Posts

WALIOMUUA ALBINO MWAKAJILA WA MBEYA WAHUKUMIWA KUNYONGWA HADI KUFA

Image
Hakimu Mwakalinga siku alipohukumiwa kunyongwa hadi kufa kwa mauaji ya Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Rungwe. Leo amehukumiwa tena kunyongwa mpaka kufa katika mauaji ya mlemavu wa ngozi Henry Mwakajila. MAHAKAMA Kuu Kanda ya Mbeya leo hii imewahukumu kunyongwa mpaka kufa watu wanne kati ya watano waliomuua Henry Mwakajila (17) ambaye ni mlemavu wa ngozi (albino). Waliohukumiwa kunyongwa mpaka kufa ni Asangalwisye Kayuni maarufu kama Katiti au Mwakatoga na Gerard Korosso Kalonge (wakazi wa Kijiji cha Mbembati wilayani Ileje), na Leonard Msalage Mwakisole na Hakimu Mselem Mwakalinga (wakazi wa Kiwira wilayani Rungwe). Mshtakiwa wa nne, Mawazo Philemon Figomole, ameachiliwa huru na mahakama hiyo baada ya ushahidi wa upande wa mashtaka kushindwa kuthibitisha pasi na shaka kwamba alihusika katika mauaji hayo. Akisoma hukumu ya kesi hiyo ya mauaji yenye kumbukumbu Namb. KIW/IR/49/2008 na PI 5/2013, Jaji wa Mahakama Kuu Dk. Revila, amesema mahakama imejiridhisha pasi

Orodha ya majina ya waliochaguliwa kujiugna Kidato cha Tano

Kuna faili limepachikwa hapo chini au Fungua linki ifuatayo kutafuta majibu hayo:  pmoralg.go.tz/selection   au Fungua linki ifuatayo yenye faili (pdf) lenye orodha hiyo:  pmoralg.go.tz....pdf TAARIFA KWA UMMA  OWM-TAMISEMI inawatangazia majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi kwa mwaka 2015. Wanafunzi waliochaguliwa ni kutoka shule za Serikali na zisizo za Serikali. Jumla ya wanafunzi 55,003 wakiwemo wasichana 23,303 na wavulana 31,700 wamechaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo vya Ufundi. Kati ya wanafunzi waliochaguliwa 29,744 wakiwemo wasichana 11,450 na wavulana 18,294 sawa na asilimia 54.08 watajiunga na masomo ya Sayansi na Hisabati; na wanafunzi 25,259 wakiwemo wasichana 11,853 na wavulana 13,406 sawa na asilimia 45.92 wamechaguliwa kusoma masomo ya Sanaa na Biashara. Wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano mwaka 2015 wataanza muhula wa kwanza tarehe 18 Julai, 2015 na hakutakuwa na fursa ya mabadiliko yo

37 WAUAWA KWA AJALI YA NDEGE INDONESIA

Image
Umati wa watu ukishuhudia ajali hiyo. Vikosi vya usalama vikiwa kazini. Sehemu ya mabaki ya ndege hiyo. Shughuli za uokoaji zikiendelea katika eneo la tukio. JAKARTA, Indonesia NDEGE ya Uchukuzi ya Jeshi la Anga la nchini Indonesia imeanguka eneo la Medan, Kaskazini mwa Jimbo la Sumatra mapema leo. Maofisa wa jeshi la nchi hiyo wamesema kuwa, tayari miili 20 ya watu waliokufa kwa ajali hiyo imepatikana katika eneo la ajali. Maofisa hao wameongeza kuwa, ndege hiyo ya uchukuzi ya majeshi ya taifa hilo, ilianguka muda mfupi baada ya kupaa angani. Ndege hiyo ya kubeba mizigo aina ya C-130 Hercules ilikuwa na wahudumu 12 na abiria 50 wakati ilipoanguka. Kuna ripoti kuwa watu bado wanasikika wakipiga mayowe katika majengo yaliyoanguka. Ndege hiyo iliharibu nyumba baada ya kuanguka katika mji wa Medan, kaskazini mwa Jimbo la Sumatra. Picha za runinga zilizorekodiwa wakati ndege hiyo ilipokuwa ikianguka na zile za kwenye mitandao ya kijamii zinaonesha moto unatoka kwenye mabaki ya

ALIKIBA - CHEKECHA CHEKETUA (OFFICIAL VIDEO)

Image
‘Chekecha Cheketua’ is Alikiba's 2nd official smash hit release through his worldwide exclusive partnership with his record label and management company 'ROCKSTAR4000' and publishing partnership with 'Rockstar Publishing'. The Music Video was released as a Worldwide 1st Exclusive with TRACE TV, TRACE URBAN and TRACE NIGERIA - @TraceNigeria @Trace_Inter #TraceTV #TraceUrban #TraceNigeria This ‘Chekecha Cheketua’ music video was Directed by Meji Alabi (@mejialabi) and JM Films (@JM_FilmsTV)

WASHINDI WA TUZO ZA TANAPA 2014 WAKABIDHIWA TUZO JIJINI MWANZA

Image
  Meneja Mawasiliano wa Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) ,Pascal Shelutete akitoa neno la ukaribisho katika hafla ya utoaji tuzo kwa wanahabari waliofanya vizuri katika uandishi wa masuala ya Uhifadhi.Hafla iliyofanyika katika Hotel ya Gorden Crest jijini Mwanza.   Baadhi ya wageni waalikwa katia hafla hiyo. Mkurugenzi wa Hifadhi za Taifa ,Tanzania (TANAPA) Allan Kijazi akizungumza katika hafla hiyo juu ya lengo la kuanzishwa kwa tuzo hizo kwa wanahabari nchini. Mkuwa wa Wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza,Baraka Konisaga akizungumza kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Mwanza wakati wa hafla ya utoaji tuzo kwa Wanahabari waliofanya vizuri katika uandishi wa masuala ya Uhifadhi. Mgeni rasmi katika hafla hiyo,Waziri wa Maliasili na Utalii,Lazaro Nyalandu akizungumza wakai wa hafla ya kukabidhi tuzo kwa washindi wa Tuzo zitolewazo na TANAPA kwa wanahabari. Mkuu wa Majaji walioshiriki kupatikana kwa washindi wa tuzo zitolewazo na TANAPA kwa wanahabari,Dkt Ayoub Ryoba a