KIFO CHA ZAOLA PARETO TANZANIA
Zao la pareto ni miongoni mwa mazao ambayo wakulima wamekuwa wakipunguza na kuacha kuyalima kabisa, huenda ni kutokana na bei yake kuwa chini au soko sumbufu. Kamera ya Benjamin Kaminyonge ilipita maeneo ya wilaya ya Makete, kata ya Matamba na kuona zao hilo likiwa kwenye shamba la ekari moja ndani ya kijiji kizima huku kukiwa na mazao kama mahindi, ngano, maharage na alzeti kwa wingi. (picha: benjaminkaminyoge.blogspot.com)