Posts

LOWASSA AENDELEA NA ZIARA ZAKE ZA KAMPENI, BARIADI MKOANI SIMIYU

Image
Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akiwapungia mkono wananchi wa Mji wa Bariadi (hawapo pichani) wakati alipowasili kwenye Uwanja wa Mpira wa Halmashauri Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu, kulikofanyika Mkutano wa Kampeni zake, anazoendelea kuzifanya katika Majimbo mbali mbali ya Uchaguzi hapa nchini. Katika ziara hiyo, Mh. Lowassa aliambatana na Waziri Mkuu wa Zamani, Mh. Fredrick Sumaye pamoja na Mwanasheria wa CHADEMA, Mh. Tundu Lissu. Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akisalimiana na baadhi ya viongozi wa Vyama vinavyounda UKAWA wa Mkoa wa Simiyu, wakati alipowasili kwenye Uwanja wa Mpira wa Halmashauri Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu, kulikofanyika Mkutano wa Kampeni zake, anazoendelea kuzifanya katika Majimbo mbali mbali ya Uchaguzi hapa nchini. Waziri Mkuu wa Zamani, Mh. Fredrick Sumaye, akihutubia

MAGAZETI YA LEO IJUMAA, SEPTEMBER 18

Image
 

Mitambo ya Kuzalisha Umeme wa gesi Yawashwa

Image
Mitambo ya Tanesco Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) limesema kazi ya kuunganisha mabomba ya gesi kutoka Kinyelezi I kwenda katika mitambo ya Ubungo I na II, jijini Dar es Salaam imekamilika. Aidha, kazi ya kuwasha mashine 10 za mtambo wa Ubungo I imekamilika na  inategemewa tatizo la kukatika umeme litafikia tamati kuanzia jana. Akizungumza na mtandao huu jijini Dar es Salaam jana, Ofisa Uhusiano wa Tanesco, Adrian Severin, alisema kazi ya kuwasha mitambo hiyo inahitaji umakini mkubwa  kutokana na mfumo unaotumika kuwa mpya. Alisema kazi ya kuunganisha mabomba ya gesi imekamilika na tatizo lililokuwapo la kukatika umeme lilitokana na matengenezo ya mfumo mpya yaliyokuwa yakiendelea kwa ajili ya kuwashwa kwa mitambo hiyo mipya. Aliwataka wananchi wawe na subira wakati kazi hiyo ikiendelea na hadi kufikia leo itakuwa imekamilika na umeme utapatikana kwa uhakika baada ya kuanza kuzalishwa kwa kutumia gesi kutoka Mtwara.  “Kuanzia jana umeme umeanza

BOKO HARAM WAMEUA WATU 380 CAMEROON

Image
  Shirika la kutetea haki za kibinadamu la Amnesty International limesema raia 380 wameuawa na wapiganaji wa Boko Haram kaskazini mwa Cameroon mwaka huu. Ripoti iliyotolewa leo na shirika hilo inasema kuna wanajeshi kadha waliouawa na wapiganaji hao ambao wamelazimisha watu 80,000 kutoroka makwao. Wanajeshi na polisi wa Cameroon nao wanadaiwa kujibu mashambulio ya kundi hilo kwa kuwakamata watu zaidi ya 1,000, wengi wao vijana. Ripoti hiyo kwa jina "Cameroon human rights under fire", inasema baadhi ya waliokamatwa na maafisa wa usalama wameuawa au kufariki kutokana na hali mbaya gerezani, hasa katika mji wa Maroua. Shirika hilo linasema watu 200 waliokamatwa na maafisa wa usalama kwenye operesheni Desemba kwa sasa hawajulikani waliko. Amnesty wanaamini Cameroon inaweza kujifunza mengi kutokana na makosa yaliyofanywa na taifa jirani la Nigeria ambako wanajeshi wametuhumiwa kutekeleza dhuluma dhidi ya raia kwa muda mrefu. Kundi

YALIYOTAWALA KATIKA MAGAZETI YA LEO TZ,SEPT 17

Image
       

JUMBA REFU ZAIDI AFRIKA MASHARIKI LAFUNGULIWA NCHINI

Image
  Jengo refu zaidi lililokamilika Afrika Mashariki na Kati lazinduliwa nchini PSPF Towers ni moja ya majengo machache marefu barani Afrika na ndiyo jengo refu zaidi lililokamilika Afrika Mashariki na Kati, likiwa na urefu wa mita 147. Majengo mengine marefu Afrika ni Carlton Centre (mita 223) lililopo Afrika Kusini, Hassan II Mosque (mita 210) lililopo Moroko, Ponte City (mita 173) lililopo Afrika Kusini, Necon House (Mita 160) lililopo Nigeria, Marble Tower (mita 152), Pear dawn (mita 152), Pear dawn (mita 152), Met Life Centre (mita 150) na 88 on field (mita 147) yote ya Afrika ya kusini. Jengo hilo lililozinduliwa na Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete, ujenzi wake ulitumia miaka minne tangu mwaka 2011 hadi 2015 limegharimu shilingi bilioni 139.20 za Tanzania lina maeneo ya ofisi na nyumba za makazi 88. Pia katika jengo hili kuna sehemu ya mgahawa, mabenki, bwawa la kuogelea, Sehemu za kufanyia mazoezi, maegesho ya magari na sehemu nyi

MAGAZETI YA JUMATANO, SEPTEMBER 16 YAPO HAPA

Image
on 6:11 AM in KITAIFA | Comments : 0

Hawaruhusiwi kutumia rasilimali za umma kwenye kampeni za kisiasa isipokuwa...

Katika ukurasa wa mbele na wa tano wa Gazeti la Nipashe, toleo 0578604 la tarehe 12 Septemba, 2015 kumechapishwa taarifa kwamba “Sefue; Marufuku kutumia magari ya serikali kwenye kampeni” Katika taarifa hiyo, imeelezwa kwamba Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue alisema “Ni kosa kwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya kutumia rasilimali za serikali yakiwemo magari katika mikutano ya kampeni ya Chama cha Mapinduzi (CCM).” Alichosema Katibu Mkuu Kiongozi ni kwamba Watumishi wa Umma wakiwemo Wakuu wa Mikoa na Wilaya hawaruhusiwi kutumia rasilimali za umma yakiwemo magari kwenye kampeni za kisiasa isipokuwa wanapokuwa katika utekelezaji wa majukumu yao kiserikali. Aidha, watumishi wa Umma wanaotaka kushiriki katika katika kampeni za kisiasa ama kugombea nafasi yoyote ya kisiasa sharti wajiudhulu nyazifa zao za utumishi wa umma. Kupitia taarifa h