Muhimu ni kwa artist wa Bongofleva wenye majina kuwa tayari kukutana wote katika mikutano inayoendelea sasa ikiongozwa vyema na wasanii wenzetu ambao wameshalipia ada ya chama chetu BASATA na tayari mikutano inaendelea mara kwa mara japo mara nyingi wanaojitokeza ni artist wenzetu wakubwa kwa wadogo lakini si wale wanaoaminika kuwa na majina makubwa. Watambue kwamba wakati ndio huu wa sisi kutambulika kama wasanii ili tuweze kudai na kupata haki zetu tunazostahili toka katika vyanzo kibao vya michongo vilivyopo kwa ajili ya muziki wetu, vitu kama usambazaji, udhamini na mambo kibao ambayo leo yanakuja lakini wanachukua watu ambao kimsingi ndio wanaotutesa na kutunyima dili miaka yote. Rais alisema tumueleze shida zetu, wajanja wakasema eti shida yetu ni studio tu, wakati tuna matatizo kibao ya msingi ikiwemo sheria ya haki miliki katika katiba ilivyopitwa na wakati na mambo kibao yanayosabisha artist wakila bia mbili,tatu wanafulia!. Ila artist wa kibongo hasa wale wanaojitambua lazima