Maelezo ya Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii kuhusu hoja za madaktari

Utangulizi

Uongozi wa Wizara umekuwa ukifanya vikao mbalimbali na Viongozi wahusika wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) katika kutatua suala la Madaktari wanaofanya mazoezi kwa vitendo (internship) na hatimaye suala hili kumalizika. Baadaye MAT waliwasilisha Hoja nane za ziada Tarehe 21/01/2012. Wizara ilifanya mkutano na Uongozi wa Chama cha Madaktari kujadili hoja zilizowasilishwa. Wizara ilitoa maelezo kama ifuatavyo:-

Madaktari kupewa nyumba za kuishi karibu na Hospitali

Serikali kupitia Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Ofisi ya Rais, Menejiment ya Utumishi wa Umma na WIzara ya Fedha inarekebisha Waraka uliotolewa kwa Taasisi kuhusu ani anastahli kupewa nyumba, ili Madaktari waendelee kupatiwa nyumba bila kujali ngazi zao za mishahara.

Pamoja na juhudi zinazofanywa na Mikoa na Halmashauri kuwapatia Nyumba Madaktari, Serikali imepata fedha kutoka Mfuko wa Dnia  (Global Fund) kwa ajili ya kujenga nyumba za Madaktari kwa kuanzia Wilaya 18 zilizo pembezoni zimechaguliwa kujengewa nyumba nane 98) kila Wilaya kama sehemu ya kuboresha hali ya upatikanaji wa nyumba kwa Madaktari.


Kuongeza posho ya kuitwa kazini baada ya saa za kazi  (on call allowance)

Wizara imefanyia kazi, maboresho ya pohso hiyo ya kuitwa kazini baada ya saa za kazi (On call allowance), na imewasilisha kwa mamlaka husika, kwa ajli ya kupata kibali. Mapendekezo hayo, yanatofautisha posho hiyo kulingana na ngazi za Madaktari na watumishi wengine.

Rufaa za wagonjwa (hasa viongozi) wanaopelekwa kutibiwa nje ya nchi

Malalamiko ya Madktari ni kwamba baadhi ya Viongozi wa Kisiasa na wa Serikali hushinikiza Daktari anayewahudumia awape rufaa ya kwenda kutibiwa nje ya nchi hata kwa magonjwa yanayoweza kutibiwa hapa nchini.

Maelezo ya Wizara ni kwamba Wizara hugharamia matibabu nje ya nchi kwa Watanzania wote bila kujali hali zao za kijamii au kisiasa ili mradi vigezo vimetimizwa. Wizara hupokea rufaa za wagonjwa hao, ambazo zimetokana na ushauri wa Jopo la Madaktari bingwa wa fani husika wasiopungua watatu.  Madaktari hao baada ya kuwachunguza wagonjwa na kuamua kuwa wanahitaji rufaa huandika majina yao na fani zao katika fomu za rufaa husika. Madaktari hao wana uhuru wa kuandika katika fomu ya rufaa kama mgonjwa anastahili kupelekwa nje ya nchi au anaweza kutibiwa hapa nchini na kwa hiyo hamna ulazima wa kumpelekea nje ya nchi.

Hata hivyo katika kipindi cha miezi mitatu (Oktoba hadi Desemba 2011) jumla ya Wagonjwa 223 walienda nje kwa ajli ya matibabu, kati ya hao ni awgonjwa 19 (8.5%) tu walikuwa viongozi wa Serikali na Siasa (Waheshimiwa Wabunge na Viongozi waandamizi Serikalini).

Majina kwa ajili ya udhamini wa madaktari wanaochukua mafunzo ya Uzamili

Malalamiko ya Madaktari ni kwamba baadhi ya Madaktari waliopata nafasi ya kuchukuwa mafunzo ya Uzamili katika Vyuo mbalimbali kukosa udhamini wa Wizara.

Hapo awali ni Madaktari 50 tu kwa mwaka ndiyo walipata udhamini kwa mafunzo ya Uzamili. Baada ya kuanza uktekelezaji wa Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi (MMAM), hapo 2007, idadi hiyo iliongezeka na kufikia Madaktari 300 kwa mwaka. Hii iliwezekana kutokana na Serikali kuwa na fedha za kutosha kutokana na ufadhli wa Benki ya Dunia. Mwaka jana ufadhili huu haukuwepo na hali ya fedha haikuwa nzuri, kiasi kwamba, ilielekezwa kupunguza bajeti. Fedha iliyobaki ilitosha kudhamini Madaktari 50 tu. Wizara inafanya jitihada za kutafuta fedha zkwa ajili ya udhamini wa Madaktari waliokosa udhamini. Tayari baadhi ya Wadau wa Maendeleo wako tayari kwa hili.

