Posts

TAARIFA YA ACT TANZANIA KWA UMMA

Image
Chama cha Wazalendo (ACT - Tanzania ) Kama mnavyofahamu, Chama cha Wazalendo ACT-Tanzania kitafanya mkutano wake mkuu na uzinduzi wa chama mnamo tarehe 28 na 29 Machi 2015. Katika mkutano Mkuu chama kitapitisha katiba mpya ya chama na kufanya uchaguzi wa nafasi mbalimbali za uongozi ikiwemo Kiongozi wa chama, Mwenyekiti wa Chama, Makamu wenyeviti, Katibu Mkuu na Manaibu makatibu wakuu. Pia chama kitachagua wajumbe wa Kamati Kuu na Halmashauri Kuu. Katika uzinduzi wa chama tarehe 29 Machi 2015 kuanzia saa tisa alasiri, viongozi mbalimbali wa ndani na nje ya nchi wamealikwa. ACT – Tanzania imemwalika Prof. Ibrahim Haruna Lipumba, Mwenyekiti wa Taifa wa CUF kuzungumza kwa niaba ya vyama vya upinzani nchini kuhusu ‘ kwa nini Tanzania bado ni nchi masikini na nini cha kufanya kuondoa umasikini’. Pia viongozi wote wa vyama vya siasa nchini, mabalozi wa nchi mbalimbali na wakuu wa asasi zisizo za kiserikali wamealikwa. Uzinduzi utaonyeshwa moja kwa moja na vituo vya tel

ASKARI MAGEREZA NA WA FFU WAKAMATWA NA NOTI BANDIA NA SARE ZA JWTZ

Image
Naibu kamishna wa jeshi la polisi Mkoani Simiyu, Charles Mkumbo akiwaonesha waandishi wa habari baadhi ya sare za JWTZ ambazo zilikamatwa askari wa jeshi la polisi Mkoani Simiyu pamoja na Askari Magereza wilayani Bariadi Jeshi la polisi mkoani Simiyu linawashikilia askari wawili wa jeshi la magereza na polisi kwa kukutwa na noti bandia ikiwa pamoja na sare za jeshi la wananchi Tanzania (JWTZ). Akitoa taarifa za kukamatwa kwa askari hao Kamanda wa polisi mkoani hapa Naibu Kamishina, Charles Mkumbo alisema kuwa askari hao walikamatwa juzi majira ya saa 9 mchana katika mtaa wa Old Maswa kata ya Nyakabindi Wilayani Bariadi. Mkumbo Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni askari mwenye namba H 2420 PC Seleman Juma (25) ambaye ni askari wa kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) Mkoani Simiyu, na askari namba B.6499 WDR Edmund Masaga (28) ambaye ni askari Magereza wilayani Bariadi. Kamanda MkmMbo alieleza kuwa baada ya askari hao kukamatwa mmoja wao PC Selemani Juma alipopekuliwa katika mfuko wa

LOWASSA AKUBALI YAISHE URAIS CCM

Image
Aliyekuwa waziri mkuu Edwad Lowasa SIKU moja baada ya Chama cha Mapinduzi (CCM), kumuonya aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa, kwa tuhuma za kukiuka Katiba na kuanza kampeni za Urais kabla ya muda, kiongozi huyo ameibuka na kudai kuwa hana njia ya kuwazuia watu wasimuombe agombee Urais. Pia Lowassa ametumia nafasi hiyo na kuwaomba wale wote ambao bado wana nia ya kumshawishi agombee nafasi hiyo ya urais, wasubiri kwanza hadi pale chama chake hicho kitakapotoa maelekezo. Akizungumza na vijana 60 wa bodaboda kutoka wilaya ya Mbarali, Mbeya waliokwenda pia kumshawishi agombee nafasi hiyo, mjini Dodoma jana, alisema si vyema kwa maofisa wa chama kuzungumzia masuala ya wanachama wao kwenye vyombo vya habari wakati kuna vikao vya chama. Alisema watu waliojitokeza na kumshawishi kuchukua fomu za kuwania nafasi hiyo ya Urais, hajawaita wala kuwalipa chochote kama inavyodaiwa na kwamba walikuwa wakifuata maneno ya Rais Jakaya Kikwete aliyoyatoa mkoani Ruvuma katika sherehe za ma

UKIJIFOSI KUMPENDA KISA MALI, PESA ZAKE, IMEKULA KWAKO

Image
Wakati fulani huwa najiuliza kwa nini tunakuwa na wapenzi, kwa nini mapenzi yakawepo? Kwa nini tunaoa ama kuolewa? Kwa nini baadhi ya watu huamua kujinyonga baada ya kuachwa na wapenzi wao? Kwa nini mapenzi yamekuwa sehemu ya maisha yetu?   Kwa nini mapenzi yameharibu baadhi ya maisha ya watu? Huwa najiuliza maswali mengi yenye kwa nini, yakihusisha mapenzi. Kwa ujumla kama nilivyo na maswali mengi, majibu pia yamekuwa mengi. Kwa vyovyote itakavyokuwa mapenzi ni sehemu ya maisha yetu na kwa hakika maisha yetu hayawezi kukamilika bila kuwepo mapenzi. Ninapozungumza juu ya mapenzi namaanisha yale yanayotoka moyoni mwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine. Mapenzi hayo, hukamilika baada ya wawili hao kuwa na hisia sawa za mapenzi. Amini kama upo katika uhusiano na mpenzi ambaye hakupendi, yaani wewe peke yako ndiyo unayempenda, wewe ni mtumwa wa mapenzi! Kama ndivyo, kwa nini uwe mtumwa? Unadhani hakuna mwingine ambaye anaweza kukupenda kwa mapenzi ya dhati na penzi hilo likawa kwa pan

