MISS MWANZA KUFANYIKA IJUMAA YA TAREHE 14/6/2013

Sindano la kumtafuta mrembo wa mkoa wa Mwanza, linatarajiwa kufanyika June 14 katika viwanja vya Yatch Club jijini Mwanza.

Warembo 18 kutoka wilaya mbalimbali za mkoa wa Mwanza wamejitokeza kushiriki shindano hilo la aina yake huku. 
 
Burudani inayosubiriwa kwa hamu kubwa ni Mh. Mbunge Joseph Mbilinyi maarufu kama sugu atakapo panda jukwaani kukumbushia enzi hizo...akishindikizwa na mkali mwingine wa Chege Chigunda kutoka TMK.

Warembo wote wanatarajiwa kuanza kambi rasmi Jumanne hii katika moja ya hoteli maarufu jijini humo.

Itakumbukwa mkoa wa Mwanza tayari ulishatoa Mrembo wa Tanzania, ambaye ni Nasreem Karim 2009 na Miriam Gerald 2010. Pamoja na mchakato wa shindano la urembo kuendelea kwa hivi sasa nchini, macho na masikio yapo mkoani Mwanza, ambako kumekua kukileta changamoto na upinzani mkali wa warembo kila Mwaka.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA