Taarifa kwa wafanyabiahara wa utalii kuhusu kusajili na kulipia ada ya leseni 2016

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
WAFANYABIASHARA WA UTALII KUSAJILI NA KULIPIA ADA YA LESENI YA MWAKA 2016

Wizara ya Maliasili na Utalii inawakumbusha wafanya biashara za utalii wasiokuwa na leseni ya biashara hiyo inayotolewa kwa mujibu wa sheria ya Utalii Na. 29 ya Mwaka 2008 Vifungu Na.10 na 31, kuwa wanatakiwa kusajili na kulipia ada ya leseni kwa mwaka 2016 ifikapo tarehe 31 Oktoba, 2016.

Biashara za Utalii husika ni hizi zifuatazo:
1Kampuni za kusafirisha watalii10Vivutio vya kuuza bidhaa za urithi (Cultural heritage centres)
2Kampuni za uwindaji wa kitalii11Wajasiriamali wa utalii wa utamaduni (Cultural tourism enterprises)
3Wawindaji Bingwa12
Kampuni za kukodisha vifaa vya utalii

4Kampuni za kusafirisha watalii kwa ndege13Maeneo ya michezo ya burdani (Theme parks, wildlife forms. Zoo, snake parks etc)
5Kampuni za kusafirisha watalii kwa Maputo (hot air balloon)14Kampuni za kukodisha magari kwa watalii
6Kampuni za kusafirisha watalii kwa farasi15Kampuni za kukatisha tiketi za ndege
7Kampuni za kusafirisha watalii kwa boti16Wakala wa kutoa huduma kwa watalii (tourist handling agents)
8Kampuni za kupandisha watalii Milimani17Nyumba za huduma za malazi (hoteli, loji, kambi za kitalii)
9Kampuni za utalii wa michezo ya kusisimua (tourism adventure sports)18Maduka ya zawadi za kitalii (Curio Chops)
i. Wizara inachukua nafasi hii pia kusisitiza kwamba ni kosa linalostahili adhabu kisheria kufanya biashara ya utalii bila ya kusajili na kulipia ada ya leseni kwa mwaka husika.

ii. Vilevile, tunapenda kuwafahamisha kuwa maombi kwa ajili ya leseni ya kufanya biashara ya utalii kwa mwaka 2017 yameanza kupokelewa katika Ofisi zetu zilizopo Dare s Salaam, Arusha, Mwanza na Iringa.

iii. Orodha ya wafanyabiashara ya utalii waliosajiliwa na kulipia ada za leseni inapatikana katika tovuti ya Wizara (www.mnrt.go.tz), na katika ofisi za Wizara zilizotajwa hapo juu.

Angalizo: Umma unatahadharishwa kutofanya biashara na kampuni za biashara za utalii ambazo hazina Leseni ya Biashara ya Utalii ya mwaka 2016, kwa kuwa kufanya hivyo ni kinyume cha Sheria.

Imetolewa na:

KATIBU MKUU
WIZARA YA MALIASILI NA UTALII
Simu: +255 22 2864230

Barua pepe:ps@mnrt.go.tz

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA