Posts

PICHA: HII NDIO IKULU YA DIAMOND PLATNUMZ ILIYOPO TEGETA

Image
Kupitia mtandao wa Instagram, mkali wa Bongo Fleva, Nasib Abdul aka Diamond Platnumz ameonyesha picha za mjengo wake mpya uliopo nje ya jiji la Dar Es Salaam eneo la Tegeta.

RAPPER FID Q APEWA TUZO YA `CHAMPION NA UMOJA WA NCHI ZA ULAYA EU

Image
Umoja wa nchi za ulaya EU wampa tuzo Fareed Kubanda a.k.a Fid Q ya CHAMPION of the 2015 Europe Year for Development in Tanzania ,Pia Fid Q alifunguka kwenye Amplifaya ya Cloudsfm nakusema amefarijika sana kupata Tuzo hiyo kwani itampa hamasa ya kufanya kazi kwa bidii zaidi. Pia Fid Q alisema amepata Tuzo hiyo kutokana na kujitolea kusaidia vijana katika jamii ili waache miadarati na japo kuwa darasa kwa sasa limefungwa ila anampango wa kulifungua tena upya darasa hilo.

Taarifa ya Wizara ya Nishati na Madini ya ufadhili wa masomo nchini China

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA NISHATI NA MADINI TAARIFA KWA UMMA UFADHILI WA MASOMO NCHINI CHINA. Wizara ya Nishati na Madini inapenda kuwataarifu watanzania wenye vigezo vya kuomba nafasi za masomo ya shahada ya juu ya Uzamili (Postgratuate) katika fani ya gesi na mafuta katika Chuo Kikuu cha Jiosayansi cha China kijulikanacho kama  China University of Geosciences (Wuhan) , Chini ya ufadhili wa Serikali ya Watu wa China, kuwa muda wa kutuma maombi hayo umeongezwa hadi kufikia tarehe 30/03/2015. Wizara ya Nishati na Madini inaendelea kuwasisitiza watanzania wenye vigezo kutumia fursa hii kwa kujaza fomu zinazopatikana katika tovuti za  http://www.csc.edu.cn/laihua au  www.campuschina.org  na  www.mem.go.tz . Pia wanaweza kufika katika Ofisi za Wizara ya Nishati na Madini, ghorofa ya Tatu ili kupata taarifa husika. IMETOLEWA NA; WIZARA YA NISHATI NA MADINI 20 Machi, 2015

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI, MACHI 21

Image

Kenya Airways Yapunguza Safari Zake Tanzania

Image
Kenya Airways Shirika la ndege la Kenya, Kenya Airways leo limeanza rasmi kupunguza safiri zake katika uwanja wa ndege wa Dar es Salaam kufuatia agizo la mamlaka ya anga ya Tanzania kuamuru shirika hilo kupunguza safari zake kutoka 42 kwa wiki hadi 14. Kenya Airways Serikali ya Tanzania inasema huo ndio mkataba wa tangu awali na kulaumu mamlaka ya anga nchini Kenya kwa kushindwa kuafikia maelewano na mamlaka ya Tanzania kuhusu jambo hilo. Tayari baadhi ya wasafiri wanaotumia ndege za shirika hilo wameanza kuathirika kufuatia shirika hilo kufuta baadhi ya safari kutoka Dar es Salaam chanzo:BBC

SIWEMA ADAI MTOTO CURTIS SIO MTOTO WA NAY WA MITEGO, AMTAJA BABA YAKE.

Image
Usiku huu kumezuka kutupiana maneno kati ya msanii wa Bongo Flava Emmanuel Elibariki maarufu kama Nay wa Mitego na mama mtoto wake Siwema. Kumezuka mjadala mkali kwenye mtandao wa Instagram mara baada ya Siwema kupost na kusema kwamba huyu mtoto wao Curtis sio wa Nay wa mitego na kutaja jina la Obasanjo kwamba ndiye baba halisi wa malaika huyu,na kuendelea kusema kwamba huyo  bwana ndiye alimvalisha pete. Mashabiki wamezidi kuchafu hali zaidi na kuanza kumponda Siwema kwa kauli yake na wengine wenye busara kutoa ushauri swala hili lijadiliwe kifamilia na sio kwenye mitandao ya kijamii. Ugomvi huu baina ya Siwema na Nay wa Mitego umeibuka hivi karibuni mara baada ya gazeti moja maarufu la udaku kuandika habari juu ya fumanizi alilolifanya Nay wa Mitego jijini Mwanza na kumkuta Siwema akiwa na Serengeti Boy, hali iliuompelekea Nay wa Mitego kumchukua mwanaye na kurudi naye jijini Dar Es Salaam.

