LILIAN INTERNET ATIMKIA MASHUJAA BENDI


BENDI ya muziki wa dansi ya Mashujaa Musica imezidi  kuibomoa bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta’ baada ya kumyakua  mnenguaji wake mahiri,Lilian Tungaraza maarufu kama ‘Intanet’.
 Meneja wa Mashujaa Band Maximilian Luhanga alisema kwamba wamweamua kuwachukua wanamuziki hao ili kuimarisha bendi yao katika idara hizo na tayari wameshasaini mkataba wa kuitumikia bendi hiyo kwa miaka miwili ambao onyesho la utambulisho linatarajiwa kufanyika jumatano ijayo katika ukumbi wa Nyumbani Lounge.
 Hii ni mara ya pili kwa Mashujaa kuibomoa Twanga Pepeta ambapo mapema mwaka huu ilimyakua mmoja ya waimbaji mahiri, Charlz Gabriel ‘Chaz Baba’..Kwa hisani ya Mama Pipilo Blog

Comments

Popular posts from this blog

PATA UKWELI KUHUSU MWANAMALUNDI, MTU WA MAAJABU ALIYEWAHI KUTOKEA KATIKA HISTORIA YA KABILA LA KISUKUMA