Posts

viwango vipya vya soka.... Brazil yashuka

* Hispania yashika ukanda, Tanzania yazidi kuzama ZURICH, Uswisi BRAZIL imeporomoka kwa nafasi mbili kwenye ubora wa viwango vilivyotolewa jana na Shirikisho la Soka la Kimataifa, FIFA, huku Hispania ikishika ukanda ikifuatiwa na Uholanzi. Mabingwa hao wa dunia mara tano, walikuwa wakishika namba moja kwenye chati hizo za FIFA tangu April 2010 imeporomoka ikiwa ni baada ya matokeo mabaya ya Fainali za Kombe la Dunia zilizofanyika Afrika Kusini. Brazil iliondoshwa na Uholanzi katika mechi ya robo fainali kwa kufungwa mabao 2-1 ambayo ilikuwa ikishika nafasi ya nne kabla ya kupanda nafasi ya pili kwenye viwango hivi vipya vya Fifa. Uholanzi ilifungwa bao 1-0 na Hispania kwenye fainali. Kwa mujibu wa viwango hivyo vipya vya Fifa, Tanzania imeshuka kwa nafasi nne kutoka nafasi ya 108 ambayo ilikuwa ikiishikilia mwezi Aprili mpaka nafasi ya 112. Januari mwaka huu, Tanzania ilikuwa nafasi ya 108 sawa na Februari kabla ya kushuka kwa nafasi moja hadi 109 mwezi Machi. Ilipanda tena kwa nafasi

The place To be In Musoma Town

Image
MASERO INN hii ni Hotel Masero inn inayopatikana pale maeneo ya mtaa wa Mukendo karibu kabisa na club Metropole,asante Mdau Rogers kwa picha hii wadau wamekupata,usikose kupata Lunch yako pale na kila haina ya madikodiko

Mpendazoe agombea ubunge kwa Chadema

Image
Viongozi wa CCJ wakikabidhiwa kadi na Mwenyekiti wa Chadema CHAMA Cha Jamii (CCJ) kimeondokwa na vigogo wake na waanzilishi kadhaa wake akiwamo msemaji wake mkuu, Fred Mpendazoe aliyetangaza kugombea ubunge kwa tiketi ya Chadema. Mwenyekiti wa chama hicho Richard Kiyabo, naibu Katibu Mkuu Nickson Ng'ihily na Msemaji wa Chama, Fred Mpendazoe jana walikabidhiwa kadi za Chadema jijini Dar es Salaam na mwenyekiti Freeman Mbowe. Muda mfupi baada ya kupokea kadi hizo, viongozi hao walitangaza nia ya kugombea ubunge katika majimbo tofauti nchini kwenye Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu. Fred Mpendazoe ambaye mwanzoni mwa mwaka huu aliacha ubunge, kuihama CCM na kujiunga na CCJ, ametangaza kuwania ubunge wa Jimbo la Segerea, Richard Kiyabo anaenda Bukene na Ng'ihily anagombea Jimbo la Temeke. Jimbo la Segerea pia linawaniwa na Dk Makongoro Mahanga wa CCM. Kabla ya kujiunga na CCJ, Mpendazoe alikuwa mbunge wa Jimbo la Kishapu mkoani Shinyanga kupitia CCM. Akizungum

MUNGU WANGU.....HUJAFA HUJAUMBIKA

Image
OMG!!!!! Take Heart. Hujafa hujaumbika Hii ndiyo ajali iliyoangamiza zaidi ya watu 230 DRC baada ya gari la mafuta kupinduka.ili ni fundisho kwetu magari yanayobeba mafuta siyo ya kukimbilia Habari hii ni kutoka tovuti ya www.u-turn.co.tz

DAWA YA UKIMWI YAPATIKANA !!!

WANASAYANSI nchini Marekani wamegundua chembechembe za kinga ambazo zinauwezo mkubwa wa kupambana na kuua virusi vya ugonjwa wa Ukimwi ambao hadi sasa hauna chanjo wala tiba ya uhakika. Ugunduzi huo tayari umethibitishwa na wataalamu mbalimbali, ikiwemo Mamlaka ya Chakula na Dawa ya Marekani. Vyombo mbalimbali vya habari vya kimataifa vimeripoti kuhusu ugunduzi huo ambao unaelekea kutoa mapambazuko mapya kwa ugonjwa huo hatari ambao umekuwa ukiathiri nguvu kazi sehemu mbalimbali duniani, hususan nchi zinazoendelea. Wanasayansi hao wa Taasisi ya Magonjwa ya Kuambukiza na Mzio (Niaida) walieleza katika taarifa yao ya wiki iliyopita kuwa kwenye utafiti huo wamebaini aina mbili za chembechembe zinazoweza kumsaidia binadamu kupambana na virusi vya ukimwi. Mkurugenzi wa Niaida, Dk Anthony Fauci alizitaja chembechembe hizo za kinga kuwa ni VRCO1 na VRCO2 ambazo utafiti wake umeonyesha kuwa zinaweza kuua virusi vya ukimwi kwa asilimia 90. Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO) dawa huthib

REDNAPP HADI MWAKA 2013

Image
Redknapp Meneja wa klabu ya Tottenham Harry Redknapp ameongeza mkataba wa kuendelea kukinoa kikosi cha klabu hiyo mpaka mwaka 2013. Mzee huyo mwenye umri wa miaka 63 ameongeza mkataba huo huku akiwa ameifanyia makubwa klabu hiyo ambayo msimu ujao itashiriki kwenye michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya baada ya kumaliza katika nafasi ya nne kwenye msimamo wa ligi kuu ya soka nchini Uingereza. Hatua hiyo ya kuamiliwa na mabosi wake na kupewa mkataba mpya imemkuna sana Harry Redknapp ambae anadai huenda imeshababishwa na utawala mzuri alionao katika kikosi chake ambapo mara kadhaa amekua akiwaeleza ukweli wachezaji wake. Kabla ya kusaini mkataba mpya, mkataba wa zamani wa miaka miwili wa Harry Redknapp ulikuwa unatarajia kufikia kikomo mwaka ujao.

Azam FC yatangaza 22: Wapya 8, Waachwa 10

Klabu ya soka nchini, Azam FC inayoshiriki ligi kuu soka ya VodaCom Tanzania Bara imetangaza usajili wa wachezaji ishirini na wawili, wanane kati yao wakiwa wapya huku kumi wa kikosi kilichopita wakiachwa. Picture Said Mohammed Abeid / Mwenyekiti - Azam FC Katika taarifa iliyomo katika tovuti ya klabu hiyo, wachezaji wapya waliosajiliwa na timu hiyo ni Mohamed Binslum (Huru), Jackson Chove (JKT Ruvu), Jabir Aziz na Ramadhan Chombo 'Redondo' (Simba), Mrisho Ngasssa (Yanga), Kalimangonga Sam Daniel Ongala Rampling 'Kali Ongala' (GIF-Sweeden), Patrick Mutesa Mafisango (APR- Rwanda) na Peter Senyonjo (Polisi-Uganda). Wachezaji waliobaki ni John Bocco, Erasto Nyoni, Jamal Mnyate, Salum Aboubakar 'Sure Boy', Vladmir Niyonkuru, Philip Alando, Luckson Kakolaki, Malika Ndeule, Aggrey Morice, Salum Swed, Ibrahim Shikanda, Ally Manzi, Seleman Kasim 'Selembe' na Ibrahim Mwaipopo. Wachezaji waliopanda toka timu ya vijana 'Azam Academy' ni sita ambao ni Sino A

Justin Bieber - Somebody To Love Remix ft. Usher

SPAIN MABINGWA WAPYA KOMBE LA DUNIA

Image
Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini pamoja na Rais wa Fifa,Sepp Blatta wakiwa na mabingwa wapya wa Dunia mara baada ya kuwakabidhi kikombe chao cha ubingwa walioupata kwa kuitungua timu ya Taifa ya Uholanzi bao 1-0 lililofungwa na mchezaji Andres Iniesta dakika nne tu kabla ya mechi kumalizika.

Ajali ya lori yaua watano mkoani Rukwa

Watu watano wamekufa papo hapo na wengine kujeruhiwa baada ya lori walilokuwa wakisafiria kushindwa kupanda mlima Lukangao na kupinduka. Ajali hiyo ilitokea juzi saa kumi na moja jioni katika kijiji cha Ntendo, Sumbawanga mkoani Rukwa. Gari hilo ni lori aina ya Scania lenye namba za usajili T 347 ATX ambalo ni mali ya mfanyabiashara Khalid Salum Abdallah, lililokuwa likiendeshwa na Abeid Said (32), mkazi wa Mazwi. Wakati likipata ajali, lori hilo lilikuwa limebeba zaidi ya magunia ya mpunga 80 pamoja na watu 10 waliokuwa wamekaa juu wakitokea kijiji cha Majimoto wilayani Mpanda. “Wakati likipanda mlima, lilipata pancha na hivyo kupoteza mwelekeo na kupinduka na watu kupoteza maisha,” alisema Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Rukwa, Isunto Mantage. Kamanda Mantage aliwataja waliokufa kwenye ajali hiyo kuwa ni mwanafunzi wa Sekondari ya Karema, Lucy Andrew (24), Fumbuka Elias (28), Mayunga Mathias (30), na wengine wawili ambao bado hawajatambuliwa. Majeruhi waliotajwa ni Athanas Choka (26), N

SHYROSE BHANJI KUGOMBEA UBUNGE KINONDONI • 2010

Image
Shy-Rose Sadruddin Bhanji Kada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Shy-Rose Sadruddin Bhanji ametangaza kujitosa katika nafasi ya ubunge jimbo la Kinondoni jijini Dar es Salaam kupitia CCM na lengo lake kubwa ni kuwa kiungo muhimu katika jamii ya wanakinondoni. Akitangaza azma yake ya kuomba ridhaa kwa wanachama wa CCM katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, Shy-Rose alisema kwa mtazamo wake neno ubunge kwa mwaka 2010 linahitaji tafsiri mpya kabisa. `…kwa sasa mbunge anatakiwa kuwa ni kiungo cha jamii badala ya kuwa mwakilishi wa jimbo kama ilivyozoeleka` alifafanua Shy-Rose. `Mwaka 2010 ni mwaka wa mabadiliko na ndio maana nimeona kwamba ili kila mwananchi kuweza kuwajibika, nafasi ya mbunge inahitaji kutafsiriwa upya ili iendane na wakati na matatizo ambayo yanayotukakabili wananch` alisema. Kwa maana hiyo amesema kwamba hata sifa za mbunge zinahitaji kutafsiriwa upya kabisa, kwani majukumu yake yamebadilika kuendana na wakati. Ametaja baadhi ya sifa hizo mpya ni kuwa mhamasishaji, kiung

WACHEZAJI 70 WACHAGULIWA KUUNDA TIMU YA SERENGETI BOYS

Image
Zaidi ya wachezaji sabini wateuliwa kuunda timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17. Zaidi ya wachezaji sabini wameteuliwa kuunda timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 SERENGENTI BOYS kutoka katika mashindano ya COPA COCA COLA ambayo tayari yameingia katika hatua ya nusu fainali. Kocha masaindizi wa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 SLYVESTER MASHI amesema vijana wanaoshiriki mashindano ya mwaka huu ya COPA COCA COLA wameonyesha vipaji vya hali ya juu na ni hazina kwa taifa Mashindano ya COPA COCA COLA yameingia katika hatua ya NUSU FAINALI kwa mchezo mmoja kati ya KINONDONI na MJINI MAGHARIBI wakati kesho KIGOMA inateremka dimbani kuivaa TEMEKE