WALIMU WAJIONDOA CWT NA KUUNDA CHAKAMWATA

CHAMA kipya cha Kutetea Haki na Maslahi ya Walimu Tanzania (CHAKAMWATA) kimesajiliwa rasmi na kupata cheti cha usajili wa kudumu kutoka Wizara ya Kazi na Ajira. Akizungumza na  FikraPevu , Katibu Mkuu wa Chakamwata, Mwalimu Meshack Kapange, anasema chama hicho kipya kinaundwa na walimu nchini waliojiondoa kutoka mikononi mwa Chama Cha Walimu Tanzania (CWT). Kapange amesema mchakato wake wa kukisajili chama hicho ulianza miaka minne iliyopita, hadi hivi juzi kilipopewa usajili wa kuendelea na shuhuli zake kisheria. “Ni furaha iliyoje kupata usajili huu wa chama chetu cha kutetea haki na maslahi ya walimu? Huu ni ukombozi kwa walimu wanaokatwa asilimia mbili za mishahara yao bila kurejeshewa wanapostaafu,” anasema Katibu Mkuu huyo. Kuundwa kwa chama kipya hicho kumetajwa na wachambuzi wa mambo kwamba kunaweza kuipasua CWT na pia kutahitimisha ukiritimba wa muda mrefu mrefu wa chama hicho. Aidha, chama hicho kitatoa fursa sasa kwa walimu nchini kuwa na hiyari ya kujiunga na chama amb

Amwacha 'sugar mammy' wake baada ya 'kumtumia kupata makaratasi'

Mwanamke mmoja nchini Uingereza mwenye miaka 64 ametelekezwa na kuachwa na kijana wake wa Kiafrika mwenye miaka 26 baada ya kumkamilishia taratibu za visa. Mwanamke huyo mlemavu, Patricia ambaye alimpenda mvulana wa asili ya Tunisia kupitia mitandao ya kijamii, alimkamilishia taratibu zote za kufika na kuishi Uingereza. Patricia alijuana na Mtunisia huyo, Mondhler katika tovuti ya mahusiano na kumpenda hatimaye kufanya taratibu za ndoa. Patricia ambaye anaishi Midlands, alielezea namna alivyokua akitafuta mpenzi wa kuishi naye milele katika redio Channel 5 nchini Uingereza. "Mwanzoni alionesha kuwa ana mapenzi ya dhati na kunishawishi kuwa miaka haimaanishi kitu zaidi ya tarakimu tu", alieleza Patricia. Lakini Mondhler alipofika tu Uingereza alimtelekeza na kumuacha mwanamke huyo solemba. via   TRT Swahili

TANZANIA INSTITUTE OF BANKERS -CONTINUING BANKING EDUCATION PROGRAMME 2015

Image

NEW VIDEO: KUTOKA KWA JUX - NIKUITE NANI

Image

Ratiba England | EPL KESHO NA JUMAPILI

Image
Ratiba England | EPL Kesho Jumamosi March 21 15:45 Manchester City vs West Brom  18:00 Aston Villa vs Swansea  18:00 Newcastle Utd vs Arsenal  18:00 Southampton vs Burnley  18:00 Stoke City vs Crystal Palace  18:00 Tottenham vs Leicester  20:30 West Ham vs Sunderland Jumapili March 22 16:30 Liverpool vs Manchester United  19:00 Hull City vs Chelsea  9:00 QPR vs Everton

HOTUBA YA ZITTO ALIYOTAKA KUITOA BUNGENI JANA

Image
Mh. Zitto Zuberi Kabwe Mheshimiwa Spika, nilijiunga na Bunge lako tukufu mwaka 2005 nikiwa kijana mdogo mwenye malengo ya kupaza sauti ya vijana kwenye masuala yanayohusu nchi yetu na pia kutetea maslahi ya wananchi wa Jimbo la Kigoma Kaskazini na Mkoa wa Kigoma. Katika kudumu kwangu kama mbunge nililelewa na kukuzwa na chama cha siasa cha CHADEMA ambacho kupitia chama hiki niliingia Bungeni. Chama hiki kilinilea na kunikuza tangu nikiwa na umri wa miaka 16 na kupitia chama hiki nimejifunza mambo mengi sana. Nimeijua nchi yangu, nimejua siasa na nimejulikana ndani na nje ya nchi. Nitakuwa mwizi wa fadhila nisipotoa shukrani zangu za dhati kabisa kwa CHADEMA na viongozi ambao nimefanya nao kazi muda wote nikiwa mwanachama na kiongozi. Mheshimiwa Spika, Chama kilinikuza kama mwanasiasa lakini watu wa Kigoma Kaskazini ndio walionipa kiti hiki ninachokalia kama Mbunge. Juzi nilipokuwa nyumbani nilipata fursa ya kuwashukuru rasmi wananchi kwa imani waliyonipa kuwatumikia kwa