA WAKE WA UNAIBU KATIBU MKUU WA CCM TANZANIA BARA

Image
M wigulu Nchemba amejiuzulu nafasi yake ya Naibu Katibu Mkuu CCM ili kupisha agombee Urais na akishindwa atarudia nafasi ikimpendeza M/kit. Nafasi ya Naibu Katibu Mkuu CCM iliyokuwa imashikiliwa na Mwigulu Nchemba imechukuliwa na ndugu Rajab Luwavi.

MAGAZETI YA LEO JUMATATU, MEI 25

Image

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI

Image

UNESCO WATOA MAFUNZO YA TEHAMA KWA WALIMU WA VYUO VYA UALIMU HAPA NCHINI

Image
  Washiriki wa mafunzo wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kumaliza mafunzo ya matumizi ya Tehama katika ufundishaji kwenye vyuo vya ualimu. Na Geofrey Adroph, Pamoja blog   Shirika la Umoja wa Mataifa Elimu ya Sayansi na Utamaduni (UNESCO) limejikita katika uboreshaji wa elimu kwa kuwapa mafunzo walimu katika somo la Teknnolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama).   Akizungumza leo katika Ufungaji wa Mafunzo yaliyoandaliwa na UNESCO wakishirikiana na China Funds in Trust Project (CFIT) yaliyofanyika kwa siku tano katika Ukumbi wa DIT, Jijini Dar es Salaam,  Ofisa Miradi wa UNESCO, Faith Shayo amesema mafunzo waliopata walimu wa vyuo vya walimu mbalimbali nchini itawasaidia katika uboresha wa elimu ikiwa ni pamoja na kuwapa vifaa vitakavyotumika katika kufundishia somo hilo.   Faith amesema ufundishaji na uelimishaji namna ya matumizi ya Tehama hii   inatokana na baada ya mkutano wa viongozi wa vyuo mbalimbali pamoja na wadau wa elimu wa hapa nchini kuona kuna mapungufu