TAARIFA KWA UMMA UVCCM TAIFA KUHUSU WAZIRI NYALANDU NA ZIARA ZA KATIBU MKUU WA CCM LIVE

Image

Messi ndiye mwanasoka tajiri duniani kwasasa upande wa makocha Jose Mourinho

Image
JARIDA LA SOKA LA NCHINI UFARANSA LIMETOA ORODHA YA WANASOKA NA MAKOCHA WENYE UTAJILI MKUBWA KWASASA ULIMWENGUNI,ORODHA HIYO KWA UPANDE WA WANASOKA INAONGOZWA NA LIONEL MESSI,UTAJILI HUO WA MESSI UNATOKANA NA JUMLA YA PESA ZOTE ANAZOZIPATA KUTOKANA NA MSHAHARA PAMOJA NA MIKATABA ALIYOSAINI NA MAKAMPUNI MBALI MBALI. wakati Messi akiongoza kwa mkwanja kwa upande wa makocha Mreno Jose Mourinho yeye anawakimbiza wenzake kwa kupata mkwanja mnono kutokana na kazi yake ya ukocha,Mourinho kwasasa ni kocha wa Chelsea ya ligi kuu ya Engla nd

MAGAZETI YA LEO ALHAMISI, MACHI 26

Image

CCM YAMUONYA TENA LOWASSA

Image
Katibu wa itikadi na uenezi CCM Nape Nnauye.  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimesema vitendo vinavyofanywa na Mbunge wa Monduli na Waziri Mkuu wa zamani Edward Lowassa ni ukiukwaji wa Katiba na kanuni za chama hicho. Aidha, kimesema vitendo vinavyofanywa na Lowassa ni kampeni za wazi za urais anazoendesha kabla ya muda kufika na hivyo kukiuka Katiba na kanuni za CCM na kuonya kuwa kama ataendelea na kampeni hizo haramu atapoteza sifa za kugombea nafasi ya urais. Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alitoa ufafanuzi huo baada ya waandishi wa habari waliopo katika msafara wa Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana kutaka ufafanuzi wa kinachoendelea mjini Dodoma kwa makundi tofauti kwenda kwa Lowassa kwa madai ya kumshawishi agombee urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu. Nape akizungumzia suala hilo alisema, “Anachokifanya Lowasa ni kuvunja kanuni na kiburi, ni matendo ya wazi ya kampeni, bila shaka anajua adhabu yake. Matendo hayo yanaweza kumpotezea sifa za kuwa

Rais Kikwete alipokanyaga mitaa ya Buguruni Kwa Mnyamani kukagua walioathiriwa na mvua

Image
Ziara hii ilifanyika huko Buguruni Kwa Mnyamani, wilayani Ilala, Dar es salaam siku ya Jumanne, Machi 24, 2015

Rais Kikwete alipokanyaga mitaa ya Buguruni Kwa Mnyamani kukagua walioathiriwa na mvua

Image
Ziara hii ilifanyika huko Buguruni Kwa Mnyamani, wilayani Ilala, Dar es salaam siku ya Jumanne, Machi 24, 2015

TAHADHARI YA WIZARA KUHUSU UTAPELI WA AJIRA YA WALIMU WAPYA 2015/2016

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI TAARIFA KWA UMMA KUHUSU AJIRA YA WALIMU WAPYA WA SHULE ZA MSINGI, SEKONDARI NA VYUO VYA UALIMU MWAKA 2015/16 JIHADHARI NA MATAPELI Kumekuwepo na Tangazo la upotoshaji kuhusu Ajira ya walimu wapya kwa mwaka 2015/16 (TANGAZO No. T.022/15TMS 2015) linalodaiwa kuwa limetolewa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na kusambazwa kwenye Mitandao ya Kijamii. Taarifa zilizotolewa katika tangazo hilo siyo za kweli na Wizara haihusiki nazo. Aidha, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi inapenda kuufahamisha umma kuwa ajira ya Walimu wa ngazi ya Cheti, Stashahada, na Shahada hufanywa na Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI baada ya kupata kibali cha Ajira kutoka Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma. Hivyo Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi haihusiki moja kwa moja na zoezi hilo. Kutokana na mgawanyo wa majukumu ya Wizara mbalimbali, taarifa sahihi kuhusu ajira mpya za walimu kwa mwaka huu wa fedha zitatang

Vyuo Vikuu Mbeya wamtaka Prof. Mwandosya awanie Urais

Image
Idd Mambo (katibu Itidadi na Uendezi, Chuo Kikuu TEKU) akimkaribisha mtoaji tamko hilo Shirikisho la Vyuo Vikuu mkoani Mbeya limefaya kongomano lililohusu uchaguzi mkuu lililofanyika katika ukumbi wa Benjamini Mkapa jijini hapa na kuchukua nafasi hiyo ya kumshawishi Prof. Mark Mwandosya kugombea nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu huu. Akisoma tamko loa wanazuoni hao mbele ya waandishi wa habari, Katibu wa shirikisho hilo Oscar Mwaihabi kutoka Chuo Kikuu cha Tumaini amesema wamefikia uamuzi huo baada ya kuona ndani ya chama hicho hakuna kiongozi mwenye sifa ya kufanana na Prof. Mwandosya na hivyo wameona Tanzania ijayo iongozwe na kiongozi huyo. “Sisi wanazuoni tumeona kuwa wewe Prof. Mark J. Mwandosya unafaa kabisa kupokea kijiti cha Urais kutoka kwa Jakaya Kikwete kwa kuwa unafaa na ni tofauti na wengine wote waliojitokeza kutangaza nia katika Chama Cha mapinduzi kutokana na uongozi uliowahi kushiriki. Hujawahi kupata tuhuma yoyote mpaka