VIJANA WATAKIWA KUJIEPUSHA NA MAKUNDI HATARISHI

Vijana Mkoani Mara wametakiwa kutojihusisha na makundi korofi na hatarishi na badala yake kujiunga na Club za Vijana ambazo zina lengo la kuleta mabadiliko na kupeana mawazo ambayo yatawasaidia katika maisha katika kujiendeleza na kupata mafanikio ya Kiuchumi,Elimu na mambo mengine ya msingi.

Kauli hiyo imetolewa na Mratibu msaidizi wa Idara ya Vijana ya Youth to Youth kutoka Jijijini Mwanza Sadick Bakary alipokuwa akizungumza na mwakilishi wa blog hii kutoka Musoma Bw. Binda kuhusiana na kampeni ya kuhamasisha Vijana Mkoani Mara kuepukana na kujiiingiza katika makundi hatarishi ambayo yamekuwa hayana faida na kuanzisha Club ambazo zitawasaidia kuwa na mtazamo wa mabadiliko ya kimaisha.

Alisema kijana kama kijana anaweza kutatua tatizo la kijana mwenzake kwa kumpa mawazo na kusikilizwa hivyo kwa kuanzisha Club kama hizo za vijana kutaweza kupata nafasi ya kukutana na kuweza kupeana mawazo ya kubadilika na kuwa na mawazo ya kujishughulisha kwa kutafuta kipato halali na kuweza kupeana Elimu zaidi ya kujiendeleza.

Alidai Club hizo zitasaidia kumfanya kijana kujitambua na kuona tatizo la kijana mwenzake kama tatizo lake na kuweza kumsaidia ili mwenzake aweze kuonekana kijana ambaye hana matatizo na kuweza kupata fursa za kupata msaada kutoka katika jamii na watu wanaomzunguka katika shughuli za kila siku.

"Vijana ambao watakuwa katika Club hizi zitakazoanzishwa atakuwa na mawazo ya kuwatoa vijana katika makundi hatarishi na kumpa halisi ya matendo hasa juu ya ukatili wa aina yeyote kwa Wanawake,Wasichana na Watoto kwa kuwa vijana wanayo nafasi kubwa na kufanya kazi hiyo.

"Tunataraji kuanziasha Club hizi Mashuleni na Mitaani na kuhamasisha vijana kujiunga kwa wingi ili kwa namna moja ama nyingine tuweze kubadilishana mawazo na kuweza kukomesha vitendo vya ukorofi ambavyo havina tija na kuwa kitu kimoja katika kuleta mabadiliko ya kimaisha,"alisema Sadick.

Alisema kwa upande wa Mkoani Mwanza mpaka sasa kumeanzishwa Club 180 ambazo zimeungana na kuunda Muungano wa Vijana Mkoa wa Mwanza na wanafanya kazi ya kuhamasisha Vijana kutojiunga na makundi hatarishi na kukomesha masuala yote ya unyanyasaji na kufanya shughuli za kujipatia kipato kwa kupitia Elimu ya ujasiriamali ambayo wamekuwa wakiipata kupitia Club zao

Aliongeza kusema kuwa mpaka sasa wamekwisha tembelea Club 13 katika Mkoa wa Mara na wataendelea kuhamasisha ili lengo la kuwakusanya Vijana na kuzungumza nao kuhusiana na athari ambazo zinapatikana katika kujiingiza katika makundi hatarishi.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA