Taarifa za kuwepo chuo feki nchini Tanzania
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania imepokea taarifa kupitia matangazo yanayotolewa na chuo kinachojiita “Japan Bible Institute Graduate School of Theology” kikijitangaza kwamba kinatoa shahada mbalimbali za uzamivu (PhD) kwenye nyanja za dini na jamii. Chuo hiki kinajitangaza kwamba kinawakilisha tawi la taasisi iliyopo nchini Marekani na kwamba makao yake makuu kwa bara la Afrika yapo Dar es Salaam, pamoja na kwamba eneo halisi ofisi zao zilipo haijaelezwa kwenye matangazo yao. Tume inachukua fursa hii kuuarifu umma kwamba chuo hiki hakitambuliki kwa mujibu wa sheria na kwamba wamiliki wa Japan Bible Institute Graduate School of Theology hawana kibali cha kutoa elimu ya chuo kikuu ambayo inatambuliwa hapa nchini. Tume inatoa tahadhari kwa umma kuepuka ulaghai ambao unafanywa na watu katika eneo hili la elimu ya juu na hivyo umma unashauriwa kuchukua tahadhari kwani vyeti watakavyotolewa havitambuliwi na Tume na hivyo haviwezi kutumika hapa nchini. Pia, wamiliki wa chuo hik