Amwacha 'sugar mammy' wake baada ya 'kumtumia kupata makaratasi'




Mwanamke mmoja nchini Uingereza mwenye miaka 64 ametelekezwa na kuachwa na kijana wake wa Kiafrika mwenye miaka 26 baada ya kumkamilishia taratibu za visa.

Mwanamke huyo mlemavu, Patricia ambaye alimpenda mvulana wa asili ya Tunisia kupitia mitandao ya kijamii, alimkamilishia taratibu zote za kufika na kuishi Uingereza.

Patricia alijuana na Mtunisia huyo, Mondhler katika tovuti ya mahusiano na kumpenda hatimaye kufanya taratibu za ndoa.

Patricia ambaye anaishi Midlands, alielezea namna alivyokua akitafuta mpenzi wa kuishi naye milele katika redio Channel 5 nchini Uingereza.

"Mwanzoni alionesha kuwa ana mapenzi ya dhati na kunishawishi kuwa miaka haimaanishi kitu zaidi ya tarakimu tu", alieleza Patricia.

Lakini Mondhler alipofika tu Uingereza alimtelekeza na kumuacha mwanamke huyo solemba.

via TRT Swahili

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA