Posts

Watishia kufunga viwanda vya bia na vya pombe kali

Image
Watengenezaji wa bia na vinywaji vikali, wametishia kufunga baadhi ya viwanda iwapo Serikali haitaipunguza ongezeko la kodi la asilimia 20 iliyolipishwa kinyume na tozo ya asilimia 10 iliyopitishwa na Bunge. Uamuzi huo umekuja baada ya wenye viwanda vya vinywaji hivyo kubaini kuwa Muswada wa Sheria ya Fedha wa mwaka 2014/15 uliotolewa Julai 11, mwaka huu, unataja kuwa kodi kwa bidhaa hizo itakuwa asilimia 20. Akizungumza jana, mwakilishi wa wenye viwanda nchini, David Mgwassa alisema uamuzi wa kupandisha kodi kinyemela umewaacha njiapanda wenye viwanda kwa kuwa hawajui walipe kodi ipi kati ya asilimia 10 au 20 na kwamba, iwapo Serikali haitapunguza, watafunga baadhi ya viwanda ili kumudu ongezeko hilo jipya la kodi. “Kila kampuni inafanya utafiti ili kufunga viwanda vyote na kubaki na kimoja kikubwa kitakachopunguza gharama. Pia ikumbukwe kuwa

DOWNLOAD NA KUSIKILIZA SINGLE MBILI ALIZOZIACHIA ALI KIBA LEO.

Image
Baada ya wapenzi wa muziki Tanzania kusubiri kwa muda mrefu sasa wamepata nafasi ya kujiburudisha na ngoma mpya kutoka kwa Alikiba. Tarehe 25 Julai, 2014 Alikiba ameachia single mbili mpya kwa wakati mmoja ziitwazo “Mwana” na “Kimasomaso”. Mwana imetengenezwa na Manwalter kutoka studio ya combination sound na Kimasomaso imekuwa sampled kutoka kwa Marehemu Issa Matona ikiwa imetayarishwa na producer Marco Chali kutoka MJ records. Alikiba anajulikana ndani na nje ya Tanzania kwa hit zake kama Cinderella, Mapenzi yanarun dunia, Single boy, na Dushelele. Cinderela ndiyo wimbo ambao mpaka sasa umeweka rekodi ya kuuza copy nyingi katika Afrika Mashariki mwaka 2008.    Mwaka 2012 Alikiba alishinda tuzo ya best Rhumba/ Zouk na wimbo wake wa “Dushelele” katika tuzo za Kilimanjaro Tanzania Music Awards. Alikiba anajulikana kwa uwezo wake mkubwa wa kuimba na utunzi wa nyimbo pamoja na kuwa mburudishaji mkali sana katika show zake za live na mpaka sasa ametembea nchi n

SOMA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JULY 25

Image

PICHA KALI 10 ZA WASANII WA BONGO #THROWBACKTHURSDAY AKA #TBT, TAFADHALI CHEKA TARATIBU

Image
Kama ilivyo kawaida leo ni siku ya Alhamis ambapo kupitia mtandao wa Instagram kuna utaratibu wa watumiaji wake kutuma picha zile za kitambo au enzi hizo.   Picha hizi zimekuwa za kuvutia kwani zinaonyesha hasa watu wanapotokea ukilinganisha kwa sasa walipo katika zile hatua za ukuaji na utafutaji wa maisha. Nimekukusanyia baadhi ya picha za wasanii maarufu hapa bongo land, ambao utawaona wasanii kama Fid Q, Ferooz, Sugu, Baba Levo,Dudu baya, Juma nature, D nob, MwanaFA, AY, TID the late Langa, Ali Kiba, Diamond Platnumz, Queen Darlin, Joho Makini, Nikki wa pili. kwenye picha hii anaonekana Fid Q, Erick Shigongo,D nob Ali Kiba pamoja na Diamond Platnumz AY MwanaFA MwanaFA katika pozi Dudu Baya Juma Nature, Ferooz, Baba levo kwa mbali TID, RAY C NA Q-CHILLA The late Langa, TID Diamond Plaatnumz akiwa na dada yake Queen Darlin Joho Makini mwenye Kofia na Nikki wa pili wakiwa na mama yao mzazi.

DIVA LOVENESS WA CLOUDS FM ATOA UJUMBE MZITO KWA WASANII WA BONGO FLEVA .

Image
Kama umekuwa mfatiliaji mzuri wa social networks na msikilizaji wa clouds fm kupitia kipindi cha "Ala za Roho"jina Diva the bawse sio geni kabisa, Diva amekuwa ni mtu wa kutukanwa pindi anapotupia chochote kwenye mitandao ya kijamii, kuna msemo unaosema hauwezi kuwafurahisha watu wote lakini kwa haya maneno aliyoyaandika na kuwahusia wasanii wenzake nayachukulia kwa mapana zaidi hasa kwa wasanii wanaotaka kujitangaza kimataifa zaidi. Hiki ndicho  alichokiandika kupitia mtandao wa instagram. divathebawse "Goodmorning Tanzania. So kuna Mtu aliniuliza kwanini Nigeria wanakuwa wameishika Africa na kuwa nominated kwenye Tuzo nyingi Africa na duniani kwa ujumla.  Kwanza ifahamike Nigeria kuna watu zaidi ya Mil170 na Tanzania ni kama watu Mil44 hivi kwa harakaharaka na hatutaweza hata robo kushindana nao sababu hawa jamaa kwanza wanashinda katika internet. Watumiaji wa Internet Tanzania ni asilimia haizidi 4 au 5. Hatufiki watu mil1 na nusu na wengi wa

VAN GAAL AANZA KWA KISHINDO MANCHESTER UNITED, YAICHAPA LOS ANGELES GALAXY 7-0

Image
Kocha mpya wa Manchester United, Louis van Gaal ameanza vizuri kibarua chake cha kukinoa kikosi hicho baada ya kupata ushindi wa goli 7-0 dhidi ya Los Angeles Galaxy katika mchezo wa kirafiki uliochezwa nchini Marekani.  kocha Van Gaal wa manchester United Man U walionekana kucheza soka la kuelewana zaidi ambapo mpaka wanakwenda mapumziko walikuwa wakiongoza mabao matatu kwa sifuri. Katika kipindi cha pili Man United walionesha kubadilika kwa kiwango cha hali ya juu, ambapo walilishambulia lango la Los Angeles Galaxy na kufanikiwa kupata mabao mengine manne na hivyo kufikisha idadi ya mabao 7-0 mpaka dakika 90 zilipomalizika.   Mabao ya Man United katika mchezo huo ambao kwa saa za hapa nyumbani Afrika mashariki umechezwa majira ya alfajiri lakini kwa huko Marekani ilikua ni usiku, yamefungwa na Danny Welbeck huku Wayne Rooney, Reece James na Ashley Young wakifunga mabao mawili kila mmoja. story:bongo5