Posts

RIPOTI: USHINDI WA TRUMP NI HATARI KWA DUNIA

Image
Trump anaongoza miongoni mwa wagombea wa Republican Shirika moja la kimataifa limesema ushindi wa Donald Trump unachukuliwa kuwa miongoni mwa hatari 10 kuu zaidi zinazokabili dunia. Shirika hilo la Economist Intelligence Unit linaonya kuwa iwapo Bw Trump atashinda urais Marekani, hilo huenda likavuruga uchumi wa dunia na kuongeza hatari za kisiasa na kiusalama dhidi ya Marekani. Hata hivyo, shirika hilo halimtarajii Bw Trump, anayeongoza kwenye kinyang’anyiro cha kumchagua atakayepeperusha bendera ya chama cha Republican, kumshinda Bi Hillary Clinton ambaye shirika hilo linasema "ana uwezekano mkubwa sana kuwa mgombea wa chama cha Democratic". Ushindi wa Trump unaorodheshwa kuwa hatari zaidi kwa dunia kushinda hata Uingereza kuondoka kutoka kwa Umoja wa Ulaya au hata makabiliano ya kivita katika bahari ya South China Sea. Kuyumba kwa uchumi wa Uchina au Urusi kuingilia kivita Ukraine na Syria na kusababisha “vita baridi” vipya ni miongoni mwa mambo ambayo yanac

Asimamishwa kazi kwa kumwongopea Waziri Mkuu

Asimamishwa kazi kwa kumwongopea Waziri Mkuu Info P Ni Mhandisi wa Maji wa Wilaya ya Chato Pampu yadaiwa kupelekwa Morogoro, yeye asema iko kijijini WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemsimamisha kazi Mhandisi wa Maji wa Wilaya ya Chato, Bw. Peter Ngunura kwa kosa la kumdanganya mbele za watu na kumpa taarifa za uongo juu ya pampu ya maji iliyodaiwa kupelekwa Morogoro. Waziri Mkuu alitoa agizo hilo jana jioni (Jumatano, Machi 16, 2016) alipokuwa akiwahutubia mamia ya wakazi wa mji wa Chato waliojitokeza kumsikiliza kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa michezo wilayani Chato, mkoani Geita. Waziri Mkuu ambaye amewasili mkoani Geita kwa ziara ya siku mbili akitokea mkoani Kagera, alisimamishwa na wakazi wa kijiji cha Kalebezo, kata ya Nyamirembe, wilayani Chato na kukuta mabango yaliyokuwa yakidai maji safi na kuelezea uharibifu wa pampu ya maji. Katika maelezo yao, wakazi hao walimweleza Waziri Mkuu kwamba mradi wa maji kwenye kata hiyo ulishakamilika lakini pa

Monduli yamzuia mwekezaji kuendelea kujenga hotali mlimani

Info Pos Hatimaye Halmashauri ya Wilaya ya Monduli mkoani Arusha imesitisha ujenzi wa hoteli ya kitalii ya mwekezaji raia wa Uholanzi, Menno Hofland juu ya Mlima Losimingori. Akihutubia wakazi wa Kijiji cha Losirwa juzi, Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Ephraem Ole Nguyaine alisema hatua hiyo inafuatia malalamiko ya wakazi hao yaliyoripotiwa na gazeti hili hivi karibuni kupinga umiliki wa ardhi kwa mwekezaji huyo. Wakazi hao wamekuwa wakimlalamikia mwekezaji huyo kuhodhi ardhi ya kijiji zaidi ya ekari 120 kinyume cha taratibu na kwamba, amekuwa akiwafukuza kwa silaha wanapopeleka mifugo eneo hilo kwa ajili ya malisho. Hata hivyo, Hofland alieleza kuwa eneo hilo ameuziwa na mfugaji, Kimeshwa Kipailel kwa kufuata taratibu zote za kijiji na kwamba awali aliuziwa ekari 50 na baadaye kuongeza 70 juu ya mlima. Kipailel alisema hajauza eneo hilo bali amempatia hekari 50 mwekezaji huyo kujenga hoteli kwani makubaliano ni kuwa watakuwa wakigawana faida. “Mimempa ni eneo langu ajenge ho

MAGAZETI YA LEO TZ,MARCH 16

Image

RAIS MAGUFULI AWAAPISHA WAKUU WA MIKOA

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr.John .P. Magufuli anawaapisha wakuu wa mikoa wateuliwa kabla ya kuanza rasmi shughuli zao za kiutendaji. Rais Magufuli ameongelea suala la wafanyakazi hewa kwenye Halmashauri zote nchini, amewapa siku 15 wakuu wapya wa mikoa kuhakikisha hakuna wafanyakazi hewa katika Halmashauri zote nchini. Rais Magufuli wafanyakazi hewa, vijana wafanye kazi watakao kataa wapelekwe kwenye makambi wakafanye kazi, awaagiza wakuu wa mikoa ndani ya siku 15 kuhakikisha hamna wafanyakazi hewa katika mikoa yao Rais Magufuli amewataka wa kuu wa mikoa hao kuhakikisha hakuna vijana ambao watakuwa wanakwenda kucheza pool table asubuhi na badala yake vijana hao wanatakiwa kufanya kazi kweli kweli hata kwa kulazimishwa. "Nimeamua kuwateua wakuu wa Mikoa nikiamini kwamba mtaniwakilisha vizuri katika mikoa yenu, Napenda niwape pole kwa sababu mtakwenda kufanya kazi kweli kweli kutatua kero za wananchi wetu. Lakini pia niwaombe wakuu wa mikoa mkasimamie watu wafanye kaz

