Posts

Sasa wateja wa CRDB na Vodacom M-PESA wanaweza kuweka na kutoa pesa

Wateja wa Vodacom M-PESA wenye akaunti katika benki ya CRDB sasa wanauwezo wa kuweka na kutoa fedha kutoka katika akaunti zao kupitia simu ya mkononi ya Vodacom iliyosajiliwa na huduma ya M-PESA. Kuzinduliwa kwa huduma hiyo sasa kunawapa urahisi zaidi wateja wa Vodacom M-PESA kuweka na kuchukua fedha zao kutoka akaunti ya benki kwa urahisi na unafuu zaidi mahali popote nchini na kwa wakati wowote pasi na kulazimika kufika katika tawi la benki ya CRDB.. Huduma hii ya ushirikiano kati ya Benki ya CRDB na kampuni ya Vodacom kupitia huduma yake ya M-PESA ni ya kwanza nchini na inalenga kuwaondolea usumbufu wateja wa M-PESA wa kupanga foleni ama kutembea umbali mrefu kufuata tawi la Benki. “Tunapoitambulisha huduma hii mpya inaamaanisha kwamba tumeongeza thamani nyengine katika simu ya mkononi na huduma ya Vodacom M-PESA.Mteja wa M-PESA kuweza kutoa na kuchukua fedha kutoka akaunti zao za CRDB kupitia simu zao za mkononi ni hatua nyengine muhimu ya kujivunia kuwa mteja wa

HUYU NDIO BIBI ANAERAP NA KUIMBA

Image
Wakati nikisikiliza xxl leo huyu bibi kanivutia sana ukiangalia umri wake na nyimbo anazoimba hapo ndo utajua kuwa kama kipaji kipo basi kipo tuuuu na kamwe hakipotei picha na story hapo chini ni kutoka website ya www.millardayo.com huyu ndio bibi ambae ana rap na kuimba, maajabu yake ameyaonyesha kwenye XXL ya CLOUDS FM leo, stori kamili nitaiweka baadae kidogo hapa hapa millardayo.com na itasikika pia kwenye AMPLIFAYA. ana umri wa miaka 51, na mpaka sasa hajapata jina la kisanii la kutumia, track yake ya kwanza ameitoa leo kafanya na MH TEMBA

HAPPY BIRTHDAY RICHARD MFINANGA

Image
happy birthday my classmate Rich wish all da best in ur life and work hard so that u will reach to ur intended goals

LIGI KUU YA VODACOM KUANZA JUMAMOSI

Image
Bw.Boniface Wambura Ofisa HabariShirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Mzunguko wa pili wa Ligi Kuu ya Vodacom kuwania ubingwa wa Tanzania Bara unaanza keshokutwa (Januari 21 mwaka huu) kwa mechi nne. Moro United itaikaribisha Yanga kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na Mtibwa Sugar itaoneshana kazi na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Manungu, Turiani. Nayo Toto Africans itakuwa mgeni wa Ruvu Shooting kwenye Uwanja wa Mlandizi mkoani Pwani na Villa Squad itapambana na Kagera Sugar katika Uwanja wa Azam Chamazi, Dar es Salaam. Januari 22 mwaka huu JKT Ruvu na Polisi Dodoma zitapepetana Uwanja wa Azam Chamazi wakati Januari 22 mwaka huu Dar es Salaam itakuwa na mechi mbili; African Lyon na Azam (Uwanja wa Azam Chamazi) na Simba na Coastal Union (Uwanja wa Taifa). Ratiba kwa ajili ya waamuzi na makamishna kwa mechi 35 za mwanzo tayari imeshatoka. Waamuzi wa kati 16 wameteuliwa kuchezesha mechi hizo huku watatu

AJIRA MPYA YA WALIMU WA SHULE ZA SEKONDARI WENYE ELIMU YA SHAHADA MWAKA 2011/12

http://www.moe.go.tz/pdf/AJIRA%20MPYA%20YA%20WALIMU%20WA%20SEKONDARI%20-%20SHAHADA%202011-2012%20Final.pdf CLICK LINK HIYO HAPO JUU KUWEZA KUYATAZAMA.

NAIBU WAZIRI MWANRI AIKATAA NYUMBA ILIYOKARABATIWA KIFISADI ,ASEMA LUDEWA SI SHAMBA LA BIBI

Image
Ziara ya ghafla ya naibu waziri Mwanri kwenda kufichua ufisadi wa kutisha Lupanga kwa kukataa nyumba ya mganga iliyochakachuliwa ujenzi wake Hii ni nyumba mpya ambayo bado inajengwa ila inavuja mabati yamechakaa kabla ya kuanza kutumika ipo Lupanga Ludewa ,naibu waziri hapa akitamani kutoa machozi kwa wizi huu wa kutisha Hii ni nyumba mpya ambayo bado haijakamilika kujengwa ila imechoka mbaya haina tofauti na pagale Maajabu nyumba mpya ya mganga Lupanga Ludewa imechakaa kabla ya kuanza kutumika imekarabatiwa kwa Tsh,milioni 7 za serikali kupitia mradi wa Mamu Hizi ndizo bati zenyewe zikiwa zinavuja kupitia kiasi,kweli Ludewa ni shamba la bibi Kuta za nyumba hiyo kwa nje zikiwa zimepigwa lenda ila ndani lenda hakuna NAIBU waziri wa nchi ofisi ya waziri mkuu anayeshughulika na serikali za mitaa na tawala za mikoa (TAMISEMI) Aggrey Mwanri amevunja ratiba iliyoandaliwa na viongozi wa wilaya ya kumtembeza katika miradi isiyo na matatizo na ku

WALIMU WAFICHA WANAFUNZI KICHAKANI BAADA YA KUFUMWA NA NAIBU WAZIRI WAKITUMIKISHA WANAFUNZI

Image
Mwalimu wa shule ya msingi Luilo kata ya Lifua wilaya ya Ludewa mwalimu Mgaya akipita katika eneo ambalo wanafunzi walikuwa wakilima na kuacha majembe na kukimbia kujificha Msafara wa naibu waziri wa tamisemi Aggrey Mwanri ukipita eneo ambalo wanafunzi walikuwa wakilima Naibu waziri wa Tamisemi akiwahoji walimu na wanafunzi waliokuwa wakiwatumikisha watoto wa shule mida ya masomo leo Mwanafunzi wa shule ya Msingi Luilo Ludewa akiwa amebeba majembe baada ya naibu waziri wa Tamisemi Aggrey Mwanri kuagiza warudi madarasani leo asubuhi Wanafunzi wa shule ya Msingi Luilo Ludewa wakiwa wamejificha katika kichaka pamoja na walimu wao kumkwepa naibu waziri wa Tamisemi Aggrey Mwanri leo Wanafunzi wa shule ya msingi Luilo kata ya Lifua wilaya ya Ludewa wakilima shamba la shule mida ya masomo majira ya saa 3 asubuhi leo baada ya kufanya ziara ya ghafla eneo hilo BAADA ya naibu waziri ofisi ya waziri mkuu Tamisem

FACEBOOK SONG BY DJ CLEO

Image
dj cleo - facebook .mp3 Found at bee mp3 search engine

KWELI WANAFUNZI WANAMBINU KIBAO ZA KUEPUKA SUPPREMENTARY

Image
Basi unaambiwa usicheze na binadamu kwenye kugundua mbinu za kila aina ili asiweze kufail mtihani......sio Mtanzania lakini ona mambo anayoyafanya kwenye chumba cha mtihani......angusha comments zako mdau.

OPPORTUNITY

Ulimwengu wa Internet unabadilika kila siku....wapo wanaoneemeka na wapo mazuzu wanaoibiwa kwenye mitandao kutokana na uchanga wao kwenye mambo ya Internet. Hivi sasa kuna kitu imeanzishwa; jaribu kugonga hapa Ulimwengu wa Internet unabadilika kila siku....wapo wanaoneemeka na wapo mazuzu wanaoibiwa kwenye mitandao kutokana na uchanga wao kwenye mambo ya Internet. Hivi sasa kuna kitu imeanzishwa; jaribu kugonga hapa http://signup.wazzub.info/?lrRef=64b9e   ili upate maelezo zaidi. Kwa kifupi, huo ni mtandao sawa na Google, Yahoo, Facebook au mtandao mwingine wowote unaoufahamu! Tofauti iliyopo ni kwamba, waanzishaji wa mtandao huu wanadai kwamba kwa wale watakaojiunga nao(members), watakuwa wanalipwa malipo kutokana na matangazo yatakayopatikana kwenye mtandao huu! Wapo, wanaoamini kwamba jambo hilo ni la kweli (kwamba members watalipwa) na wapo ambao hawaamini kabisa! Binafsi, ninaamini kwamba, ktk dunia hii lolote linawezekana! Unachotakiwa kufanya ni umakini wako tu

Mvua inanyesha, wao wapo tu wamsikiliza Dkt. Slaa

Image
  Ama kwa hakika siasa ni zaidi ya itikadi na ufuasi, kwa wengine ni sawa na dini kabisa. Kweli siasa sasa imewakolea baadhi ya Watanzania kiasi kwamba sasa wanataka kusikia kwa masikio yao wenyewe si kuambiwa, na kushuhudia kwa macho yao wenyewe na siyo kuhadithiwa liwake jua, inye mvua, wamedhamiria! Sasa jama isiwe sababu, kila chama kitake kwenda kuhutubia mvua itakaponyesha, maana watu kwa sayansi iliyozidi maarifa hawakawii kuitisha mvua ili mkutano wao nao uwe na picha zenye matone matone ya mvua, LOL, taratibu jama. Picha zinazoonekana hapo zimetoka kwenye blogu ya  Mbeya Yetu .

Anatafutwa kwa kutokomea na fedha za michango ya harusi

Maisha magumu, ukapa mifukoni umekolea kweli kweli kwa wananchi, hadi kulazimika kuiba michango ya harusi? Eh! Jeshi la Polisi Mkoani Singida linamtafuta mhasibu wa kitengo cha mishahara wa Halmashauri ya Wilaya ya Singida, Imani Abduli, anayetuhumiwa kutoweka na sh milioni sita zilizochangwa kwa kwa ajili ya harusi ya mmoja wa askari wake. Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na baadhi ya watumishi wa ofisi ya mkurugenzi mtendaji wa wilaya hiyo zinasema kwamba alitoweka na kiasi hicho cha fedha siku mbili baada ya kikao cha mwisho cha maandalizi ya harusi hiyo kilichofanyika siku mbili kabla ya harusi.