Posts

Wapiganaji wa IS kuondoka kusini mwa Damascus

Image
Na RFI Nchini Syria, makubaliano yaliowashangaza wengi yamefikiwa juu ya kuondoka Jumamosi hii kwa watu 4000 katika maeneo matatu kusini mwa mji wa Damascus. Watu hao ni pamoja na wapiganaji wa kundi la Islamic State (IS), wapiganaji wa kundi la Al-Nusra Front na raia wa kawaida, vyanzo vilio karibu na mazungumzo vimebaini Ijumaa Desemba 25. Hii ni mara ya kwanza kwa mkataba kama huu unaolishirikisha kundi la Islamic State. Mkataba huu unaruhusu watu 4000, ambao ni raia pamoja na wapiganaji hasa wa kundi la Islamic State na wale wa kundi la Al-Nusra Front, kuondoka katika kambi ya wakimbizi wa Palestina ya Yarmuk, k

Uchaguzi wa marudio hatutaki kusikia Zanzibar

Chama cha Wananchi CUF Zanzibar kimesema hakipo tayari kupokea maazimio ya mazungumzo ya kutafuta mwafaka wa Uchaguzi Mkuu kama yatakuwa yanakwenda kinyume na maamuzi waliofanya wananchi kupitia Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 Mwaka huu. Tamko hilo limetolewa na Mkurugenzi wa Uchaguzi na Mipango wa Chama hicho, Omar Ali Shehe katika mahojiano maalum na Nipashe Jumapili juu ya mazungumzo ya kutafuta mufaka wa Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar. Mazungumzo hayo yanaogozwa na Rais wa Zanzibar DK. Ali Mohamed Shein na kuwashirikisha Makamo wa kwanza wa Rais wa Zanzibar na Mgombea urais kupitia CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi pamoja na marais wastaafu wa Zanzibar. Alisema CUF kiko tayari kupokea maamuzi na kuyaheshimu kutoka katika Kamati hiyo ya mazungumzo kama yatakuwa yamezingatia maamuzi ya wananchi waliyoyafanya kupitia Uchaguzi Mkuu huo. Inaaminika kuwa matokeo yaliyofutwa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) yalikuwa yakimpa u

Magazeti ya Leo Jumatatu, December 28

Image
           

Ahukumiwa kwa alichokiandika Facebook kuhusu uvamizi wa kituo cha polisi Tanzania

Image
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imemhukumu Bruno Kimaryo, kifungo cha miaka miwili jela baada ya kupatikana na hatia ya kusambaza ujumbe katika mtandao wa kijamii wa kuyapongeza majambazi yaliyovamia Kituo cha Polisi cha Stakishari na kuua polisi. Aidha, mshtakiwa huyo ametakiwa ama kulipa faini ya Sh. 600,000 kwa kosa hilo.  Katika tukio la Stakishari lililotokea Julai 12, mwaka huu, majambazi yalivamia kituo hicho na kuua polisi wanne na raia watatu pamoja na kupora bunduki 20 aina ya Sub Machine Gun (SMG).  Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Mkazi Mkuu, Waliarwande Lema, baada ya kupitia ushahidi uliotolewa na mashahidi watano wa upande wa mashtaka. Alisema vielelezo vitano na utetezi wa mshtakiwa vinaonyesha kuwa Bruno alifurahia kitendo kilichofanywa na majambazi hao na alitamani kila kituo cha polisi kivamiwe. Alisema mshtakiwa huyo katika ujumbe wake huo alitumia viunganishi vya maneno yasiyokuwa ya kibinadamu ya auawe, avamiwe na kuwa utetezi wake u

Magufuli amalizia Baraza la Mawaziri

Image
Picha naEast Africa Television (EATV) Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemalizia kujaza nafasi za uteuzi wa Mawaziri na Naibu Waziri alizobakiza wakati akitangaza baraza la Mawaziri la kwanza katika awamu ya tano ya utawala wake Uteuzi huo ni kama ifuatavyo; 1. Amemteua Profesa Jumanne Maghembe kuwa waziri wa maliasili na utalii. 2. Dk. Philip Mpango ameteuliwa kuwa Waziri wa Fedha na Mipango 3. Dk Joyce Ndalichako ameteuliwa na kuwa Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi 4. Mhandisi Gerson Lwenge ameteuliwa kuwa Waziri wa Maji na Umwagiliaji. 5. Prof. Makame Mbarawa ameteuliwa kuwa waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano 6. Mh. Hamad Masauni ameteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Katika hatua nyingine Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewatakia heri watanzania wote katika Sikukuu za Maulid, Christmas na Mwaka Mpya na kuwataka washerehekee kwa amani na utulivu. Ger

Magazeti ya Leo Alhamisi, December 24

Image