Katibu Mtendaji NACTE ajiuzulu

Image
Info P Aliyekuwa Katibu Mtendaji wa NACTE, Primus D Nkwera (kulia) akifafanua jambo Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Elimu ya Vyuo vya Ufundi (NACTE), Dk. Primus Nkwera amejiuzulu nafasi yake. Uamuzi wa kujiuzulu kwa Dk. Nkwera ulitangazwa katika ofisi kuu za Baraza hilo zilizopo Mikocheni Dar es Salaam juzi na Mwenyekiti wa Bodi,Mhandisi Steven Mlote na kusababisha baadhi ya wafanyakazi kuangua kilio. Akizungumza katika kikao cha dharura cha wafanyakazi wote wa baraza hilo, Mlote alisema Dk. Nkwera amejiuzulu ili kulinda hadhi ya Nacte kutokana na habari iliyoandikwa na Gazeti la Dira ikimtuhumu mambo mbalimbali. Gazeti hilo la Dira la Jumatatu tarehe 07/03/2016 toleo no.405 lilimtuhumu Katibu Mtendaji wa NACTE, Dk. Primus Nkwera kughushi vyeti vya shahada ya uzamivu baada ya kusomeshwa na serikali Afrika Kusini na kufeli. Mlote alisema kwa mujibu wa Dk. Nkwera, nafasi hiyo haipaswi kushikwa na mtu mwenye tuhuma ya aina yoyote, na ametafakari na kuona ajiweke kando na u

Waajiri na wadaiwa wa mikopo ya elimu ya juu wapewa siku 60

Info Post ent Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) inatoa siku 60 kuanzia tarehe 14 Machi, 2016 kwa wanufaika wote wa mikopo wanaodaiwa na HESLB kujitokeza na kuanza kulipa madeni yao kabla ya kuchukuliwa hatua za kisheria. Aidha, katika muda huu wa siku 60 waajiri pia wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanatekeleza wajibu wao wa kisheria wa kuwasilisha taarifa za waajiriwa wao waliohitimu katika vyuo vya elimu ya juu ndani na nje ya nchi. Taarifa zinazopaswa kuwasilishwa zijumuishe majina kamili ya waajiriwa, vyuo na mwaka waliohitimu. Itakumbukwa kuwa Sheria iliyoanzisha HESLB (Sura 178) (kama ilivyorekebishwa) inatoa wajibu kwa mnufaika wa mikopo ya elimu ya juu na pia wajibu kwa mwajiri. Wajibu wa Mwajiri Hivyo basi, taarifa hii inalenga kuwakumbusha waajiri ambao bado hawatimizi wajibu wao kisheria (kifungu cha 20) wa kuwasilisha majina ya waajiriwa wao wote ambao ni wahitimu wa vyuo vikuu kwa HESLB ndani ya siku 28 tangu waajiriwe. Adhabu ya kutotekeleza

BREAKING NEWS: RAIS MAGUFULI AFANYA UTEUZI WA WAKUU WA MIKOA 26

Image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa wakuu wa Mikoa 26 ya Tanzania Bara, ambapo kati yao 13 ni wapya, 7 wamebakizwa katika vituo vyao vya kazi, 5 wamehamishwa vituo vya kazi na 1 amepangiwa Mkoa Mpya wa Songwe. Uteuzi huo umetangazwa na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi, Mhandisi Mussa Ibrahim Iyombe leo tarehe 13 Machi, 2016 Ikulu Jijini Dar es salaam. Wakuu wa Mikoa walioteuliwa ni kama ifuatavyo; 1. Mh. Paul Makonda - Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam. 2. Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Elias Kyunga - Mkuu wa Mkoa wa Geita. 3. Meja Jenerali Mstaafu Salum Mustafa Kijuu - Mkuu wa Mkoa wa Kagera. 4. Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga - Mkuu wa Mkoa wa Katavi. 5. Brigedia Jeneral Mstaafu Emmanuel Maganga - Mkuu wa Mkoa wa Kigoma. 6. Mh. Godfrey Zambi - Mkuu wa Mkoa wa Lindi. 7. Dkt. Steven Kebwe - Mkuu wa Mkoa wa Morogoro. 8. Kamishna Mstaafu wa Polisi Zerote Steven - Mkuu wa Mkoa

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI, MACHI 13

Image

SERIKALI YA TANZANIA NA NORWAY ZASAINI MAKUBALIANO KUWEZESHA WAHANDISI WANAWAKE WANAOHITIMU VYUO VIKUU

Image
Msajili wa Wahandisi (ERB) Eng. Steven Mlote akielezea mafanikio yaliyopatikana tangu kuanza kwa Ushirikiano katika masuala ya Uhandisi kati ya ERB na Serikali ya Norway. Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani akijadiliana jambo na Balozi wa Norway nchini Tanzania, Hanne –Marie Kaarstad wakati wa kusaini Makubaliano ya Awali ya Programu ya kuwasaidia na kuwaendeleza Wahandisi wanawake walioko vyuoni yenye lengo la kuongeza idadi ya Wahandisi waliosajiliwa kwa ngazi ya Ushauri jana jijini Dar es salaam. Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Eng. Edwin Ngonyani akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway, Tone Skogen (Katikati) kuhusu Mafanikio wanayoyapata Wahandisi Wanawake wa Tanzania kutokana na msaada wa Mafunzo ya kuwasaidia na kuwaendeleza Wahandisi wanawake walioko vyuoni kutoka Serikali ya Norway Mwenyekiti wa Bodi ya Wahandisi nchini Prof. Ninatubu Lema (kulia) na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Norway, To

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI

Image