Kuhamisha Madaktari Bingwa wenye mikataba ya Ajira na Hospitali ya Taifa Muhimbili

Wizara kuwahamisha Madaktari Bingwa iliyoingia nao mkataba wa udhamini wa masomo ya uzamili na wakati huo huo wakiwa na mikataba ya ajira na Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Wizra imekwisha rekebisha kasoro ya mikataba hiyo. Hospitali ya Taifa Muhimbili tayari inatumia mikataba mipya inayoonesha kuwa daktari akipata ufadhili wa Wizara atapangiwa kutuo kulingana na mahitaji ya taifa.

Baada ya Serikali kupandisha hadhi ya hospitali za Mikoa kuwa Hospitali za Rufaa na Mikoa, ni muhimu sana kwa Madaktari Bingwa kwenda kufanya kazi katika hospitali hizo. Daktari Bingwa ndiye anayepaswa kuwa kichocheo cha kuifanya Hospitali husika ipate rasilimali zinazotakiwa (vifaa, watumishi, majengo na fedha). Aidha ataifanya hospitali hiyo itoe huduma zinazotakiwa. Hii ni kulingana na Sera ya Afya na Mpango wa Maendeleo ya Afya ya Msingi (MMMAM). Mpango Mkakati wa Afya Na. 3 aunaozipandisha hadi Hospitali za Mikoa kuwa Rufaa, ili kuongoza huduma za uningwa karibu na wananchi.

Posho ya mazingira hatarishi (Risk Allowance)

Hapo awali, Seirkali ilijumuisha posho mbalimbali kwenye mishahara ya watumishi, piosho ya mazigira hatarishi ikiwa ni mojawapo ya posho hizo. Hata hivyo, Serikali imetambua umuhimu wa kuzitenganisha posho hizo na mishahara kwa watumishi wa kada za afya wanaofanya kazi katika mazingira hatarishi. Wizara kwa kushirikiana na mamlaka  husika wanalifanyia kazi suala hili.

Ajira za Madaktari

Wizara imewaajiri Madaktari wote walioomba kuajiriwa. Tatizo kubwa ni kwamba wengi wa Madaktari hao hawaendi kule wanakopangiwa kwa kuwa wanapenda kbaki Dar es Salaam, ambapo hata hivyo nafasi ni chache. Ilikubalika kuwa MAT na vyama vingine vya kitaaluma viwe ni wadau katika kutoa taarifa kwa Madaktari na Wataalamu wengine kuhusu kuwepo kwa nafasi za ajira za Madaktari.

Aidha Serikali imekuwa ikiongeza nafasi za ajira za watumishi wa kada za Afya kutoka nafasi 1,677 mwaka 2005/2008 hadi kufikia nafasi 9.391 kwa mwaka wa fedha 2011/2012.

Kutaka Mshahara wa Shilingi Milioni 3.5 kwa mwezi

Mishahara ya watumishi wa Serikali, hufuata Miundo ya Utumishi (Scheme of Service) iliyopo. Aisha, serikali imeboresha muundo wa watumishi wa sekta ya afya. Baada ya kuboreshwa kwa muundo huo, kwa hivi sasa, Watumishi wa afya wanapata mishahara mikubwa kuliko watumishi wengine serikalini.

Wito kwa Madkatari walio katika mgomo

Wakati serikali inashughulikiwa hoja za Madaktari, Wizara inatoa wito kwa Madkatari wote kurudi na kuendelea kufanya kazi za utabibu ili kuokoa maisha ya Watanzania, kama tulivyokubalina katika kikao na viongozi waliokuja Wizarani tarehe 21/01/2012.

Ni vyema Madaktari wakatambua juhudi zinazofanywa na serikali, za kuboresha maslahi ya watumishi wa sekta ya afya, kama ilivyoelezwa hapo juu, na kuziunga mkono.

Hata hivyo, serikali inatamka kuwa, milango iko wazi ya kujadili masula ahaya, na wataalamu wote wa sekta ya afya.

Asanteni kwa kunisikiliza

Imetolewa: 26/01/2012

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA