Na Waandishi Wetu Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva a.k.a Rais wa Manzese, Hamad Ally ‘Madee’ hivi karibuni alilala katika Kituo cha Polisi cha Kigamboni, Dar akihusishwa na utekaji wa dereva wa bodaboda, Suedi Waziri (pichani) kisha kumpa kipigo ambapo inadaiwa alisoteshwa kinomanoma. Msanii wa Muziki wa Bongo Fleva a.k.a Rais wa Manzese, Hamad Ally ‘Madee’ akiwa mikononi mwa Polisi. Baada ya tukio hilo lililotokea mwishoni mwa wiki iliyopita, Ijumaa lilinasa picha zinazomuonyesha msanii huyo akihenyeshwa kituoni hapo huku mmoja wa watu wanaoishi karibu na eneo hilo akinyetisha kuwa, licha ya ustaa wake Madee alikiona cha mtemakuni. Dereva wa bodaboda, Suedi Waziri aliyetekwa na kushambuliwa na Madee. “Mimi nilikuwepo pale kituoni, nilimshuhudia akiwa amepigwa pingu huku polisi kama sita hivi, mmoja akiwa na silaha wakiwa wamemuweka chini ya ulinzi wakimpeleka mahakamani.“Alionekana aliyechoka sana huku akiwa na hofu ila inavyodai