MKUU WA MKOA WA MWANZA AFUNGUA KAMPENI YA USAFI JIJINI MWANZA

Mkuu wa mkoa wa Mwanza Mh.Evarist Ndikiro amefungua rasmi kampeni ya kuweka jiji la Mwanza katika hali ya usafi akishirikiana kwa ukaribu kabisa na Meya wa jiji la Mwanza Mh.Stanslaus Mabula, kampeni hii imeandaliwa na Halmashauri ya jiji la Mwanza ikishirikiana kwa ukaribu kabisa na chuo kikuu cha mtakatifu Agustino (SAUT) kilichopo jijini hapa.

Kampeni hii inalengo la kutoa elimu na kuhamasisha jamii juu ya umuhimu wa kuliweka jiji la Mwanza katika hali ya usafi, kampeni hii imekuwa na kauli mbiu hii 
"Pamoja Tuliweke Jiji letu safi"
Mkuu wa mkoa wa mwanza MH.Evarist Ndikiro akiwa na baadhi ya viongozi wengine wa jiji la Mwanza katika kuzindua kampeni ya usafi leo katika jiji la mwanza.
Wa pili kutoka kushoto ni Meya wa jiji la Mwanza Stanslaus  Mabula pamoja na mkuu wa mkoa wa Mwanza Evarist Ndikiro katika kampeni ya usafi.
Mkuu wa mkoa wa mwanza mh.Evaristi Ndikiro akifanya usafi wa jiji la mwanza leo.
Wa pili kutoka kushoto ni meya wa jiji la mwanza na kulia kwake ni mkuu wa mkoa wa mwanza Mh.Ndikiro wakifanya usafi
Mkuu wa mkoa wa mwanza akipewa  mfagio
Mkuu wa mkoa wa Mwanza akishika mfangio kama ishara ya kushirikiana na wakazi wa jiji la mwanza katika suala nzima la usafi.
Baadhi ya wanachama wa SSPRA kutoka chuo cha SAUT wakishiriki katika kufanya usafi pia.
hawa ni baadhi wa wakazi wa jiji la mwanza wakiwa katika zoezi la usafi ililofunguliwa leo na mkuu wa mkoa wa mwanza MH.Evarist Ndikiro 
    Baadhi ya wanachama wa sspra wakifanya usafi.


Kutoka kushoto ni rasi wa chuo cha mtakatifu augustino Mh. Dovakmwene Mscheshi akifanya usafi pamoja na wakazi wa jiji la mwanza.
 Wakazi wa jiji la mwanza wakifany usafi

 Wakazi wa jiji la mwanza wakifanya zoezi la usafi leo
Mwenyekiti wa media and publications Mussa Mbilinyi akishiriki leo katika suala nzima la usafi wa jiji.

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA