DOWNLOAD NA KUSIKILIZA SINGLE MBILI ALIZOZIACHIA ALI KIBA LEO.

Baada ya wapenzi wa muziki Tanzania kusubiri kwa muda mrefu sasa wamepata nafasi ya kujiburudisha na ngoma mpya kutoka kwa Alikiba. Tarehe 25 Julai, 2014 Alikiba ameachia single mbili mpya kwa wakati mmoja ziitwazo “Mwana” na “Kimasomaso”.
Mwana imetengenezwa na Manwalter kutoka studio ya combination sound na Kimasomaso imekuwa sampled kutoka kwa Marehemu Issa Matona ikiwa imetayarishwa na producer Marco Chali kutoka MJ records.


Alikiba anajulikana ndani na nje ya Tanzania kwa hit zake kama Cinderella, Mapenzi yanarun dunia, Single boy, na Dushelele. Cinderela ndiyo wimbo ambao mpaka sasa umeweka rekodi ya kuuza copy nyingi katika Afrika Mashariki mwaka 2008. 
 
Mwaka 2012 Alikiba alishinda tuzo ya best Rhumba/ Zouk na wimbo wake wa “Dushelele” katika tuzo za Kilimanjaro Tanzania Music Awards. Alikiba anajulikana kwa uwezo wake mkubwa wa kuimba na utunzi wa nyimbo pamoja na kuwa mburudishaji mkali sana katika show zake za live na mpaka sasa ametembea nchi nyingi sana duniani kuburudisha wapenzi wa muziki. Sasa unaweza kupata nyimbo mbili mpya za Alikiba bure katika tovuti ya Mkito 
DOWNLOAD KUTOKA MKITO

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA