PATA LYRICS ZA ONE THE INCREDIBLE UPATE DARASA BUREEEEEEEEE

Pure mathematics lyrics

Yap, yeayah
Ah, M-Lab (M-Lab is in the house)
Moko, don’t touch it
Yeah,
Ahsante, Ah

Beat kali haifai bila vocal
Daily nakula dry, niko high kama popo
Fanya worldwide sio ku try kama local
Fake MC ukijikoki mi na squeeze kama fofo
Ah,
Verse baridi vaa koti
Salamu kwa wanangu wote sina ripoti
Bado mishemishe sapoti mwanangu opi
Kila biti natoboa kama juisi ya kijoti
Ni discipliner nawasimamisha wima
Minya rapper [Mi nyarapa] mpaka sura kama simu ya kichina
Mistari na vina, kwenye shari habari sina
Mchagga halali, macho kwenye salari daima
Zunguka kote hauna rafiki kama noti
Sista duu hauna mnafiki kama shosti
Tafuta deal uza hata pipi we bitoz
Tafuta njia haya maisha hayamuliki kama tochi

Chorus

Chap chap chap chap ni sawa
M-Lab, pure math, rap ni dawa
Chap chap chap chap ni sawa
Pure mathematics (dogo kapagawa)
x2

We unachana mi nachana mpaka basi
Niko booth nina bic, karama na karatasi
Sina hofu, nina speak salama kwa sala safi
Ila ukinivaa vibaya nakuchana kama vazi
Sanaa, gharama haramu chati
Harakati hii kubwa hupaswi simama kati
Verse inacheza Judo, kata na sarakasi
Baba mama mbarikiwe kusimama kaa wazazi
Pure namba, hapa zinajamba za kubuni
Mshamba kawa mjanja, mjanja ana ujanja wa kihuni
Banja kwenye beat weka ladha ya sabuni
We ni base ten log mi ni namba ya kirumi
Hii ni classic, hata isipotamba kama Dumi
Kasi ya ma-rapper ina sanda kama uchumi
Nina punchline na kick kama chuo kikuu cha ngumi
Pure mathematics, sina banda n’na kampuni
So

Chorus

Chap chap chap chap ni sawa
M-Lab, pure math, rap ni dawa
Chap chap chap chap ni sawa
Pure mathematics (dogo kapagawa)
x2

Kuna rapper mwenye akili na rapper batili
Rapper anayepata akisaka na asiyepata akisaka dili
Tofauti kati ya rapper wa kwanza na rapper wa pili
Wa pili anataka u-master huku hajapata umahiri
Fungua ukurasa kwenye darasa la hip-hop
Somo halisi tunaoandika kusikika anataka pomo
Midomo inasikika ikisema na mikono
Inashika makoleo na kuzika waliomo
Waliopotea njia wanataka kurudi nyuma
Wapotovu wamechuna, waovu wamenuna
Inawauma,
Wamepoteza mwelekeo,
Maendeleo yamegota watafanya nini leo?
Panapo matatizo tunataka suluhisho
Likizo inawekwa kando tunakaza mpaka kifo
Na tulivyo, sio watu wa matambiko
Tumeshiteka kambi na kupekua maficho
So,

Chorus

Chap chap chap chap ni sawa
M-Lab, pure math, rap ni dawa
Chap chap chap chap ni sawa
Pure mathematics (dogo kapagawa)
x2

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA