Mwaka 2011 ulikuwa mzuri katika nyanja kadhaa za TZhiphop na miradi mingine , ingawa, kama kawaida, changamoto za hapa na pale hazikosekani. Kwa upande wa wasanii, kwa ujumla wale chipukizi walioanza kusikika mwaka 2010 waliweza kujikita kwenye masikio na nyoyo za wengi. Mwamko wa mashabiki wanaoongezeka ni ushahidi thabiti. Kwa upande mwingine, tunapenda kuwaasa mashabiki pamoja na wasanii waendelee kujifunza kuhusu historia na misingi ya Hip Hop . Mwaka 2012 bila shaka unaonekana utakuwa mzuri zaidi. Wale waliochomoza mwaka 2010 na kufanya vizuri mwaka 2011 wanapevuka. Vivyo hivyo, wale walioanza kusikika mwaka 2011 wanaelekea kuzuri! Wasanii wanne chipukizi wanaojitegemea wameamua kuunganisha vichwa na kuunda Miraba Minne, chini ya uongozi wa mtayarishaji wa ala, Ray. Ndani ya Miraba Minne kuna Maalim Nash (alikuwa anatumia jina ‘Nash MC’), P The MC , msanii mpya ndani ya M-Lab , Songa , na ZAiiD … Kaa tayari kupokea mixtape yao kwa mikono miwili . Tunatambul