Posts

NEW UPTODATE: WEMA SEPETU AVISHWA PETE NA MWINYI KUTOKA MACHOZ BAND

Image
 Mtu mzima Mwinyi akaenda chini pwaaaa...  Akakumbatiwa watu weweeeeeee  Heeeh si akaweka pete kidoleni pale kabaaaaaaa  Mabusu hihaaaaa, watu pipooooo  Wema Sepeta na Bodyguard wake  Wema & Abou

CHADEMA YAITEKA MTWARA

Image
  Aliekuwa Mbunge wa Arusha Mjini, Mh Godbless Lema akihutubia maelfu ya wananchi wa Mtwara katika Viwanja vya Mashujaa jana. CHADEMA wako mikoa ya kusini mwa Tanzania kwa ziara ya kuimarisha chama hicho katika maeneo hayo na pia kuutanzaza mapango wao mpya wa kuwashirikisha wananchi katika shuguli za chama (Movement for Change-M4C) kuanzia jana hadi Juni 11, 2012 ********* DHANA ya kuwa mikoa ya kusini ni ngome ya Chama cha Mapinduzi jana ilifutika vichwani mwa wakazi wa mikoa hiyo, baada ya umati mkubwa kujitokeza, kuulaki msafara wa viongozi na hatimaye kuhudhuria mkutano mkubwa wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Mashujaa, mkoani Mtwara.  Msafara huo wa kitaifa ukiongozwa na Mwenyekiti Freeman Mbowe, ulipata mapokezi ya vijana wakiwa katika msafara wa pikipiki magari na baiskeli karibu na daraja la Mikindani na kuelekea katika uwanja wa Mashujaa ambapo umati mkubwa wa watu ulifurika kupita kiasi.  Akihutubia katika mkutano huo Mwenyekiti wa CHADEMA Ta

BASATA YAWATAKA WASANII KUONGEZA THAMANI KATIKA KAZI ZAO

Image
Mtendaji Mkuu wa asasi ya Musoma Handcrafts Haroun Sabili akitoa elimu kwa Wasanii na Wajasiriamali wa Sanaa za mikono kwenye programu ya Jukwaa la Sanaa wiki hii. Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti, Mafunzo na Habari wa BASATA Godfrey Lebejo akisisitiza jambo wakati akihitimisha programu ya Jukwaa la Sanaa wiki hii. Aliwataka wasanii kuongeza thamani katika kazi wanazozalisha. Akina mama Wasanii wa Sanaa za mikono wakiangalia moja ya kazi iliyobuniwa na kuongezewa uthamani. Kazi hiyo ilikuwa imetengenezwa na malighafi kutoka masalia ya viumbe wa baharini. Sehemu ya Wasanii na Wadau wa Sanaa za Mikono waliohudhuria kwenye programu ya Jukwaa la Sanaa wiki wakifuatilia darasa kwa makini. Na Mwandishi Wetu Huku kukiwa na juhudi za kutambuliwa na kuthaminiwa kazi za wasanii ndani na nje ya nchi, Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) limewataka wasanii kuongeza thamani kwenye kazi zao ili kuzipa ubora zaidi. Wito huo umetolewa mapema wiki hii na Mkurugenzi w

MTATIRO: HILI LA ZANZIBAR HALIUNGWI MKONO “LABDA NA MWENDA WAZIMU TU”

Image
JULIUS MTATIRO katibu mkuu wa chama CUF Tanzania bara ********************* Habari za uchomaji wa makanisa Zanzibar katika vurugu za hivi karibuni haziungwi mkono kwa namna yoyote ile. Yeyote anayefanya vitendo hivi ni gaidi kwa sababu anafanya vitendo vya kigaidi. Serikali ya zanzibar ichukue hatua kali sana za kisheria kwa yeyote aliyehusika na vitendo hivi bila kujali yeye ni nani. Kuchoma makanisa ni jambo la hatari sana, sielewi anayefanya hivi yeye ni dini gani, sijui ni dini ipi inayoruhusu uchomaji wa nyumba za ibada za dini nyingine, ni dini ya shetani peke yake inaweza kufanya hivyo. Kuna watu wanasema ati ni “waislamu” ndiyo wanafanya vitendo hivyo, mie nakataa, nasema wanaofanya hivyo siyo waislamu.  Waislamu walioko Zanzibar naowajua mimi ni wakarimu, ni watulivu na wasikivu na wanapenda amani. Hata mapambano ya wafuasi wa CUF na CCM yaliisha kwa wao wenyewe kuridhiana. Wazanzibari siyo wakatili kiasi hiki. Kuchoma makanisa hakuwezi kufananishwa

HIVI NDIVYO GRADUATION YA SSPRA ILIVYOFANA

Image
Wiki iliyopita siku ya Jumamosi ilifanyika sherehe ya kuwaaga mwaka wa 3 ambao walikuwa ni wanachama wa SSPRA ambapo sherehe hii ya mahafari ilifanyika katika ufukwe wa ziwa Victoria- -Royal Sunset Beach. Mgeni rasmi katika mahafari hayo alikuwa ni Afsa uhusiano (Public Relations Manager) wa halmashauri ya jiji la mwanza  BW. Joseph Alex Mlinzi. Wanachama 45 walitunukiwa vyeti vyao na wengine 21 kutunukiwa vyeti vya shukrani kwa kuweza kuiongoza vizuri Association mpaka hapa ilipofikia. Mgeni rasmi .Joseph Mlinzi aliweza kuwapa nasaa wahitimu wote na kuweza kuipongeza  Association kwa kuweza kupiga hatua kubwa sana ukilinganisha na umri wa Association  tangu imeanzishwa...Mgeni rasmi pia aliweza kutoa kiwango cha shilingi Million 1 na laki 2(1,200,000) kwa ajili ya kuweza kuimarisha mfuko wa chama. Zifuatazo ni baadhi ya picha ambazo zilichukuliwa wakati wa sherehe hiyo. Mgeni Rasmi Joseph Mlinzi ambaye ni Meneja Uhusiano wa jiji la Mwanza akiingia ukumbini. Mwenyek